Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Na mm nimeishi na mtu ugali wa mtu mmoja Basi atapika mle Kama watatu HV
Huyu bwana namuonaga lege lege HV

Mtu unatakiwa upige heavy weight
 
Hahahahahhaaaaa nimecheka Sana wakati mwingine sio vzuri kutwambia Habari za nguruwe tafadhari lakini
 
...hivi ndivyo maisha ya binadamu yalitakiwa yawe ili kumtofautisha na mnyama pia maisha huwa ni ya Furaha zaidi na Amani unapoishi kwa kusaidia watu.!Mzee azidi kupumzika kwa Amani kwa matendo yake.
 
Ila ugenini kunaweza kukufanya usiwe na raha kuna sehemu nilifikia kabla ya kulala usiku wanaka ibada wanakusanyika sebuleni wakiamka ahsubuhi saa 12 kaibada nami sijazoea hiyo michongo
Wewe tumefanana alfu unakuta hyo familia ya Ina roho mbaya sna majirani hawaele wani nao
 
Ndio maana wasukuma wakienda mijini wanateseka sana..ugenini wewe jilie zako nje ukija homu unagusa tonge moja tu ya kuzugia.
Sipendi kulala kwa mtu sana
ERoni
Haha, mkuu familia nyingi za Dar watu hawali sana, nahisi matumbo yetu yamekuwa madogo au shida nini sijui.

Binafsi wakija wageni wanaume natoa tahadhari mapema, japo maza house anajua sana kupima share ila sipendi aibu za kijinga.
 
Iliwahi kunikuta nikawa natoka kuongezea kwa mama ntilie!!
 
Mkuu mm nimekulia mjini ni mwembamba sana ila ninakula sana, mkate mzima nafuta, chapati nakula NNE kwa kujibana sana, Kuna mgahawa Fulani nakulaga mchana chakula ni expensive ila wananifahamu nauziwa plate mbili za wali au pilau kwa bei ya plate moja ugali nakula plate mbili ndo nishibe, wanaiita msukuma, nameza dawa za minyoo kila mwezi lakini kula kupo palepale, cha ajabu sinenepi hata kidogo nazidi kukonda mpaka najiuliza chakula ninachokula kinaendaga wapi?, mwaka 2012 nilihudhuria semina flan ya mambo HIV njombe wakati wa msosi niliweka mlima wa wali na viazi ndizi Kuna wazungu wakawa wanabishana kama nitamaliza nikasema moyoni hawa hawanijui, nilifuta plate nikanyanyuka nikaongeza plate ya pili nikafuta nikala matunda na maji juu, hahahaha
 
Ni vizuri kupiga msosi nawakubali sna wazee was heavyweight kula nusu nzima ya ugali
 
Mbona mkija vijijin mnakula sanaa
Huwa vijijini wanatushangaa tunavyokula kidogo, binafsi nikienda kijijini kweli ninachokula wananshangaa, ila nikikaa zaidi ya wiki naanza kuzoea mazingira na kula kunaongezeka taratibu.
 
Hao Wana asili ya uchoyo.
 
Alichokitaka huyo shemeji yako ni utake kuondoka. Kwa kifupi alikufukuza kijanja kama ulivyotamania. Ni hesabu wanazozitumia sana wanawake mijini wakitembelea na ndugu toka mikoani, hasa ndugu wa upande wa 2. Kama huamini ondoka, siku ingine uje ghafla muda wa msosi, utupie jicho mezani uone shehena huta amini macho yako.
 
Je wewe ni msukuma umeenda mjini? Vumilia tu utarudi shamba.
 
Wazee walisema " ..... UGENI SI KITU CHEMA!!!"
 
Mkuu hivyo vitambi ni vya bia tuu hamna kitu hapo ndani....... Nashangaa siku flani tumetoka na mwenyeji wangu kupiga gambe kidogo......., Kwa sababu ni mwanaume na kitambi chake ikabidi nimshawishi tupige b&w moja ili apunguze mafuta......

Weee nashangaa mtu nusu glass tuuu anaongea kipare mixture kikurya mwisho akalala......., Yaani mwili hauna nguvu kabisa ya kuhimili pombe kidogo ila mtambi huo duuh....., ikabid nibebe mzigo wangu hivyohivyo pakiza kwenye chuma yake peleka nyumbani huko.........

Ila jamani kuleniii acheni mambo ya ajabu... mko wanne pika wali kilo moja angalau ili mtu ashibe sio maswala ya kuonjeshana......,
 
Dah mimi nimeshakataa kukaa nyumba ya mtu ugenini,unateseka msosi hushibi nilishawahi dakwa jikoni nadokoa chakula asubuhi asubuhi njaa kali😀😀😀,yaani jamaa hawali kabisa,ka ugali kadogo

Nikaona hapa nateseka nikawa naenda kula mtaani khaaa.
Kukaa kwa watu ni taabu
 

Unajaza wanga usio na faida. Ugali Sahani mbili zote za nini?! Au unalima heka tatu kwa siku
 
Wewe tumefanana alfu unakuta hyo familia ya Ina roho mbaya sna majirani hawaele wani nao
Hapana hawana shida na mtu wako vizuri hata mimi walikuwa wananitreat vizuri mno ila linapokuja suala la ibada zao hapo ndipo nilipokuwa naona miyeyusho ni wasabato jumamosi moja walinibeba kkwenda nao sabato
 
Mwambie mwenyeji wako. Funguka atakuelewa. Utapigiwa na kupakuliwa kiasi cha kutosha kwako.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…