Nipo Tunduma, toka mafuta yapande yafikie 2,900 nauli tunalipa 1,000 ya daladala kituo kwa kituo

COMMAN

Senior Member
Joined
May 1, 2012
Posts
110
Reaction score
47
Mimi niko mji wa Tunduma toka siku mafuta yapande yafikie 2,900 nauli huku tunalipa 1000 ya daladala kituo kwa kituo.

Hakuna mamlaka zozote zinazokemea suala hili wiki ya pili, hakuna trafik wala sumatra wanaochukua hatua. Sasa inamaana hiyo ndo bei elekezi? Waziri.

Wakuu wa wilaya na wahusika wote, sasa hivi tunatafta hela kwa ajili ya nauli tu na mafuta ya kupikia, hebu waangalieee.

Mimi kinachoniuma siendi kazini tu, napata dharula zingine lazima nisafiri, unakuta nauli tu natumia 4000 hd 6000. Hebu piga hesabu unarnda kazini na mkeo, kutafta riziki kwa biashara ndogondogo. Mtoe nauli hiyo halafu mle huko mchana. Sasa mnarudi nyumbani na sh. ngapi isitoshe biashara halali ina faida kidogo
 
Yaani waziri Makamba ndio hapo unapofeli. Mimi ni shabiki wako, lakini kwa hili hapana upo kimya sana.
 
ngoja tusubiri majibu
 
Hizo ni daladala zao walioko kwenye mamlaka, kuna dalili nchi kumfia mtu mikononi,
 
Yaani waziri makamba ndo hapo unapofeli....mimi ni shabiki wako..lakini kwa hili hapana.upo kimya sana.
Hapo ndipo unapokosea, huwezi kuwa shabiki wa mwanasiasa especially Waziri, Wazir yampasa awajibike katika nafasi yake.

Hayo mambo ya ushabiki peleka kwenye music industry au sports.
 
Kwani hamna madiwani na meya wao ambao ndio wanaendesha serikali local ya hapo, piganeni
 
Kuna mawaziri mizigo...hawamsaidii Mama Samia.

Mheshimiwa Rais Anza kufumua wizara na watendaji wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…