Nini tafsiri ya ndoto hii ?

Few tips kuhusu ndoto (Biblical Perspective)

1. Kwanza ndoto ni bayana au halisi (kuna watu zaidi ya 10 kwenye biblia waliota ndoto na ikawa kweli, Mfano Yakobo, Yusufu, Mwokaji na Mnyweshaji wa mfalme Farao, Mfalme Suleiman, Daniel, Mfalme Nebukadreza, Yusuph mumewe Mariamu, Mke wa Pilato, Mamajusi wa mashariki.

Wote hawa waliota ndoto na zikawa kweli, hata mfalme Suleiman alipata ufalme na utajiri kupitia ndoto.

2. Ndoto ikijirudia maana yake jambo hilo ni hakika na ni lazima litokee (Mfalme Farao aliota ndoto ikajirudia mara mbili, Yusuph akamwambia kuwa kwa kuwa imejirudia maana yake ni ya muhimu sana. Pia kurudia kwa ndoto maana yake unapuuzia.

3. Ndoto ni lugha ya mawasiliano ya rohoni, Mungu au shetani anaweza kuja kwa njia ya ndoto

4. Vitu unavyoviona kwenye ndoto vyaweza kuwa sio exactly what they look like, mfano unapoona mbwa haina maana kuwa ni mbwa kweli... kawaida kuna sheria ya rohoni ya kubadilisha maumbo inayotumiwa na ufalme wa Mungu na hata shetani pia, ni kanuni. Mfano Yesu baada ya kufufuka aliwahi kuwatokea wanafunzi wake akiwa na sura nyingine (Mark 16:12). Therefore, mtu mbaya kama mchawi anapokuja kukudhuru anavaa sura nyingine ili usimtambue, hii ni kanuni ya rohoni. Mchawi huyo anaweza kuwa ndugu yako anajua utamwona na kumtambua hivyo ananuizia umbo lolote, mbwa, paka, nyoka, n.k

5. Kwa ufahamu wangu ndoto hiyo sio nzuri hata kidogo, tafadhali tafuta msaada wa haraka sana kwa mchungaji mwenye maarifa ya ndoto, nakushauri uende kwa any pastor anayesali Ufufuo na Uzima, Kawe; they are experts in that area.

Alternatively, ningekuwa mie nikishtuka tu kwenye hiyo ndoto naanza kuivunja hapo hapo kisitokee kitu chochote kibaya kinachopangwa katika ulimwengu wa roho, in the name of Jesus. Kwa taarifa yako matatizo ya watu yanaanzia rohoni na huwa wanayaona katika ndoto ila hawajui what they mean and their impacts. Ndoto ni monitoring system ya maisha ya mtu na ndio moja ya sababu Mungu kuweka usingizi.

I have a lot to say about dreams lakini hayo ni machache sana.
 
Kumuona mbwa kwenye ndoto kunahusiana na ngono na uasherati punguza hayo mambo kama unayafanya sana
 
unaonywa kwa habari ya mwanamke atakayekujia siku za usoni tu. Atakuwa rafiki sana kwako ila atakutia wazimu kimapenzi kiasi kwamba utajisahau na ndiye atakuharibia future yako. Huyu atakufanya masikini wa kutupwa ndipo akuache.
Ushauri:
Kama unaye mke, usilogwe ukaonja mchepuko. Hata akijitupa miguuni pako usimwangalie japo kwa mara moja tu. (Hit and run) ndiyo mwisho wako.
Kama huna mke, uchumba wako utakuwa wa shida kwani watakujia wawili kwa mpigo nawe utashindwa kuchagua. Atakaye kutega ndiye atakumaliza. Usimguse yeye atakaye kutega eg Nimekosa usafiri, naogopa kulala peke yangu etc usimguse mchukue huyo wa pili.
Huu ni ushauri hata kwa wengine wenye matatizo ya kuchagua mchumba.
 

mkuu, asante kwa ushauri mujarab.
 
Kuna tabia mbaya umeanza kujihusisha nayo hivi karibuni. unatakiwa uache.
 
Hujawahi kuwa mwizi au kuiba ki2 chochote?...isijekuwa wenye mali zao ndio wameamua kukuzingua kwa style hiyo...Nakushauri rudisha mali za watu ulizochukua (kama zipo) maana wameanza na mbwa next tyme itakuwa mamba
 
Mbwa anawakilisha matatizo ya kiafya. Tegemea kupata tatizo kubwa la kiafya litakalokudhoofisha.
 
Jamani usiku wa kuamkia leo nimeota kuwa pinda amefika ofisini kwangu,tukaanza kuongelea habari za katiba. Tukabishana sana kuhusu mjadala wa katiba ulivyohodhiwa na ccm. Mwisho akaniambia hawezi kuendelea kubishana na mtumishi wa umma mwenye mlengo wa upinzani. Nakumbuka nilimwambia kuwa watumishi wengi wa umma upinzani upo myoyoni na si majukwaani, akamwamuru RAS aniwajibishe Mara moja. Mara nikasikia hodiii, Mzee mmoja amefika Asubuhi sana akiwashitaki Polisi kwa kumwomba pesa bila kosa wakati yeye ni mlalamikaji. Ila jamani hii si mara ya kwanza,wakati uchaguzi wa 2005 unakaribia niliota,nikmwona mkapa akigombana na Kikwete kwenye corridor ya muhindi mmoja anaitw a Iqbar,yupo upanga jirani na salander bridge. Hoja kubwa kwao ilikuwa nani atakuwa waziri mkuu Kikwete akiwa rais.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…