Nipo single, haya ni Matumizi yangu ya wiki moja - nipe ushauri

Nipo single, haya ni Matumizi yangu ya wiki moja - nipe ushauri

Safi braza.... Dawa ya mjinga ni kuumia tu.

Aliyepotea mpoteze zaid asirudi teena.

Unatoa sadaka 75 unakuja kuomba ushauri... Akamuombe askofu wa jimbo anayempa ulaji.
Kwani ameandika kwamba hiyo sadaka anapeleka kanisani???
 
Daaahh, na mimi nimechoma 156,900/= kuanzia tarehe 1/6/2019 hadi 8/6/2019.

Kucontrol matumizi huku ukiminimize inahitaji umakini sana
Oa mkuu tena uoe mwanamke mkuda ambae hana matumizi makubwa ya pesa akusaidie kucontrol matumizi ya pesa...... Naona wewe mwenyewe umeshindwa
 
Hayo matumizi mbona yapo juu sana mkuu, unataka ununue vitu vyote kama unaishi na demu babu.

Deile nunua visamaki vya buku vile au misumari (dagaa), nyanya. Monthly nunua kitunguu, mafuta na unga wa ugali tu. Hivyo ndio masela tunavyoishi!

Sasa we unataka ununue hadi hoho,binzari, letuce,gilgilani magetoni!? Utakwama tu!!!
Mmmmmh unamshauri ale bora liende
 
Ongeza sadaka, ratio ya sadaka na take home yako ni ndogo mnoo

Msisitizo usiache kutoa katika vile ulivojaaliwa hata kama ni kidogo Mungu nae mpe fungu lake ndani ya kile alichokuruzuku

Hayo mengine chukua ushauri wa baadhi ya wachangiaji mengine changanya na yako
 
mzee punguza vitu visivyo na msing kisha save money
hapo kwenye sadaka navojuaga ni utoe kile ulicho nacho. na inaonekana
wew ni muumin wa manabii wa zama hizi. sio mbaya
we cha kufanya uwe una beba pesa ya kukutoha usafiri mpaka church na kurudi na buku la sadaka pesa ingine iache home. kaza moyo ndugu .
ile chenji ya sadaka anzisha hata kamradi kadogo yani uwe unaingiza pesa sasa au vp
kamradi kanaweza kuwa ka buku teni au chini au juu kidogo ili mradi baada ya kutumia pesa nyingine ziwe zinaigia au vp jmaa
Sadaka:-
25, 000 ndo nimetoa direct
50,000 ni kwa watu wenye shida zaidi ya mimi
 
Weka utaratibu huu natumaini unalo fridge
Mchele kg 10 (16,000 - 22,000) - humalizi kwa mwezi
Samaki sato kg 2 (20,000)-utagawa kwa siku 4 (funga separate)
Nyama kg 2 (12,000) - siku 8 (1/4
Kg kwa siku)
Kuku 2 (15,000) - siku 4 (1/4 per day)
Nyanya sado 1 (4000-5000)
Vitunguu sado 1 (3000)
Bamia, hoho, karoti - (6,000)
Mafuta lita 3 - (17,000)
Tambi 2 (3000)
Unga kilo 5 - (10,000)
Maharage kilo 2 - 4000
Viazi ndoo ndogo - 7000
Na vingine vidogo vidogo - 15,000
Jaza fridge lako hapo unatoboa mwezi hayo mengineyo akili kumkichwa
. Nilipoviona nilihisi kama budget itakua kubwa vile lakn kwa haraka haraka ni kama 160,000 . hii nikiwa na familia ntaifanyia kazi. Kwa sasa itakua nafanya uharibifu
 
Mkuu kwenye hiyo hela ya ndugu unatoa kila wiki au una kituo cha kulelea yatima?

Dah! ila kiukweli tunatofautiana kwenye hiyo bajeti yako ya wiki, ongeza elfu 50 mwenzio ndio bajeti ya Mwezi na nna mke na mtoto 1.
 
Umerogwa na huyo mchungaji, yaani unampelekea 75,000/= bure.
 
Weka utaratibu huu natumaini unalo fridge

Mchele kg 10 (16,000 - 22,000) - humalizi kwa mwezi

Samaki sato kg 2 (20,000)-utagawa kwa siku 4 (funga separate)

Nyama kg 2 (12,000) - siku 8 (1/4
Kg kwa siku)

Kuku 2 (15,000) - siku 4 (1/4 per day)
Nyanya sado 1 (4000-5000)

Vitunguu sado 1 (3000)

Bamia, hoho, karoti - (6,000)

Mafuta lita 3 - (17,000)

Tambi 2 (3000)

Unga kilo 5 - (10,000)

Maharage kilo 2 - 4000

Viazi ndoo ndogo - 7000

Na vingine vidogo vidogo - 15,000

Jaza fridge lako hapo unatoboa mwezi hayo mengineyo akili kumkichwa
Jumla?.. au tuanze kujumlisha?
 
hiyo bajeti haina uhalisia kama haina maji inamaana wiki nzima hukunywa maji? vifurushi vya cm n.k, sijaona hata umehonga wala pombe haipo
 
hiyo bajeti haina uhalisia kama haina maji inamaana wiki nzima hukunywa maji? vifurushi vya cm n.k, sijaona hata umehonga wala pombe haipo
mkuu hii bajeti ni wiki moja kma nilivyo specify , cm bando hua naunga la mwez, maji na umeme vipo ndo maana.

Sinywi pombe ,sivuti sigara na nimesema kua nipo single ( sina demu)
 
Mkuu kwenye hiyo hela ya ndugu unatoa kila wiki au una kituo cha kulelea yatima?
Dah! ila kiukweli tunatofautiana kwenye hiyo bajeti yako ya wiki, ongeza elfu 50 mwenzio ndio bajeti ya Mwezi na nna mke na mtoto 1.
ndo mana nikaona nijitafakari, ahsante mkuu
 
Hiyo bajeti ni kubwa mno unaweza ukaishi kwa bajeti ndogo tu na wewe ukawa na maisha mazuri tu poromoa hiyo bajetibyote ukija hapa isizidi laki moja kwa mwezi
 
Back
Top Bottom