Wadau, mimi nashangaa sana. Mlimani city unakuta samaki samaki pamejaa kupitiliza hadi tunasimama hapa parking area, lakini spots za pembeni wahudumu hadi wanabembeleza watu kuingia lakini kutupu!! Ni nini siri ya huyu jamaa wa samaki samaki? Ni business tactic gani anaitumia kuvutia watu hivi aisee.
Kwenye nyama choma festival, banda la samak samak watu wanakanyagana miguu hakuna hata nafasi ya kupumia! Mabanda ya pembeni peupe!!??
Ni siri tuambiane na tujifunze!
Nashukuru sana kwa swali zuri, ndio maana tunasema sio rahisi kuielezea BUSINESS MODEL kwamba huyu anafanya hivi na vile,,, la sivyo ingekuwa rahisi sana watu ku copy na ku paste na kufaulu pia ! ! !
Pia wasomi na watafiti wa biashara ndio wangekuwa vinara kwa biashara, ni sawa na kusema kwa mashule ya sekondary ST,MARY wanafanyaje kwa kuwa washindi wa kwanza miaka yote ? watu wameiga sana na hata kuwahamisha watumishi/waalimu karibia wote kila mwaka bado HAWAFANIKISHI,,,,,,,,,,,
Mara nyingi BUSINESS MODEL inafanana na founder wa biashara, pana vitu vidogovidogo sana na vingi vinapuuzwa kwa kuchanganya na vikubwa vinavyoonekana INAKAMILIKA,,,,
Na kuhama toka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine ni kama ilivyo ujasiriamali inahitajika isipungue 10 yrs na hata zaidi kwa kuwa sambamba na mhusika
Waweza kutambua baadhi tu kwa ku-google GET's General Enterprising Tendecies