Nini mtazamo wako kuhusu kuongezeka kwa kasi kwa wachekeshaji Tanzania?

Nini mtazamo wako kuhusu kuongezeka kwa kasi kwa wachekeshaji Tanzania?

Bila shaka utakubaliana nami kwamba, kwa kipindi Cha hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la comedians Tanzania ukilinganisha na miaka ya nyuma kidogo, zamani comedian wengi walikuwa agego, yaani wenye umri mkubwa kidogo japo hata Vijana wachache walikuwemo.

Lakini ni tofauti kabisa na Sasa, siyo watoto, Vijana mpaka wazee wamekuwa comedian na wengi wamewekeza kwenye social media. Ni jambo zuri maana imesaidia watu wengi kujiajili.

Hoja yangu ya msingi ni, kwanini kumekuwa na ongezeko kubwa la comedian Tanzania? Je, ndiyo kusema kwamba maisha magumu yanayosababishwa na ukosefu wa ajira rasmi imewafanya watu wengi kujiajiri kupitia comedy? Au ni ubora wa elimu yetu umeleta Vijana wengi wabunifu? Au kukua kwa Teknolojia nchini?

Je, kama taifa, hakuna tatizo kwa watu wake haswa Vijana kujikita kwenye comedy zaidi? Nini mtazamo wako?
Njaa, kukosekana ajira
 
Wanalipwa pesa nzuri sana huko, nadhani ndio sababu
 
Kuna kipindi cha watu baki hapa dstv asilimia kubwa ni upuuzi
 
Back
Top Bottom