Nini tafsiri ya ndoto hii ?

Nini tafsiri ya ndoto hii ?

Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikiota ndoto niking'atwa na mbwa na ndoto hii imekuwa ikijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kuwauliza wachungaji, manabii na watu mbalimbali wanipe tafsiri ya ndoto hii 'iliyoniganda' kwa miaka mingi sasa lakini sijafanikiwa kupata jawabu. Najua humu kuna manabii, wachungaji na watu wenye pako tofauti wanaoweza kunisaidia kuotolola (kutafsiri) ndoto hii. Inawezekana hili likawa aina fulani ya pepo chafu linalotaka kuniangamiza. Nikijua aina ya pepo hili itakuwa rahisi kupanga mkakati wa kulikemelea mbali kabla halijanidhulu.

Nawasilisha.
:israel:
 
unang'atwa umekaa au unakimbia anakuja kuku attack?
 
unang'atwa umekaa au unakimbia anakuja kuku attack?

najikuta tu mbwa from nowhere akianza kunishambulia na kuning'ata miguuni. mashambulizi yakikolea nagutuka kutoka usingizini. yaani hii ndoto inanitesa kwa miaka mingi sana.
 
Ni pepo mahaba.mwone pastor au mtumish yeyote akuombee lakin pia jicomit kwa MUNGU funga hata wk moja omba utiishe nafsi
 
as a matter of fact huna haja ya kutafuta au kuchunguza aina ya spirit omba mungu akuponye God heals he never treats...
 
as a matter of fact huna haja ya kutafuta au kuchunguza aina ya spirit omba mungu akuponye God heals he never treats...

U have said it wisely. But please hapo kwenye Mungu anza na herufi kubwa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
najikuta tu mbwa from nowhere akianza kunishambulia na kuning'ata miguuni. mashambulizi yakikolea nagutuka kutoka usingizini. yaani hii ndoto inanitesa kwa miaka mingi sana.

labda nyumba unayokaa.....uki lala nyumba tofauti umewahi ota?
 
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikiota ndoto niking'atwa na mbwa na ndoto hii imekuwa ikijirudia mara kwa mara. Nimejaribu kuwauliza wachungaji, manabii na watu mbalimbali wanipe tafsiri ya ndoto hii 'iliyoniganda' kwa miaka mingi sasa lakini sijafanikiwa kupata jawabu. Najua humu kuna manabii, wachungaji na watu wenye pako tofauti wanaoweza kunisaidia kuotolola (kutafsiri) ndoto hii. Inawezekana hili likawa aina fulani ya pepo chafu linalotaka kuniangamiza. Nikijua aina ya pepo hili itakuwa rahisi kupanga mkakati wa kulikemelea mbali kabla halijanidhulu.

Nawasilisha.
:israel:

ndugu yangu uko serious kweli? maana umesema ulitafuta ushauri kwa wachungaji bila mafanikio. sasa humu jf utakubaliama na lipi maana kila atasema lake. lakini kwa ushauri wangu kama kweli unaota hivyo, kwanza kabisa chunguza maisha yako yakoje na Mungu, pili mimi naamini wachungaji walikuambia uyakabidhi maisha yako kwa Yesu ili atawale maisha yako nami nasisitiza hilo hilo, mwisho ukishampata Yesu ndoto ndoto kama hizo na nyingine zinazofanana hizo kamwe hutaota tena, vinginevyo humu jf unatafuta masangoma
 
mbona mbwa ni rafiki wa binadamu iweje ndoto ijirudie iyo tu kama vip uwe unapiga beer zako 3 daily kabla hujalala upate usingizi mwanana.
 
Ni pepo mahaba.mwone pastor au mtumish yeyote akuombee lakin pia jicomit kwa MUNGU funga hata wk moja omba utiishe nafsi

Asante kwa ushauri mkuu, nitaufanyia kazi ushauri wako.
 
ndugu yangu uko serious kweli? maana umesema ulitafuta ushauri kwa wachungaji bila mafanikio. sasa humu jf utakubaliama na lipi maana kila atasema lake. lakini kwa ushauri wangu kama kweli unaota hivyo, kwanza kabisa chunguza maisha yako yakoje na Mungu, pili mimi naamini wachungaji walikuambia uyakabidhi maisha yako kwa Yesu ili atawale maisha yako nami nasisitiza hilo hilo, mwisho ukishampata Yesu ndoto ndoto kama hizo na nyingine zinazofanana hizo kamwe hutaota tena, vinginevyo humu jf unatafuta masangoma

Asante mkuu.
 
mbona mbwa ni rafiki wa binadamu iweje ndoto ijirudie iyo tu kama vip uwe unapiga beer zako 3 daily kabla hujalala upate usingizi mwanana.

mmmhh, bia ni ngumu kumeza mkuu! sijawahi hata kunusa harufu yake.
 
Ukiona hivo ujue ni roho la uzinzi inakufatilia na kukusumbua so pray against it
 
Back
Top Bottom