nini tofauti ya haya maneno!

mashakaDaima

Member
Joined
May 3, 2013
Posts
38
Reaction score
5
huwa nashindwa kabisa ni namna gani na mahali gani kuyatumia maneno haya, "ONYESHA" na "ONESHA" kwani huwa yanawachanganya sana watu. Mfano mtu anasema "Juma ametuonesha mpira na mwingine anasema Juma ametuonyesha mpira" sasa hapo nani yuko sahihi?
 
Onyesha ni Hali ya kufanya mtu aone kitu fulani mf,Juma alionyesha kitabu. kwa swala la onesha ni Hali ya kutoa matumizi,sifa,maana na mambo mengine ambayo yanaweza kuoneshwa.Mf,onesha matumizi ya gari kwa nchi ya Tanzania.unaweza ukaulizwa swali Kama hilo.nafikiri umeweza kupata chochote kile.......

Pro J
 
Onyesha ni ku Onya yaan kutoa Angaliz😵nesha linatokana na Mzizi ona kwa hiyo Onesha ni kusaidia kutazama, mfano ni sahihi kusema Ameonesha kilipo kikwazo sio ameonyesha kilipo kikwazo. Mfano.Ni maonesho ya Biashara sio maonyesho.
 
Onyesha ni ku Onya yaan kutoa Angaliz😵nesha linatokana na Mzizi ona kwa hiyo Onesha ni kusaidia kutazama, mfano ni sahihi kusema Ameonesha kilipo kikwazo sio ameonyesha kilipo kikwazo. Mfano.Ni maonesho ya Biashara sio maonyesho.

Sasa kwa nini kamusi zina neno "onyesha" likimaanisha kutazama?

Ina maana wale wataalam wote walioshiriki kuzitunga hizo kamusi wamekosea?
 
'Onyesha' yatoka kwenye mzizi 'onya' na 'Onesha' yatoka kwenye mzizi 'ona'. 'Kuonya' ni tofauti na 'kuona'.Si sahihi kusema:'Juma ametuonyesha mpira'.Sahihi ni 'Juma ametuonesha mpira'. Si sahihi kusema 'Kutakuwa na maonyesho'.Sahihi ni kusema 'Kutakuwa na maonesho'. Kuonya ni kukaripia au kutisha.Kuona ni kutazama kwa ajili ya kutambua. Kwahiyo,chochote kihusucho kutazama,kuangalia na kuchungulia,neno sahihi ni ona(kuona/kuonesha).
 

Kwa hiyo nikisema Vuta-Nkuvute "ananionea" nitakuwa namaanisha yeye anaona kwa niaba yangu au nitakuwa namaanisha hanitendei haki?

Nakushauri ufungue kamusi ua TUKI uangalie maana ya "onyesha" kabla hujaja na simulizi zisizo na mamlaka.
 
Sasa kwa nini kamusi zina neno "onyesha" likimaanisha kutazama?

Ina maana wale wataalam wote walioshiriki kuzitunga hizo kamusi wamekosea?

usihadaike na hilo jiamini, zinakosolewa Pinalcode za kisheria itakuwa hizo kamusi , Mzizi wa Neno ni Ona sio Onya, ona inazaa Onesha na Onya inazaa Onyesha!
 
Kwa hiyo nikisema Vuta-Nkuvute "ananionea" nitakuwa namaanisha yeye anaona kwa niaba yangu au nitakuwa namaanisha hanitendei haki?

Nakushauri ufungue kamusi ua TUKI uangalie maana ya "onyesha" kabla hujaja na simulizi zisizo na mamlaka.

Mkuu, lugha kama yalivyo mavumbuzi mengine, hufanyiwa review mara kadhaa kupata utengamavu. Hapo mwanzo neno ONYESHA lilitumika kweli na sishangai ukiniambia kuwa lipo kwenye kamusi ya TUKI lakini si neno sahihi.

Kama TUKI watatoa toleo jipya la kamusi, hilo neno ONYESHA halitatumika kwa maana ya zamani. Kwa kifupi neno sahihi ni ONESHA na hiyo ni kwa mujibu wa BAKITA, review ya mwaka 1998. Neno 'onyesha' lina maana isiyo rasmi ya MAONYO kutokana na shina ONYO
 
usihadaike na hilo jiamini, zinakosolewa Pinalcode za kisheria itakuwa hizo kamusi , Mzizi wa Neno ni Ona sio Onya, ona inazaa Onesha na Onya inazaa Onyesha!

Niwekee mamlaka inayoeleza hivyo.
 

TUKI toleo la 2010 (chapa ya tano) lina "onyesha".

Oxford toleo la 2012 lina "onyesha"

Na hao BAKITA katika ukurusa wa tovuti yao wanatumia "maonyesho". Kama huniamini bofya hapa.
 
TUKI toleo la 2010
(chapa ya tano) lina "onyesha".

Oxford toleo la 2012 lina "onyesha"

Na hao BAKITA katika ukurusa wa tovuti yao wanatumia "maonyesho". Kama
huniamini bofya
hapa.

acha ubishi wewe,unaukataa ukweli ulivyo?au unatumia vitabu vibaya kama nukuu ya dr.nchimbi,jinsi alivyoinukuu biblia?
 
Onyesha ni ku Onya yaan kutoa Angaliz😵nesha linatokana na Mzizi ona kwa hiyo Onesha ni kusaidia kutazama, mfano ni sahihi kusema Ameonesha kilipo kikwazo sio ameonyesha kilipo kikwazo. Mfano.Ni maonesho ya Biashara sio maonyesho.

Upo sahihi kabisa mkuu. Yapata siku kadhaa zilizopita niliandika uzi ukihusiana na jinsi baadhi ya members humu Jf wanavyopatwa na misukosuko ya kusoma na kuandika hasa hasa katika lugha ya Kiswahili. Niliweza tolea mfn mdogo tu jinsi watu wanavyokosea matumizi kati ya neno ONESHA na ONYESHA. Kunawaliojaaliwa mameno ya kebehi na matusi walisema yao. Ila kuna member moja ndio alinichanganya zaidi kwa kutetea hoja na kudai yakuwa lugha ya Kiswahili inaanzakutumika zaidi kimatamshi kabla ya Kisarufi. Nilimuacha aamini anachosadiki na alichofunzwa. Mfan mwingine wa haraka ukiangalia zaidi mpaka leo kuna watu humu ambao hawajui uandishi sahihi kati ya neno NDIO na NDIYO. Kuna wanotamka Bibilia badala ya Biblia, Sifuri badala ya Sufuri.
 
Onyesha ni ku Onya yaan kutoa Angaliz😵nesha linatokana na Mzizi ona kwa hiyo Onesha ni kusaidia kutazama, mfano ni sahihi kusema Ameonesha kilipo kikwazo sio ameonyesha kilipo kikwazo. Mfano.Ni maonesho ya Biashara sio maonyesho.

Mkuu ingawa tunatofautiana kiitikadi,ila hapa uko sahihi!
 
Je na hapa lipi neno sahihi "yupo sahihi" au "yuko sahihi".....!???
.
Hapa, "yuko" itakuwa ina maanisha sehemu au mahali,ila "yupo" inahusika na mtu mwenyewe moja kwa moja.Kwa hiyo yupo sahihi ni sahihi zaidi. Naweza kusahihishwa!
 
Mpaka sasa hakuna aliyeniwekea rejea ya kamusi ya Kiswahili yenye neno "onesha" na isiyo na neno "onyesha".

Nashangaa kwa nini!?!
 
.
Hapa, "yuko" itakuwa ina maanisha sehemu au mahali,ila "yupo" inahusika na mtu mwenyewe moja kwa moja.Kwa hiyo yupo sahihi ni sahihi zaidi. Naweza kusahihishwa!

mkuu huu ni kama ugonjwa ama mazoea ambayo tumeyaacha na mwisho wa siku yamejenga tabia. Si wewe tu ni wengi tu humu hujikuta wametumia neno "yuko" badala ya "yupo" na hii inatokana na ulemavu wa ndimi katika kunena ambao upelekea na mkono kuandika.....!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…