Nipeni ushauri: Je, nimpeleke kwenye vyombo vya sheria au nimuachie Mungu?

Nipeni ushauri: Je, nimpeleke kwenye vyombo vya sheria au nimuachie Mungu?

Kiti Chema

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2017
Posts
1,793
Reaction score
1,961
Habari wana Jf. Bila kupoteza mda niende moja kwa moja kwenye lengo, mimi tangu mwaka jana niliajiriwa kwenye kampuni ya mtu binafisi,

Kipindi ninaajiriwa msimamizi mkuu walikuwa ni wahindi baada ya kama miezi 4 wale wahindi wakaondoka kwao wakafanya kumkabidhi MTANZANIA ili aimiliki hiyo kampuni baada ya hapo ndipo maisha ya kufurahiya kazi yalitoweka nikaanza kuteswa kwa kupewa kazi nyingi ambazo zilinilazimu kutoka usiku wakati nimeingia muda wa kazi asubuhi saa 2:00, na tena kutumia computer mpaka macho yanauma kutokana na kazi nyingi.

Baada ya hapo yule Boss wangu mpya akanipunguzia mshahara pia na pesa ya chakula na chai ikapunguzwa. Me nilivumilia lakini jambo lililonifanya kuandika uzi huu yaani tangu mwezi wa kwanza mwaka huu mpaka mwezi wa tano sikulipwa hata mia katika mshahara wangu maana kila nilipokuwa nikidai yeye anasema nivumilie kampuni imeshuka katika kiwango cha mapato.

Uamuzi niliouchukua niliamua kuacha kazi na kila nikimdai anasema kuwa deni halifungi hata nikienda kushitaki haita saidia lolote.

NAOMBENI USHAURI JE NIENDE KUDAI HAKI YANGU KWENYE VYOMBO VYA SHERIA AU MUNGU NDIYE ATAFANYA KISASI MWENYEWE

Na sheria ya kazi inasemaje maana ninachohofia mimi sikupewa mkataba au karatasi ya kusaini wakati naingia ktk kazi hiyo
 
mkuu lakini kuna jamaa tuliyekuwa tunafanya naye kazi na yeye aliondoka hivi nikimuita si anaweza kuwa kama shahidi wa kunitetea
Hebi tuambie kwanza mkataba wa ajira yako ulikuwa na vipengele gani muhimu kuhusu ajira yako?
 
Hebi tuambie kwanza mkataba wa ajira yako ulikuwa na vipengele gani muhimu kuhusu ajira yako?
sikupewa mkataba wowote. Kumbuka hii ni kampuni binafsi me niliitwa na kuwapa vyeti vyangu walipovithibitisha wakasema anza kazi ikawa asubuhi nikiingia nasain tu basi siku zinaendelea mwisho wa mwezi napewa changu
 
usiogope walikuwa wanakulipa nssf, walikuwa wanakulipa paye madeni ambayo hayafungi ni haya ya mitaani hawezi kukufanyisha kazi bila kukulipa nenda labour utaelezwa haki zako
 
kama upo dar ukienda kwa makonda utasaidiwa tu yule jamaa yuko fear sana japo tunamchukia bure
 
Mkuu, unapatikana mkoa gani?
Ukitoa jibu, itapendeza pia ukiweka wazi jina la kampuni yenye ulikua ukifanyanayo ili tujue jinsi ya kukusaidia.
Na usiogope kuianika hiyo kampuni kwa jina, kwasababu ulisha acha kazi na hivyo hawana la kukufanya.
 
sikupewa mkataba wowote. Kumbuka hii ni kampuni binafsi me niliitwa na kuwapa vyeti vyangu walipovithibitisha wakasema anza kazi ikawa asubuhi nikiingia nasain tu basi siku zinaendelea mwisho wa mwezi napewa changu
Dogo pole sana, hili tatizo umejitakia mweyewe. Utafanyaje kazi kama house boy? Sekta binafsi sasa ziko taabani achana nao tafuta Maisha pengine.
 
Mkuu, unapatikana mkoa gani?
Ukitoa jibu, itapendeza pia ukiweka wazi jina la kampuni yenye ulikua ukifanyanayo ili tujue jinsi ya kukusaidia.
Na usiogope kuianika hiyo kampuni kwa jina, kwasababu ulisha acha kazi na hivyo hawana la kukufanya.
hapana mkuu me nalinda usalama wangu kwanza. Nashukuru kwa mchango wako tu
 
Pole sana...

Ina maana ulikua unafanya kazi kama kibarua... mtihani kweli kweli...


Cc: mahondaw
Daaaah. Hilo ndilo lililonicost mimi bila kujua kuhusu maswala ya mikataba. Akiliyangu ilinituma kwamba ilimuladi tu uaminifu na kulipwa mshahara basi
 
usiogope walikuwa wanakulipa nssf, walikuwa wanakulipa paye madeni ambayo hayafungi ni haya ya mitaani hawezi kukufanyisha kazi bila kukulipa nenda labour utaelezwa haki zako
niende labour befor mahakama kufungua kesi
 
Back
Top Bottom