Nioe mke mwingine?

Pole sana Mulama, mimi nakushauri tafuta kazi kwa bidii zote kwa kuwa umeshajua mkeo ni wa namna gani hata kama ni biashara fanya kwa bidii zote, kisha Muombe Mungu ambadilishe mkeo hapo lazima kuna watu wanamdanganya tu na kwa kuwa akili yake haina akili yeye hajui kuchuja na kuangalia alikotoka. Ukipata kazi (natamani uape kazi nzuri kushinda yake) muangalie kama atajifanya kupretend anakuheshimu kisha mkumbushe aliyokufanyia
 
Pole sana ila sikushauri kuoa mke mwingine maana utamuongezea midomo ya kulisha naye atazidi kuwanyanyasa. Fight na maisha kwanza yakae level kwa faida ya mtoto wako.
 
Pole sana ila sikushauri kuoa mke mwingine maana utamuongezea midomo ya kulisha naye atazidi kuwanyanyasa. Fight na maisha kwanza yakae level kwa faida ya mtoto wako.
 
Unasubiri yakukute ya 20%? Anza upya.. si Ujinga.. we wa kiumeni.. acha kulialia..aliyekengeuka ni mwanamke na si wewe...!!:crazy:
 

Nyumba kubwa

Toa ushauri tafadhali kumsaidia Bwana Mulama - JF watu wanavyeo/fani na majina bandia
 
Pole sana ila sikushauri kuoa mke mwingine maana utamuongezea midomo ya kulisha naye atazidi kuwanyanyasa. Fight na maisha kwanza yakae level kwa faida ya mtoto wako.

Hii naita post yangu ya mwaka
 

Mulama,

Umeshaanza maadalizi ya QT? Maana naona kwa STD VII hapo kwenye RED yawezekana ulisoma ENZI ZA MWALIMU!
 
Wewe hujamjulia tu, mpe tu penzi zito huo ujinga ujinga wake atauacha muda si mrefu, kama hajapata ngoma atarudi tu.
 
Mulana pole kwa yalokukuta. Mimi naamini wengi wa wanandoa (haswa wa imani ya kikristo) huwa tunaishi kwa kushikilia vimistari viwili katika kiapo cha ndoa: kamsatari kanakosema, ...'hadi kifo kitakapotutenganisha...' na '... kilichofungwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe..." pengine kwa cases tofauti tofauti kama hii ya mulana basi ni vema kuziangalia sentesi hizi kwa macho mawili tena makubwaa! is it worth kushikilia mistari hii kwa kigezo cha kuogopa kumkosea mungu kwa kuvunja ndoa aliyoiunganisha while by doing that unamkosea Mungu million times ukijaribu ku-defend kosa moja la kutengana ktk ndoa??? mimi binafsi siamini katika hilo. kwa mtazamo wangu ikifika mahali ndoa ile haina maslahi yoyote kwako wala wa familia yako (mke na watoto) ni bora kupeana nafasi kila mtu aendelee na zake, kwa habari ya kuwa ulimsomesha n.k. n,.k bado usiwe mtumwa ya hicho ulichokifanya.... funga buti kaanze safari ya maisha mapya utaumia kwa muda lakini utasahau na kila kitu kitaenda sawa, kwa shida hizo ulizonazo huwezi kupata muda wa kufikiria kuhusu maendeleo. hivyo nakushauri kakangu ichukue hiyo kama changamoto katika maisha na ni mapito tu endelea na maisha yako na achana na hiyo kero unayoiita 'mke'
 
Mulama,

Kama ndoa yako ya miaka 11 ni halali na kama hii hoja umeileta ikiwa ni wewe mwenyewe muathirika basi nakushauri usikurupuke kuoa mwanamke mwingine...

Kuoa TENA hakujawahi kuwa ni suluhisho la matatizo ya ndoa duniani kote - Mke wa pili huwa ni MBAYA zaidi kuliko Mke wa kwanza, na watatu ni mbaya zaidi kuliko wa pili, e.t.c.

Kutokana na post yako inaonekana mkeo wa kwanza mlishaachana (kwa uzuri au kwa ubaya), equally na mkeo wako huyu "msumbufu" alikwisha achika (kwa uzuri au kwa ubaya) and that tells me that nyote ni "broken-heart" kwa kuwa mahusiano yenu ya kwanza YALISHINDWA KUSIMAMA.. Kwa mantiki hiyo basi, inawezekana sana hata hiyo miaka 11 imekuwa ni ya "kubahatisha" zaidi na ndiyo maana wewe binafsi umeshindwa kuongeza hata elimu kiasi cha kutosha na mkeo pia haujamsomesha kiasi cha kutosha..

Administrative Secretary (post form IV) siyo "investment" ki-elimu bado angaweza kuwa kwenye nafasi kubwa zaidi kama kumsomesha kwako na mahusiano yenu ya ndoa yangekuwa IMARA toka mwanzo.. Na wewe pia kama ungekuwa hauna "element" ya "Utegezemezi aka Mario" kwa miaka kumi na moja ungekuwa una japo Diploma na au umejiajiri mwenyewe e.t.c

Kwahiyo I would boldly say, Ndoa yenu haijajengwa kwenye msingi imara, na, kwa maana hiyo basi inabidi NYOTE wawili mrudi kwenye "drawing board" na muanze upya kutengeneza ndoa yenu, of which naamini kwa msaada wa Wazazi, Ndugu, na Viongozi wa Imani za kiroho mnaweza kuanza upya maisha mema ya ndoa yenye heri na baraka... Ikishindikana, basi, ni vyema, kila mmoja akachukua mkondo wake mpya wa maisha na ku-MOVE ON kwa maana kuwa you two were not meant for each other...

Jioni Njema - Nawahi Bia za Baridi pale Baracuda kabla Tanesco hawajakata umeme!
 
Mulama.... Pole sana, kama una uhakika wa hili basi oa mke mwingine... Lakini zungumza nae kwanza na kama kweli anakupenda basi atajirekebisha
Eti MwanajamiiOne, hiyo hapo nyekundu ​huwa kweli inawezekana kwa binadamu?
 
mwngine huyo....,dah mzee sometimes mwanamke kukuzidi elimu napo issue sana pole kaka,mpe talaka moja kwa kuanzia, kama ni muislam ingawa sio lengo la Mungu ndoa kupeana talaka!
 
Ndugu huyo sio mke.na ukiendekeza ngono atakuua kwa UKIMWI.na kuoa ni yaleyale coz wanawake walio wengi ni wanafiki na hawana huruma.kinachoumiza ni huyo mtoto.tafuta kazi yoyote.kuanza upya si ujinga.bora kuwa kunguru kuliko kushi kama mtumwa.komaa kaka usione aibu katika kutafuta maisha.tumia huu mda kujipanga.wewe mwanaume,mwanamke asikuzidi akili ya maisha.jifanye mjinga upate mtaji huku unapiga kikazi chochote.kazi za ulinzi kibao.komaa.mia
 
jitahidi upate shughuli,huyo mwanamama atakuheshimu,mwombe mungu sana kila lenye mwanzo linamwisho,and what goes around comes around b
 
Pole sana! Haya ndo matatizo ya kuoa kwa kukurupuka mkifikiri mnapendana eti kwa sababu kila mmoja ameachika, kaachwa na mtoto. Baada ya maisha kubadilika ndipo imekua dhahiri kwamba hamna upendo. Angalia, kama imani/misingi ya ndoa yako inaruhusu kupigana chini....jiweke pembeni.
 
Mulama,

Umeshaanza maadalizi ya QT? Maana naona kwa STD VII hapo kwenye RED yawezekana ulisoma ENZI ZA MWALIMU!

Ki ukweli ni hoja nzito mkuu, lakini imekuwa bahati kuwa umekwisha ijibu kwamba nimekwishaanza maandalizi ya QT, na ninachokazania ni lugha hiyo ambayo wameniambia kuwa it is a ladder to all higher learnings. Pia kutokana na michango yenu ilinihamasisha nikajitutumua kukaweka kakizungu kadogo ako nionekane nami nimo kwenye social class ya wasomi. Au nimekosea jamani?!
 

Ukisoma katika fafanuzi zangu zilizokuwa zina jibu michango yenu, nimeainisha ya kwamba mama wa mtoto wangu alisha fariki sikuachana naye.
Sina element ya utegemezi ni kwamba tulikutana kazini kwenye kiwanda cha biscuits yeye akiwa teller mimi mwendesha mashine, hapo utaona kwamba si miaka yote 11 nilikuwa namtegemea yeye bali alikuwa ananitegemea kwani mimi nilikuwa nalipwa zaidi yake ndio maana nikaweza kumsomesha kozi.

Mimi std vii yeye form iv, ukiangalia kwa haraka mwenye priverrege ya kozi ni yeye, ndio maana nikamtanguliza yeye asome ili akiwa anafanya kazi nami nianze kusoma kama walivyosema wachangiaji kuwa eleimu haina mwisho.

Matatizo yanaanza baada ya kiwanda kufungwa nikawa sina kazi ndio anaonyesha true color tuki approximate ni kama miaka miwili hivi ndio mtafaruku umeanzia.
Nadhani umenielewa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…