Nipo safarini usiku huu ila nina mashaka sana na mtu niliyekaa nae siti ya jirani

Nipo safarini usiku huu ila nina mashaka sana na mtu niliyekaa nae siti ya jirani

changaule

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2020
Posts
6,039
Reaction score
10,151
Wakuu nipo kwenye bus naelekea Morogoro na nimefika maili moja kwasasa, bus nililopanda ni 2 by 2 na pembeni yangu kuna msichana ananitia mashaka mno namuhisia ni mtu wa tofauti nikimaanisha sio jamii yetu (binadamu).

Mashaka yangu yanaanzia wapi?

Huyu msichana ni mrembo halafu anaonekana mjanja fulani hivi lakini cha kunishangaza konda kamuomba jina na namba yake ya simu ili amuandikie tiketi kwa njia ya online lakini akasema namba hajaishika kichwani. Ikabdi konda achukue namba yangu ili aandike tiketi kwa niaba yake kisha mimi ndio nijue namfowadia vipi tiketi yake.

La pili simu yake hachati wala hapigiwi na wala nini, kaibwaga tu kwenye kikoba. Kwa mtoto wa kike kwa mida kama hii kusafiri lazima uulizwe ulizwe na ndugu au mchumba wako au mumeo kuwa umefika wapi kwasababu ni safari ya usiku sana lakini kwa huyu ni kimya kimya.

Ukimuuliza swali lolote anajibu kwa haraka sana halafu lazima aulize swali hilo hilo kwangu kwamba na wewe je. Morogoro tutaingia usiku sana kwanzia saa nane sasa kama ni kweli sio jamii ya binadamu nitamkacha vipi? Maana kama hana nia nzuri basi hata nikichukua pikipiki itakuwa bado sio salama kwangu.
 
Anataka damu zenu. Gari itapata ajali mutakufa weengi yeye atapona.
Hongera Kwa kukaa jirani na Jini Mkuu
 
Upumbavu unatamalaki. Huyu mtoa uzi pengine ni kiongozi wa ukoo
Ingekuwa safari ya asubuhi au juoni nisingemuhisia vibaya ila hii ni safari ya usiku wa manane. Halafu kila kitu ajui yaaani hata anapoenda hapajui anachokijua ni msamvu tu basi anapoelekea baada ya msamvu hajui ni sehemu gani. Anasema babake ndiye atamuelekeza aahukue pikipiki anatakiwa aende kijiji gani.. tumefuka Ruvu hafanyi hata update kwa huyo babake kumjulisha kafika wapi.
 
Ingekuwa safari ya asubuhi au juoni nisingemuhisia vibaya ila hii ni safari ya usiku wa manane. Halafu kila kitu ajui yaaani hata anapoenda hapajui anachokijua ni msamvu tu basi anapoelekea baada ya msamvu hajui ni sehemu gani. Anasema babake ndiye atamuelekeza aahukue pikipiki anatakiwa aende kijiji gani.. tumefuka Ruvu hafanyi hata update kwa huyo babake kumjulisha kafika wapi.
Shughulika na mambo yako, ndiyo ujumbe anaokupa
 
Shughulika na mambo yako, ndiyo ujumbe anaokupa
Nakuelewa sana mkuu, kumbe ni hivyo. Lakini mkuu ni kwamba mimi sipendagi kuongea kuongea lakini kwanzia apande yeye ndiye kawa muongeaji ananiongelesha. Kaanza kuuliza hivi ni Abood eeh nikajibi sio. Hivi wewe nawe umetoa elfu kumi nikamjibu ndio. Na muda si mrefu anataka tushee kanga tujifunike wote nikakataa maana somo silielewi bado.
 
Back
Top Bottom