Niokoleeni watoto wangu tafadhali wanaJF

Niokoleeni watoto wangu tafadhali wanaJF

Pole sana kwa kuuguza,nenda hospital, Kuna ugonjwa unaitwa eczema Ni pumu ya ngozi huwapata Sana watoto Ni nafikiri ndo Tatizo la mwanao, huwa vinawasha Sana, tiba sijui Ila hospital utapata usichoke
 
pia angalia sabuni za kufulia nguo,na wengine wanareact na jonson products zinareact kama hivi mtoto wetu alipata shida,pia vyakula vyakununua muache vyakwenye mabox,pia mama asijipulizie mapafyum au mafuta mafuta malotion inaleta mzio kwa mtoto.pole sana,mafuta ya nazi yakupikwa nyumbani ndio atumie.jaribu hayo kwanza
 
Dr. kundi tabata ndio alitusaidia sisi mtoto alipopata shida hii
 
Kacheka kwa sababu si kila kitu kuombewa kwani mleta mada kanisa hakuliona? Mimi nilitegemea wewe ungetoa ushauri mzuri wa tiba ya mtoto na si vinginevyo,l

Kwani ni ushauri gani kaomba?kama ni hospitali pia aliziona na dawa kashajaribu,Njoo Lugalo hospital
 
Acheni kudanganya watu.
Nyie ndio husababisha watu kuathirika zaidi kwa kiwapeleka Makanisani Badala ya Hospitali.

Km Makanisa yanatibu kwanini Kadinali Pengo alilazwa Hospitali?
Hivi lini Mtaacha Kuwaongopea watu na kuuacha huo Usanii wenu?

Gwajima anadanganya watu kuwa yeye anatembea Na Yesu wakati amekamatwa anatembea na Bastola na Akatamka mwenyewe kuwa mara zote anatembea na Silaha Kwa ajili ya Kujilinda.

Uongo pia Ni fani lkn Nyie fani hio Bado sana.

Asiyejua maana haambiwi maana,UKRISTO NI TIBA PIA
 
Tena visit wale jamaa wa forever living..kwa hali aliokua nayo mtt ni nzito kiukweli..na Dawa zao zipo vzuri..yu can try them
 
Asiyejua maana haambiwi maana,UKRISTO NI TIBA PIA

Km ni tiba ilikuwaje Kadinali Pengo apelekwe Hospitali?

Au Kwanini Wakati Gwajima Anazimia pale polisi Msimpeleke kanisani mkakemea tu kwa jina la Yesu.
Ikabidi akimbizwe Muhimbili?

Wacheni Usanii nyie.
 
Pole sana mkuu. Motto akiumwa mzazi anakosaga raha kabisa.

Mtoto akilia na wewe chozi.

Mnnnh. Mungu atawasaidia. I hope Kuna blood tests zitakazofanywa.
 
Ujue kuna watu huku wanajua kila mwana jf anaishi dar,,,uliza mtu yupo wapi kwanza sio njoo hapa temeke mara njoo hapa kariakoo,,wengine tupo nanjilinji
 
Back
Top Bottom