Kilimanjaro- Usangi huko kwa wapare chief.Umeandika vizuri tu na umeeleweka safi. HIYO FAMILIA NZURI SANA, MPAKA NATAMANI NINGEKUWA MIMI NIMEPITA HAPO. KWAKUWA HUJATAJA MKOA SIO MBAYA UNGETAJA INGEKUWA POA ILI SIKU NIKIKATIZA HUKO NIKAWASALIMU.
Ndo siku nyingine uende guest au hotel
Wala hawamfukuzi tatizo mazoea,mm mwenyew alishakujaga mdogo wangu kutoka kijijini,asubuhi ilivyofika nikaenda kuchukua mkate,basi yule ndugu yangu alimishangaa Sana mkate tule wawili.Hapo wanakufukuza kijanja.. Hawataki kukuona na inawezekana unalala sebuleni au nawatoto..
Sio b
Kula kidogo haiusiani na budget Sio budget Matumbo ya watu wa mjini yameshazoea portion ndogo Nyie wa mikoani ugali kilo moja unataka ule peko yako ni tumbo la kibinadamu ni pipa
Sio uchoyo kwa mtu anayejitambua huwezi enda ishi kwa mtu labda muwe ndugu wa damuAcha uchoyo
Safi sana. Siku nikienda huko nakujulisha ili nikasalimie hapo, maana huwa nazunguka sana mikoani.Kilimanjaro- Usangi huko kwa wapare chief.
Sio uchoyo kwa mtu anayejitambua huwezi enda ishi kwa mtu labda muwe ndugu wa damu
Hao chakula ni cha shida na wana roho za kimasikiniNashukuru Wadau kwa michango yenu
Ila nipo mtwara ndani ndani , kwanza ni kijijin hakuna gest kbsa,Cha pili migahawa imefungwa maana wengi hapa wamefunga si mnajua huu mwezi wa Ramadhani,
Pale sokon Kuna watu jion wanauza uji na ftali ,
Ila apo wanapo uza Kuna duka la dawa la huyu dada nilipofikia na anauza mdogo wake , Jana nimeenda nikaona nikinywa uji dogo atakuja kuchoma nikala chungwa moja,
Daah yan
Mi naenda kwa watu kuanzia saa 9 mchana, maana nina hakika washakula, naondoka kabla ya 12Ndugu hao ndio
Kuna familia unaenda unajua kabisa ni hawana uwezo unanunua mboga na vitu vingine unawapelekea na ukifika wanapika kilichopo na ulicholeta wanatenga mezani au kwenye mkeka na hawabanii sasa unakuta watu wana uwezo lakin wachoyoo
Ni kweli ili usihangaishe watu wengine tunapenda mgeni akija ale hata kama wali maharage na chai ale ashibe tu ndio aende yaan mgeni kuja halaf asile bora asijeMi naenda kwa watu kuanzia saa 9 mchana, maana nina hakika washakula, naondoka kabla ya 12
Napigia mstari HAO NI WACHOYO.Kuna mahala nipo mimi ni mgeni, unakaangiwa nusu kuku na hapo wanataka ule na supu.Ukikaa kidogo wanakukaangia ndizi na perege kwa kweli nimekula.Pasaka wakataka kuniua wakanipikia machalari na minyama mikubwa kama ngumi ya mandonga.
Sijakaa vizuri wakaniletea chipsi na nyama za mbuzi za kuchoma.Hamadi wakaleta pilau mbuzi na vipande vya tikiti sijui na saladi.Nikala mpaka nikakasirika kwa furaha.Walivyo kiboko wakaniletea na supu.Mara paap bia hizi nkasema mi sinnywi bia wakaniletea soda tatu, ya mchana, ya asubuhi na ya jioni wakati wa kulala.Ratiba ya kuzinywa nilipanga mimi.
Yaani wakuu nilikuwa na uhakika wa kula nusu kuku kila siku.saa nyingine asubuhi kidari mchana Firigisi, jioni kipaja asubuhi namalizia kidari wakati mwingine.Nimekaa siku kumi na nne.Kuna kazi nilienda kuifanya kwao wameniambia nirudi tena kufanya ingine.NAONA KUCHELEWA.
SHIKAMOO WALE WATU WALIJUA KUNINYOOSHA KWA KWELI.ila mkuu pole hao watu ni wachoyo.jaiwezekani chakula ambacho hata panya hamalizi mle watu wanne.HAO NI WACHOYO.
Hata na mimi nashukuru nilizaliwa familiya ilokuwa na uwezo wa kilisha mtaa mzima so ishu ya vyakula nyumbani ni tangu tukiwa wadogo.kuna sisi tulio kulia maisha ya kula kila mda tukifika sehem ya bajet bajet hatukai tuna lala mbereee
nakumbuka tuu zamani tulipokuwa wadogo home
maziwa yakumwaga
matunda kamayote
nyama ya kuku usiseme
mahindi
yani unakuta namsosi wakutosha unapikwa tunakula na kusaza
Hadi leo nyumba ambayo chakula hakibaki naiona ina mapungufu
mama alituambia msimalize chakula chote lazima kibaki kidogo anaweza kuja mtu mwenye njaa Kali mkashindwa kumsaidia japo tonge moja na akawafia
tenga msosi mtu ale aache kikibaki kesho kinapaswa watu wananywea chai
duh kweli.sisi hatuna uchoyo sababu ya mama katufunza kuishi na watuHata na mimi nashukuru nilizaliwa familiya ilokuwa na uwezo wa kilisha mtaa mzima so ishu ya vyakula nyumbani ni tangu tukiwa wadogo.
Nakumbuka tukiwa wadogo baba akiwa hai, kwanza akitoka safari anachinja ng'ombe kijiji kizima wakija kumsalimia wanakula na nyama wanabeba.
Akitoka safari chakula kinapikwa kuanzia asubuhi hadi jioni yaani kila anekuja kumsalimia baba lazima ale.
Maisha ya mama baba akiwa hai ni full time jikoni na wafanyakazi wawili
Nyumbani wageni ni full time na wengine wanalala mpaka baba akisafiri tena ndo mama anapumzika.
wabibi, baba akifika kila jion wanafata mafuta ya taa na sukali hao wote lazima waondoke wamekula, chakula kikiisha lazima mama apike kingine hata kama ni usiku.
Nyumba yenye chakula cha kutosha haikosi wageni na wafanyakazi wa kutosha. Kwetu kulikuwa kama sherehe most of the times.
Siku baba yangu amefariki watu wazee kwa vijana walilia sana. Msiba ulimaliza zaidi ya mwezi na zilichinjwa ngombe zaidi ya 10 sikumbuki idadi maana tulikwa nazo kama 300 hivi.
Kama una uwezo lisha watu washibe ili ukifa tupate na machozi ya kukulilia.
Msibani kwa baba watu walikuwa wanalia hivi:,
Wazuri hawadumu, tulikula bure, nyama tulipewa bure, sukari bure mafuta bureee, wewe mtoto nini kimekupata? Wanapiga geneza wamama, amkaaaaa sisi tunakula wapi? Amkaaa watoto wetu wanalipiwa na ada na nani? fulani amkaaaaaaa. Loh nimekumbuka mbali.
Pole sana binti kwa kukumbukia nyakati hizo za maisha. Mshukuru Mungu aliruhusu hilo litokee kwa wakati wake. Kamwe usiache mafundisho hayo ng'wanikeHata na mimi nashukuru nilizaliwa familiya ilokuwa na uwezo wa kilisha mtaa mzima so ishu ya vyakula nyumbani ni tangu tukiwa wadogo.
Nakumbuka tukiwa wadogo baba akiwa hai, kwanza akitoka safari anachinja ng'ombe kijiji kizima wakija kumsalimia wanakula na nyama wanabeba.
Akitoka safari chakula kinapikwa kuanzia asubuhi hadi jioni yaani kila anekuja kumsalimia baba lazima ale.
Maisha ya mama baba akiwa hai ni full time jikoni na wafanyakazi wawili
Nyumbani wageni ni full time na wengine wanalala mpaka baba akisafiri tena ndo mama anapumzika.
wabibi, baba akifika kila jion wanafata mafuta ya taa na sukali hao wote lazima waondoke wamekula, chakula kikiisha lazima mama apike kingine hata kama ni usiku.
Nyumba yenye chakula cha kutosha haikosi wageni na wafanyakazi wa kutosha. Kwetu kulikuwa kama sherehe most of the times.
Siku baba yangu amefariki watu wazee kwa vijana walilia sana. Msiba ulimaliza zaidi ya mwezi na zilichinjwa ngombe zaidi ya 10 sikumbuki idadi maana tulikwa nazo kama 300 hivi.
Kama una uwezo lisha watu washibe ili ukifa tupate na machozi ya kukulilia.
Msibani kwa baba watu walikuwa wanalia hivi:,
Wazuri hawadumu, tulikula bure, nyama tulipewa bure, sukari bure mafuta bureee, wewe mtoto nini kimekupata? Wanapiga geneza wamama, amkaaaaa sisi tunakula wapi? Amkaaa watoto wetu wanalipiwa na ada na nani? fulani amkaaaaaaa. Loh nimekumbuka mbali.
Luckyline umekulia familia ambazo chakula kingi na ni kitu cha kawaida so huwezi kuwa mchoyo, wachoyo wengi wamekulia familia ambazo chakula ni kidogo na kikipikwa watoto ni kugombania kula huku manung'uniko ya Huyu anakomba yanasikika. Wasukuma wakipika chakula mgeni akala akashiba ndio furahayake, hata kama ni mpita njia utakula kwanza then ndo mtaanza kufahamiana, ugali unatengwa kwenye sufuria wa moto balaa nilishindwa kula nikawa napuliza tonge basi hadi vitoto vinanishangaa eti naungua, ugali haujaisha unaletwa mwingine aise wasukuma wanakula balaa.Huyu kuku usimnunuwe ushanunua kitimoto inatosha.
Shemeji yako ni mchoyo kesho unaondoka wewe leo wakipakuwa pakuwa kingi ushibe watajua wenyewe.
Hivi ndugu yako haoni hiyo hali anajifanya kujisahaulisha nyumbani mnavyo kula? Kwa nini asimwambie mke wake apike chakula cha kutosha?
Mgeni anatakiwa ale atowe ka jasho kha!