Nishati Safi ya Kupikia, Mwarobaini tunao na ni Bora kuliko Gesi

Kwanza nakupongeza mleta hoja. Ni mada nzuri na umeieleza kwa wepesi hata mwananchi wa kawaida anaielewa.

Pili, nakuunga mkono kuwa kati ya nishati zote zinazotajwa katika mazingira ya kitanzania ni umeme ndio nishati safi na nafuu na inayopatikana maeneo mengi ya nchi yetu.

Binafsi, hizo nishati ulizozielezea zote nimeishazitumia na nimeamua kubaki na nishati moja ya umeme wa Tanesco
ambayo kwangu (nina familia ya watu 7) naona ni nafuu sana nikilinganisha na nishati nyingine maana kwa mwezi natumia wastani wa Tshs 25,000/ kununua umeme na unanitosheleza kwa matumizi yote ya umeme ikiwemo mwanga, jokofu, kunyoosha nguo, TV, radio, kusaga matunda na kupikia. Jiko la umeme ninalotumia ni la teknolojia ya Kijerumani linatumia umeme kidogo ukilinganisha na majiko ya umeme ya kizamani au ya kichina.

Mtungi wa gas upo kwa ajili ya dharura umeme unapokatika. Kwa hiyo nami nashauri serikali yetu ielekeze nguvu kuhakikisha inasambaza miundo mbinu ya umeme maeneo yote ya nchi yetu hasa vijijini na iweke ruzuku kwenye majiko haya ili mwananchi wa kawaida aweze kumudu gharama yake kwani mimi nilinunua jiko hilo mwaka 2022 kwa bei ya Tshs 290,000/ badala ya kupigia chapuo biashara ya gas (LPG) ambayo ni miradi inayonufaisha nchi za kigeni inakozalishwa gas kuliko nchi yetu.
 
Tatizo kubwa la serikali ya ccm wanachoangalia kwenye kila mradi wao watapata nini sio nchi wala wananchi watapata nini
Tayari kwenye hili wafanyabiashara wa gesi ambao wengine ni makada wa ccm wameshachora mchoro wa kupiga pesa ndefu wakishirikiana na wanasiasa waliopo madarakani.
 
Siku wakigoma ghafla kutusuply gas tunakula vibichi.
Hawawezi kugoma sababu tunawapa dollar (kwahio pesa za kununua vitu vingine tunatumia kununua kitu ambacho tunacho) na kila siku tunalalamika dollar ikipanda maisha yanapanda kumbe ni sisi wenyewe tunapenda utegemezi (au kwa uhalisia wachache wanatuumiza wengi ili wao wafaidike)
 
Akili kubwa hii.

Mkuu naomba dondoo kidogo kuhusu gas asilia kwenye vinyesi.

Kuna utaalamu gani masinki ya vyoo kuweza kutoa nishati ya kupikia?
 
Akili kubwa hii.

Mkuu naomba dondoo kidogo kuhusu gas asilia kwenye vinyesi.

Kuna utaalamu gani masinki ya vyoo kuweza kutoa nishati ya kupikia?
Ni kwamba Kinyesi kinavyooza kinatoa ile gesi methane sasa ujazo wa Methane hio hadi uwe wa kutosha kukufanya wewe uweze kupika labda utumie mifugo au sehemu ambapo wanashusha mzigo mwingi
Ukiona hapo juu Ng'ombe mmoja anaweza kushusha mzigo mwingi zaidi na anatoa Gesi nyingi zaidi kuliko Binadamu yaani Ng'ombe mmoja ni kama binadamu 16... lakini kama una magereza unaweza kutumia mzigo wa wafungwa na hii ishafanyika hata Malawi...

 
Mkuu ahsante kwa kunitoa tongo tongo.

Swali nililouliza, pamojana takwimu uloambatisha, limekuja kujibiwa vizuri zaidi na maelezo ya mfungwa wa gereza la Malawi.

Kumbe kuna vifaa maalumu vya kukorogea hiyo 'poo' vinaitwa digester pia na kiwango mahsusi cha kutosha kinachotakiwa kukorogwa ili kuzalisha gas ya kukidhi.

Katika simulizi hiyo wanaeleza kiwango cha nishati hiyo muda flani kilipungua baada ya idadi kubwa ya wafungwa kuachiwa kutokana na gonjwa la covi!

Maana yake ni kuwa walipoachiwa 'mali ghafi' ya kuzalishia ilipungua.

Ahsante mkuu, nimeelewa bila shaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…