Nipo ugenini, wanapika chakula kidogo mno

Inanikumbusha mwaka 2012 nilipata kazi Singida, nikafikia kwa mtoto wa mjombaake mama.
Alikuwa ni mshkaji wa miaka kama 35 or 38 hivi.
Dah, mwamba alikuwa anapika wali robo. Mimi nishazoea kufukia mzee,nikamwambia aka sema niwe napika mimi nkasema poa.
Nikanunua vyakula,nikawa napika kilo nzima jioni mahesabu na kesho tunywee chai ila kila nkiamka asubuhi nakuta ubwabwa umelowekwa ila yeye keshatoka.
Nikajua yeye ndo anaefanya hivyo akishakula,nkaona so kesi nkaanza kula mgahawani tuu kibishi.
Ila mwamba nilivyohama pale kisha nikaonyesha dalili za kutoboa akaanza mambo ya kuniendea kwa waganga ili anizime maana hiyo kazi aliniunganishia babaake na nilikuwa kitengo cha malipo.
Kiukweli alinisumbua sana na kazi nikaacha.
Kuna wengine sio life style ni uchoyo tuu wa asili.
Na hapo ulipo itakuwa huyo mke wa jamaa ndo anasauti hapo ndani,so anaamua atakavyo.
 
Halaf sio kwamba wao wanakula kidogo hapana huko wanapotoka makazini kwao wanakula wanashiba wakifika home wanajazilizia kidogo
Watu wa hivyo siku wakija kwenu wapikie chakula kingi na kizurii wale sana
Exactly,,nna huyo mama ndugu ukienda kwake familia kubwa atapika wali kwa ricecooker vikombe vitatu na vimboga mshenz then kinatengwa kdg sanaaaa mezan
Wakija kwangu mkoan tunawaandaliaa vzr sanaa kwa muda wote watakaokaa
Wanakula sana mpk unajiuliza why kwao hawapiki vingi
Sipend tabia ya kupika chakula kidogo ht watu wananyumban kwangu wanafahamu ilo km tunatafuta hela basi watu wa nyumba yetu wale na kushibaa wasisahau kushukuru Mungu
 
Ndio hivyo boss
 
Duh mzee wako alikua mtu wa watu

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
Alikufa at age of 30 yrs can you imegine.
Si unajua mtu akifa gafla maneno mengi lazima yatoke nani kasababisha?
Ilikuwa 1993 baba alikuwa akimsomesha sekondari bint wa bibi mmoja.
Siku mbili kabla ya kifo chake huyo bibi alikuja nyumbani akakuta baba yuko holi akaanza kulia nini kimempata mtoto wangu?
Huyo bibi alivyotoka analia akasikia umbea kuwa fulani wenda kafanya kitu.

Huyo bibi wakati huo alikuwa mmama wa makamo, mimi nilikuwa mdogo ila hiyo kumbukumbu ninayo.

Bibi huyo niliona kavua ndala kakimbia peku akielekea kwa huyo mtu walokuwa wakimsema wenda kafanya jambo baya kwa baba.

Alivyofika kwa huyo mtu nasikia alitembea na magoti akimuomba kama kafanya chochote basi asemè anataka nini. Nasikia huyo mtu akajibiwa bora akipelekwa hospital arudi jeneza na wengine tuwe na maisha mazuri.

Bibi huyo alirudi nyumbani analia akasema kama kuna mkono wa binadamu kwa mwanangu huyo mtu nishuhudie akimfata mwanangu. Nadhani huyo bibi alijuwa lazima baba afe.
Baba akapelekwa hospital j2.
Haya yote yanatokea mama alikuwa kaenda kujifungua......
Baba alikuwa amemsomesha kaka fulani hivi ana exposure ya kwenda hata sehem x, mbali kweliii alivyoona hali inakuwa mbaya ikabidi aandike barua amtume huyo kaka amwambie mama awahi. Usafiri zamani ulikuwa wa shida sana.
Huyo kaka alivyofika akakuta mama kajifungua mtoto wa kiume, akarudisha taarifa kuwa mama kajifungua atakuja alihamisi.
Juma nne huyo kaka akarudisha majibu kuwa mama kajifungua mtoto wa kiume atakuja alhamisi.

Baba akasema neno la mwisho " nimekufa bila kumuona mwanangu wa kifume" na dk hiyo akafariki.

Kweli mama anafika siku hiyo ya alhamisi analeta mtoto hajui habari za msiba wamesubiri wapi anakuta tunazika. Iliuma vibaya mno. Naikimbuka hiyo siku ila nilikuwa mdogo sikujua kuwa hatorudi.

Mtuhumiwa mauti nae yamemkuta mwaka jana baada ya miaka 29 ila yeye amedumu. Ameona wajukuu zake baba yangu hakuona kitu.

Mtuhumiwa siku alipo kufa, yule bibi aliyeenda kumuoma kama kafanya kitu arudishe moyo baba apone, bibi alivyosikia kifo cha mtuhumiwa wa kifo cha baba, alilia akasema fulani uliniulia mwanangu ukijua Mungu hakuoni? hayo ni malipo yako.

Maskini huyo bibi hata hamzai baba yangu sema tu alimsomeshea binti yake na huyo binti kwa sasa ni mwalimu mkuu.

Fatilia hata kwenu, watu wema wanaosaidia jamii hawawezi ishi muda mrefu. Akiishi sana miaka 50.
 
Mimi hata hapo home ningekua sili.Nakula kitaa nikirud jion unawaletea na zaga za hapa na pale ila msosi Nehiii..
 
Ila ugenini kunaweza kukufanya usiwe na raha kuna sehemu nilifikia kabla ya kulala usiku wanaka ibada wanakusanyika sebuleni wakiamka ahsubuhi saa 12 kaibada nami sijazoea hiyo michongo
Kwangu utapachukia sana 😢
 
Kiukweli huwa wanakuwa wachoyo huwezi bania watu unaoish nao chakula
Watu wanaopika msosi kidogo makwao wakienda kwingine wanakula sana tena vizuri tu
 
Mimi hadi leo huwa namtania mama kuwa kama asingeishi maisha ya kulisha watu sasa amezeeka angekuwa hata na nyumba 4. Yeye huwa anacheka na kusema kila mtu amekuja duniani kwa purpose fulani, Anyways.

Aisee kwetu kulikuwa na watu!!!! Sijui walikuwa wanatoka wapi wale watu, unakuta mtu na mdogo wake wote wapo kwetu... Ila chakushangaza msosi haukuwa kipengele. Mama alikuwa ninja sana, now naelewa ile menu plan yake, lengo ilikuwa watu wale washibe.
Asubuhi saa 1 uji na popcorn viko tayari.

Saa 4 vinapikwa viazi, mihogo na maandazi yakutosha na chai.

Saa nane ugali maharage,nyama na mboga majani. Au ugali, utumbo, mboga za majani na maharage, au ugali, maini, majani na maharage.

Usiku makande +wali na maharage/dengu/kunde/choroko na mboga za majani. Mchicha+chinese na ndizi mbivu au parachichi.

Juice za ukwaju na ubuyu, kipindi cha maembe ndio mnapata juice ya embe. inatengenezwa magaloni na magaloni yanajazwa kwa friza kama yote.

Vyakula vilikuwa havipishani muda sana, Watu wanajikuta bado wameshiba hawali sana.

Mchele ulikuwa unaletwa kutoka igunga magunia hata mawili, mahindi, maharage, mafuta ya alizeti na vitunguu vilikuwa vinaletwa kutoka kijijini kwetu, huko mzee mama alikuwa na mashamba kama heka 70 hivi... na kuna vijana wanakaa kwake (kijijini) wanalima, hadi wanavuna, na wenyewe wanachukua vyakula humo humo, vingine vinakuja mjini, vingine vinauzwa.

Anyways.. kwa maana ya chakula cha kujaza tumbo, kilikuwepo chakusaza kuhusu balance diet hapo ndio sina uhakika. Na sababu watu walikuwa wengi, hata watu wakupika na kuosha vyombo walikuwa wengi, unakuta wadada wa umri wa usichana wako wa5 au 6.
 
Inspired by mama, na mimi kwangu kukiwa hakuna watu napika kivivu vivu vitu fancy fancy. Kukiwa na watu, labda wageni familia imeongezeka, kuna vyakula huwa nawapopolea hivyo, wakila kwa uroho lazima kila mtu atafute kitanda kilipo alale kwanza 🤣
 
Kwanza ni aibu sana kulisha watu wasishibe. Sijui hata hao wenyewe wanajisikiaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…