Nishati Safi ya Kupikia, Mwarobaini tunao na ni Bora kuliko Gesi

Nishati Safi ya Kupikia, Mwarobaini tunao na ni Bora kuliko Gesi

NB: Ushauri wa kuachana na LPG (Mitungi ya Gesi ya Sasa Majumbani) itaacha wengi ambao ndio Biashara yao kwenye hasara ila kwa kurekebisha hilo Serikali inaweza kushauriana nao au kuwawezesha kwa mikopo wawekeze kwenye matengenezo na marekebisho ya vifaa vya Umeme; kwahio badala ya kuagiza majiko kutoka nje assembly plants zinaweza zikawa nchini jambo ambalo litakuza ajira na kuwapa wigo waliopo kwenye biashara ya LPG kunufaika na Umeme - Badala ya Mihan, Oryx, Taifa gesi tutakuwa na Mihan, Oryx, Taifa Cookers
 
12 volts induction cookers
 

Attachments

  • IMG_9828.png
    IMG_9828.png
    97.8 KB · Views: 9
  • IMG_9825.jpeg
    IMG_9825.jpeg
    27.4 KB · Views: 9
  • IMG_9824.jpeg
    IMG_9824.jpeg
    25.1 KB · Views: 9
  • IMG_9823.jpeg
    IMG_9823.jpeg
    30.8 KB · Views: 9
  • IMG_9821.png
    IMG_9821.png
    54.4 KB · Views: 9
  • IMG_9820.png
    IMG_9820.png
    98.5 KB · Views: 10
12 volts induction cookers
Naam hizo ni vema sana ila unajua hata kuna solar cookers yaani mtu unaweza kupika hata keki au kuchemsha maji au kupika chakula kwa kutumia nishati ya jua moja kwa moja ? Ingawa hizi zipo ila maisha ya mwendo kasi tunayoishi wengi wanapenda kitu rahisi rahisi...

Ingawa kuhusu solar na kama utahitaji kutunza hio nishati kwenye battery ili uweze kupikia usiku au wakati hakuna jua utaona hapo kuna cost ya battery (ambayo mpaka sasa hivi katika nishati ya jua bottleneck ni battery / utunzaji ambao bado ni gharama)

Ndio maana nilishashauri hapa kwamba kila mtanzania mwenye paa la nyumba aweze kuwauzia umeme Tanesco umeme ambao Tanesco watautunza kwenye Natural battery (Bwawa la Nyerere)
 
  • Nashukuru kwa michango yote chanya iliyotolewa.
  • Kwa 'upepo wa sera' ulivyo, lengo kuu ni kuwahakikishia 'big boys' wa gesi asilia soko la uhakika kupitia ruzuku.
  • Si rahisi sana kuwagomea 'big boys' kwa kuwa wana ubavu wa kuamua nani ashike nafasi za juu za uongozi.
  • Kanuni na sheria zote hufungwa ili kwanza 'big boys' wanufaike, kisha raia wengine.
  • Hivyo basi, nashauri mifumo ya uzalishaji wa biogas kwa mtu mmoja mmoja upewe kipaumbele pia.
  • Wazalishaji na wasambazaji binafsi wa mitambo midogo, ya kati na mikubwa ya biogas wapewe nafasi. Kwa nndan
  • Nashukuru kwa michango yote chanya iliyotolewa.
  • Kwa 'upepo wa sera' ulivyo, lengo kuu ni kuwahakikishia 'big boys' wa gesi asilia soko la uhakika kupitia ruzuku.
  • Si rahisi sana kuwagomea 'big boys' kwa kuwa wana ubavu wa kuamua nani ashike nafasi za juu za uongozi.
  • Kanuni na sheria zote hufungwa ili kwanza 'big boys' wanufaike, kisha raia wengine.
  • Hivyo basi, nashauri mifumo ya uzalishaji wa biogas kwa mtu mmoja mmoja ipewe kipaumbele pia.
Wazalishaji na wasambazaji binafsi wa mitambo midogo, ya kati na mikubwa ya biogas wapewe nafasi. Kwa mfano digester, pipe, storage tank n.k zilizo rahisi kusafirisha, kufunga, kurekebisha n.k ili watu walio tayari kujizalishia gesi wafanye hivyo.
  • Ikumbukwe malighafi nyingi za kuzalishia biogas zipo mpaka vijijini, ila vifaa ndio changamoto.
  • Nimeshuhudia vyoo vya maji vikitumika kuzalishia gesi, nikatamani kweli wanifungie home, ila jitihada zangu za kuwapata wataalamu waliofanya kazi ile zimegonga mwamba.
 
  • Nashukuru kwa michango yote chanya iliyotolewa.
  • Kwa 'upepo wa sera' ulivyo, lengo kuu ni kuwahakikishia 'big boys' wa gesi asilia soko la uhakika kupitia ruzuku.
Dunia ndivyo ilivyo watu wenye pesa zao ndio wanaowaweka watoa maamuzi na wanaoamua kwenye madaraka au waamuzi pia wana hisa kwenye mambo mengi yanayofanyika..., hivyo mimi sikatai wanufaike ila wanufaike pale ambapo na wananchi na Taifa litanufaika....

Kuhusu gesi asilia ya Mtwara ni kama nilivyosema..., hii ili iwe practically njia moja ya kufanya huwa ni kuweka mabomba kutoka inapotoka mpaka inafika / tumika (ni kama Russia ana bomba kutoka huko kwao mpaka sehemu nyingi za Europe...

Sasa kutandaza hizo pipe sio mzaha na kwanini tutandaze pipe mpaka mlimani kwa bibi na babu fulani wakati hao wote wana umeme unawafikia ? Utaona kwamba njia rahisi ni kupeleka pipe mpaka sehemu chache ili nishati hio ya gesi asilia iweze kuchemsha maji ya kuendeshea turbines na kutengeneza umeme ili umeme huo upitie kwenye nyanya na kumfikia babu na bibi mlimani ili waweze kupika kitoweo chao....
  • Si rahisi sana kuwagomea 'big boys' kwa kuwa wana ubavu wa kuamua nani ashike nafasi za juu za uongozi.
  • Kanuni na sheria zote hufungwa ili kwanza 'big boys' wanufaike, kisha raia wengine.
Mbaya zaidi hata raia hatuna information yaani tumewaachia watu ndio watuamulie na wafikiri kwa niaba yetu bila kuhoji kwahio hata tukiambiwa kibaya ndio kizuri au hiki ndio kizuri zaidi hatuwezi kubisha zaidi ya kukubali..., kwahio cha maana ni kupata taarifa sahihi ili tukifanya maamuzi yawe ni ya manufaa..., pia hata hao big boys wanaweza kuwekeza kwenye vifaa vya umeme, (kutengeneza, ku-assemble na kuagiza) itakuwa ni raia wenzetu wananufaika na sio hii LPG ambayo tunanufaisha mataifa mengine pia...., na kupanda kwake kwa bei hatuna say yoyote...
  • Hivyo basi, nashauri mifumo ya uzalishaji wa biogas kwa mtu mmoja mmoja upewe kipaumbele pia.
Wazalishaji na wasambazaji binafsi wa mitambo midogo, ya kati na mikubwa ya biogas wapewe nafasi. Kwa ndani
Kuzalisha Biogas hata sasa hivi wewe haukatazwi unaweza ukaishi off-grid na kupikia kutumia samadi ya mifugo yako, tena hapo utakuwa unaishi sustainably.., lakini kwa nchi yetu nina uhakika umeme ukishuka sana (jambo ambalo linawezekana kabisa) kwanini mtu aangaike na kushughulika na vinyesi wakati akibonyeza tu switch baada ya muda ubwabwa umeiva...
 
Dunia ndivyo ilivyo watu wenye pesa zao ndio wanaowaweka watoa maamuzi na wanaoamua kwenye madaraka au waamuzi pia wana hisa kwenye mambo mengi yanayofanyika..., hivyo mimi sikatai wanufaike ila wanufaike pale ambapo na wananchi na Taifa litanufaika....

Kuhusu gesi asilia ya Mtwara ni kama nilivyosema..., hii ili iwe practically njia moja ya kufanya huwa ni kuweka mabomba kutoka inapotoka mpaka inafika / tumika (ni kama Russia ana bomba kutoka huko kwao mpaka sehemu nyingi za Europe...

Sasa kutandaza hizo pipe sio mzaha na kwanini tutandaze pipe mpaka mlimani kwa bibi na babu fulani wakati hao wote wana umeme unawafikia ? Utaona kwamba njia rahisi ni kupeleka pipe mpaka sehemu chache ili nishati hio ya gesi asilia iweze kuchemsha maji ya kuendeshea turbines na kutengeneza umeme ili umeme huo upitie kwenye nyanya na kumfikia babu na bibi mlimani ili waweze kupika kitoweo chao....

Mbaya zaidi hata raia hatuna information yaani tumewaachia watu ndio watuamulie na wafikiri kwa niaba yetu bila kuhoji kwahio hata tukiambiwa kibaya ndio kizuri au hiki ndio kizuri zaidi hatuwezi kubisha zaidi ya kukubali..., kwahio cha maana ni kupata taarifa sahihi ili tukifanya maamuzi yawe ni ya manufaa..., pia hata hao big boys wanaweza kuwekeza kwenye vifaa vya umeme, (kutengeneza, ku-assemble na kuagiza) itakuwa ni raia wenzetu wananufaika na sio hii LPG ambayo tunanufaisha mataifa mengine pia...., na kupanda kwake kwa bei hatuna say yoyote...

Kuzalisha Biogas hata sasa hivi wewe haukatazwi unaweza ukaishi off-grid na kupikia kutumia samadi ya mifugo yako, tena hapo utakuwa unaishi sustainably.., lakini kwa nchi yetu nina uhakika umeme ukishuka sana (jambo ambalo linawezekana kabisa) kwanini mtu aangaike na kushughulika na vinyesi wakati akibonyeza tu switch baada ya muda ubwabwa umeiva...
Kwenye maelezo ni rahisi kutumia biogas, Ila kiutendaji si rahisi. Ukisikia mtu anatamani kutumia kitu flani na akashindwa, ujue kuna ugumu. Hakuna mtu mwenye akili timamu asiyeoenda mambo mazuri na rahisi.
 
Kupunguza gharama za umeme, na uhakika wa kupatikana pia itakuwa mkakati mzuri.
Pia serikali iwezeshe upatikanaji wa betri bora za sola na kwa gharama nafuu.
 
Kwenye maelezo ni rahisi kutumia biogas, Ila kiutendaji si rahisi. Ukisikia mtu anatamani kutumia kitu flani na akashindwa, ujue kuna ugumu. Hakuna mtu mwenye akili timamu asiyeoenda mambo mazuri na rahisi.
Biogas sio rahisi inahitaji uangalizi kuna kazi inatakiwa ifanyike ndio maana sijasema watu watumie Biogas ila kama wewe ni mkulima na unayo au magereza na wanazalisha kinyesi cha kutosha basi wanaweza kutumia Biogas..., ila rahisi zaidi ni umeme mtu haufanyi lolote ni kuchomeka tu plug na bei ikiwa ndogo kuliko gesi ni nani atatumia gesi ?
 
Kupunguza gharama za umeme, na uhakika wa kupatikana pia itakuwa mkakati mzuri.
Hilo lipo wazi na ndio njia kuu ya kufanikisha ninachosema...
Pia serikali iwezeshe upatikanaji wa betri bora za sola na kwa gharama nafuu.
Tatizo la mpaka leo kuhusu solar bado ni battery, na battery tunaagiza na energy density ya battery bado hairidhishi ndio maana nilishatoa wazo la mtu mwenye solar wala hasihangaike kuhifadhi umeme kwenye battery..., tanesco wafunge smart meter mtu akizalisha anawauzia Tanesco kama credit na Tanesco kama hautumiki kwa wakati huo unakwenda mpaka kwenye bwawa la nyerere unatunzwa kwa kutumia pump na kuhifadhi maji kutoka bwawa la chini mpaka la juu (hio itakuwa ni battery kubwa na ya gharama ndogo)

 
Kwa mahesabu ya haraka haraka kilo moja ya LPG ni kama 13.6 Kwh (yaani units 13.6) ule mtungi wa kwenye elfu 60 average tuseme una kilo 15 (ingawa sio 15 kuna uzito wa cylinder) kwahio mtungi huu una kama 13.6 x 15 = 204 Units

Kwahio tuseme kwa bei ya sasa ya mtungi inabidi unit moja iwe kwenye 294/= (60,000/= gawia 204)

Tukija kwenye ufanisi kama mtu atatumia induction cooker ambayo ni most efficient kulikio hata gesi.... (Kuna vyanzo vinasema zaidi ya mara tatu) utaona kwamba umeme unaweza ukawa Nishati Safi Kabisa ya kupikia na gharama ndogo kabisa...
 
Ushauri mzuri Sana huo lakini kwa bara hili la kiza hasa kusini mwa Sahara desert ni ndoto za alnacha.
 
Naunga mkono hoja! Majiko ya induction cooker yapo mpaka ya 12 Volts na yana weza kuwa powered na solar pannel. Pia Watanzania wanatakiwa wawezeshwe kwenye Bio Gas systems zinazozalisha Ges kutokana na mabaki ya Chakula, mimea na vinyesi vya wanyama.... mitungi ya LPG bado ni mzigo kwa familia nyingi na hata hawa mama Ntilie. Ipo haja hawa mama Ntilie wapewe Biogas system waweze zalisha ges ya kupikia kutokana na mabaki ya vyakula na mboga mboga wanazopika katika kazi zao
Kama watu kupata Milo mitatu ni shida wataweza kweli kupata pesa ya kununua hizo induction cooker ?

Kuna kisiwa huwa hakilipi madeni ya umeme,kwa halii unategemea serikali itakuwa na sera ya kupunguza gharama kwenye umeme ili iwe nishati kuu ya kupikia nyumbani ?
 
Kama watu kupata Milo mitatu ni shida wataweza kweli kupata pesa ya kununua hizo induction cooker ?

Kuna kisiwa huwa hakilipi madeni ya umeme,kwa halii unategemea serikali itakuwa na sera ya kupunguza gharama kwenye umeme ili iwe nishati kuu ya kupikia nyumbani ?
Tunapenda kudeka sana! Na pia kujisifia kama sisi Masikini.Umasikini wa Watanzania wengi ukiwemo na wako wewe mtoa mada ni wa kujitakia na kujiendekeza. Tanzania kwa sasa Tasaf inajitaidi kuondoa Umasikini na isitoshe sizani kama kuna familia ya Kitanzania inashindwa kula kwa siku kama unavyosema. Kuhusu Kisiwa kisicholipa Umeme! Zanzibar na Pemba Nyumba, Ofisi na Viwanda vina mita za Luku- akuna anaetumia Umeme Bure.Kampuni ya Umeme Zanzibar ZECO ina kusanya pesa na inafanya kazi kama huku. Kuna Nguzo za umeme zina anguka wanazibadilisha, transformers zinaunguwa wanazibadilisha etc. Mimi na Wewe atujui mkataba wa Tanesco na Zeco unasemaje juu ya kuuza,Kusambaza na kuhudumia njia za Umeme kisiwani Zanzibar, isije kuwa kuna Vitu Tanesco avifanyi hivyo Zeco akawa ana punguza malipo to Tanesco kufanya yeye mwenyewe- So tuache kushabikia na kusambaza habari ambazo atujui ukweli wake.Ata Muungano ukivunjika leo (God Forbid🙏) Wewe na mimi Ukapuku wetu autoisha. (ata kama Tanzania Bara itasave Trilions of money from Zanzibar -atutoingiziwa ata shillingi kwenye simu zetu)..Ni roho mbaya ulioyonayo na sumu iliyojaa moyoni mwako! Mungu akujalie macho ya kiroho kuona na kujua ukweli. Umasikini wako wa kifikra na wa moyo wako ,Ukuepuke usije kuwa kichaa physical🙏
 
Kama watu kupata Milo mitatu ni shida wataweza kweli kupata pesa ya kununua hizo induction cooker ?

Kuna kisiwa huwa hakilipi madeni ya umeme,kwa halii unategemea serikali itakuwa na sera ya kupunguza gharama kwenye umeme ili iwe nishati kuu ya kupikia nyumbani ?
Serikali ya Tanzania Yes inaweza kupunguza bei ya Umeme. Lakini kumbuka kuwa Tanesco kutokana na wizi, ufujaji wa pesa na mikataba yenye walakini na sasa Mikopo ya kuwezesha hii Miradi kufanyika na Garama ya ges na mafuta ya kurun Generators kwenye sehem ambazo azijaunganishwa na grid ya Taifa na madeni makubwa ambayo Taasisi nyingi za Serikali ya Tanzania (wewe unaona Zanzibar tu😁)- Taasisi za Serikali huku tunapoita Tanzania Bara zina daiwa pesa nyingi na Tanesco kuliko Tanzania Visiwani:Iwapo Tanesco ikiaendeshwa kimakini kwa kufuata Ukweli na uhadilifu, ikaweza lipa madeni na kurudisha mikopo iliyonayo hakika ipo siku Umeme utakuwa nafuu sana.
Ila iwapo jambo kama hili na yanayofanana na hili yataendelea , Umeme kuja kuwa wa garama ndogo tusahau👇🏽👇🏽👇🏽
 
Serikali ya Tanzania Yes inaweza kupunguza bei ya Umeme. Lakini kumbuka kuwa Tanesco kutokana na wizi, ufujaji wa pesa na mikataba yenye walakini na sasa Mikopo ya kuwezesha hii Miradi kufanyika na Garama ya ges na mafuta ya kurun Generators kwenye sehem ambazo azijaunganishwa na grid ya Taifa na madeni makubwa ambayo Taasisi nyingi za Serikali ya Tanzania (wewe unaona Zanzibar tu😁)- Taasisi za Serikali huku tunapoita Tanzania Bara zina daiwa pesa nyingi na Tanesco kuliko Tanzania Visiwani:Iwapo Tanesco ikiaendeshwa kimakini kwa kufuata Ukweli na uhadilifu, ikaweza lipa madeni na kurudisha mikopo iliyonayo hakika ipo siku Umeme utakuwa nafuu sana.
Ila iwapo jambo kama hili na yanayofanana na hili yataendelea , Umeme kuja kuwa wa garama ndogo tusahau👇🏽👇🏽👇🏽
Kuweka kumbukumbu sawa, Zanzibar imeshasema umeme iliokopeshwa na TANESCO, haiwezi kuulipa, haitalipa na imetaka isamehewe. Hakuna mkataba wowote wa kufidiana hilo.

Jambo la ajabu kuhusu madeni ya TANESCO kwa taasisi za umma hapa Tanzania ni namna yalivyotengenezwa na namna ambavyo Tanesco wanasema wanadai wakati wanao uwezo wa kulipwa kwa 100% bila kutumia nguvu, maneno wala blah blah. Jibu liko kwenye Prepaid. Nunua umeme ili uutumie na sio tumia umeme ili uje kuulipia. Zoezi simple kabisa, ni Tanesco kuset meter kwenye hizo taasisi ili wanunue umeme kabla, na kwa kila pesa wanayotoa kununua umeme basi na deni linakatwa juu kwa juu kidogo kidogo. Kama Unit itauzwa 280 basi wao watauziwa shilingi 300, ili hiyo ziada ya shilingi 20 ilipie deni mpaka siku deni limekwisha.
 
Kuliko pesa za Tasaf kutumiwa kuwagawia bure kaya maskini zilipaswa kutumika kuwaunganishia umeme (gharama za kuunganishiwa umeme wa Tanesco vijijini ni shilingi elfu 27 tu) na kusaidia kununua majiko ya umeme ya induction (bei ya rejareja ni wastani wa shilingi 135,000 kwa single plate). Hapo watakuwa wameokoa mambo mengi.
 
Kama watu kupata Milo mitatu ni shida wataweza kweli kupata pesa ya kununua hizo induction cooker ?
Kama wameanzisha mfuko wa Nishati safi ya kupikia na wanapanga kutoa Ruzuku ili watu wanunue vifaa vya gesi (sasa hapo sijui kama wataendelea kuwapa ruzuku ya kununua gesi) na hata wakiwapa ruzuku hizo pesa zinakwenda nje ya nchi kwenye kuagiza hio Gesi...,

Kwahio kama wanapanga kutoa ruzuku ili kufanya hayo hapo juu..., kwanini wasitoe ruzuku ya watu kununu induction cooker, better still kwanini hawa ambao sasa wamewekeza kwenye LPG (Gesi za sasa za kupikia za majumbani) wasihamie kwenye ku-assembly hizi induction cooker na repairs; na pia kutengeneza sufuria zake (sababu sio kila sufuria inafanya kazi kwenye induction cooker lazima iwe electromagnet...
Kuna kisiwa huwa hakilipi madeni ya umeme,kwa halii unategemea serikali itakuwa na sera ya kupunguza gharama kwenye umeme ili iwe nishati kuu ya kupikia nyumbani ?
Umeme unajua ukishazalisha ni kama maji umefungulia bomba utumie usitumie unapotea..., sasa kuliko kuendelea kutumia gesi ambayo sio gharama nafuu kwa Tanzania kwanini tusiwabane hao walipe wakitumia (after all kuna luku) Pili umeme ukiwa hata Tshs 50 au 25/= kwa unit nani unadhani hataacha kupikia ? hapo juu post number 30 nimeweka mchanganuo usio rasmi ambao gesi ukinunua mtungi wa kilo 15 ni kama units 290 sasa hapo kama kila unit ni tshs 50 mtungi huu utakuwa umenunua kwa chini ya elfu 15...

Lakini bado kuna utamu zaidi sababu induction cooker ina ufanisi zaidi ya mara tatu ya gesi hapo utatumia mara tatu zaidi kuliko ungetumia gesi hivyo cost ambayo mtu anatumia kwa kununua huo mtungi itakuwa ni chini ya elfu 5 (5,000/=)

Hizo ni hesabu siziso rasmi kama umeme utakuwa Tshs. 50/= kwa units ukiwa chini ya hapo bei itakuwa ndogo zaidi
 
Kuliko pesa za Tasaf kutumiwa kuwagawia bure kaya maskini zilipaswa kutumika kuwaunganishia umeme (gharama za kuunganishiwa umeme wa Tanesco vijijini ni shilingi elfu 27 tu) na kusaidia kununua majiko ya umeme ya induction (bei ya rejareja ni wastani wa shilingi 135,000 kwa single plate). Hapo watakuwa wameokoa mambo mengi.
Kwanza hili la kuunganisha watu ingebidi hata iwe bure ukizingatia Nguzo, Nyaya na Mita sio mali yako bali ni mali ya Tanesco....

Kuhusu watu kutumia umeme hata kama sio induction cooker kama unit ikiwa Tshs 100 tu hapo nimepiga hesabu zisizo rasmi itakuwa nusu ya bei ya mtu anayenunua mtungi..., kwahio hata kuchemsha maji ya chai ukitumia jug kettle, kupika wali ukatumia rice cooker na pressure cooker katika mengine tayari unakuwa katika bei nafuu kama ungetumia gesi
 
Serikali ya Tanzania Yes inaweza kupunguza bei ya Umeme. Lakini kumbuka kuwa Tanesco kutokana na wizi, ufujaji wa pesa na mikataba yenye walakini na sasa Mikopo ya kuwezesha hii Miradi kufanyika na Garama ya ges na mafuta ya kurun Generators kwenye sehem ambazo azijaunganishwa na grid ya Taifa na madeni makubwa ambayo Taasisi nyingi za Serikali ya Tanzania (wewe unaona Zanzibar tu😁)- Taasisi za Serikali huku tunapoita Tanzania Bara zina daiwa pesa nyingi na Tanesco kuliko Tanzania Visiwani:Iwapo Tanesco ikiaendeshwa kimakini kwa kufuata Ukweli na uhadilifu, ikaweza lipa madeni na kurudisha mikopo iliyonayo hakika ipo siku Umeme utakuwa nafuu sana.
Ila iwapo jambo kama hili na yanayofanana na hili yataendelea , Umeme kuja kuwa wa garama ndogo tusahau👇🏽👇🏽👇🏽
Ni kwamba tunachezewa sana..., Kama tulikuwa tunanunua umeme kutoka kwa Private sectors kina Dowans..., Iwapo tulikuwa tunatumia mafuta / diesel generators na sasa tunaweza tukatumia Hydro Electric Power Generation ambapo itapunguza operation costs..., kwanini bei isishuke ?
 
Ni kwamba tunachezewa sana..., Kama tulikuwa tunanunua umeme kutoka kwa Private sectors kina Dowans..., Iwapo tulikuwa tunatumia mafuta / diesel generators na sasa tunaweza tukatumia Hydro Electric Power Generation ambapo itapunguza operation costs..., kwanini bei isishuke ?
Bei itashuka pale Tanesco atakapomaliza lipa Madeni yake yote.
 
Back
Top Bottom