SoC04 Nishati ya ‘hydrogeni’ mbadala wa utunzaji wa umeme itasaidia kupunguza changamoto kutokana na upungufu wa umeme na hitilafu kwenye gridi ya taifa

SoC04 Nishati ya ‘hydrogeni’ mbadala wa utunzaji wa umeme itasaidia kupunguza changamoto kutokana na upungufu wa umeme na hitilafu kwenye gridi ya taifa

Tanzania Tuitakayo competition threads

voiceupp

Member
Joined
Aug 17, 2022
Posts
16
Reaction score
27
Uzalishaji wa umeme unapokidhi mahitaji nchini unachangia kwenye ukuaji wa uchumi kutokana na shughuli nyingi za viwanda vikubwa na vidogo kuendeshwa kwa utegemezi wa umeme Umeme unapokua wa uhakika uzalishaji wa bidhaa huongezeka na gharama za uendeshaji hupungua.

Wananchi waliojiajiri kupitia shughuli zinazotegemea umeme huepuka hasara ya kuharibikiwa na bidhaa, na kwa kushindwa kuendesha shughuli zao kwa ufanisi. Jambo ambalo huwakatisha tamaa na kuwarudisha nyuma kiuchumi.

Changamoto kubwa kwenye uzalishaji wa umeme ni kwamba umeme unahitajika kuwepo kwa kiwango sahihi kwenye gridi. Kiwango kilichopo kwenye gridi kisizidi au kupungua kiwango cha matumizi.

Hivi sasa Tanzania baada ya kuwasha baadhi ya mashine za kuzalisha umeme kwenye bwawa la Nyerere tumeshuhudia umeme ukizalishwa kupita kiasi hali inayopelekea kuzima baadhi ya mashine kuepuka changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa.

Bwawa la nyerere linaweza kuzalisha megawati 2115, kwa mwaka 2023 uhitaji wa umeme nchini ilikua ni megawati 1363.94. Ingawa uhitaji wa umeme huongezeka kadiri siku zinavyokwenda kutokana na matumizi kuongezeka.

Uzalishaji wa umeme wa maji huathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Uzalishaji kupungua yanapotimu majira ya kiangazi na kipindi cha ukame kutokana na mabwawa kupungua kina hivyo nguvu ya maji inayozungusha mashine za kuzalisha umeme kupungua.

Changamoto kubwa nyingine ni hitilafu za mara kwa mara zitokeazo kwenye gridi ya taifa jambo ambalo hupelekea ukosefu wa umeme kwa saa kadhaa kwenye maeneo mengi nchini.

Nishati ya hydrogeni suluhisho la upungufu/kuzidi umeme na hitilafu kwenye gridi ya taifa;
Ingawa changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa inaweza kutatuliwa kwa kuuza umeme nchi jirani, lakini swali la kujiuliza ni Je, umeme huo utakua wa uhakika kwa kipindi chote? Hii ni ili kuepuka kushindwa kusambaza umeme wa uhakika pindi itakapotokea upungufu wa uzalishaji au hitilafu kwenye gridi ya taifa au kuongeka kwa matumizi ya umeme nchini.

Kuepuka changamoto hii ni vizuri kuchagua njia nzuri na sahihi ya kukabiliana na changamoto za umeme nchini. Njia ambayo itaweza kutumika kwenye matumizi mengine endapo hakutotokea upungufu wa umeme.

Njia nzuri ni kuhifadhi umeme unaozalishwa na kuweza kuutumia pindi uzalishaji utakapokua mdogo. Itafanyika endapo uzalishaji wa umeme utazidi kiwango cha matumizi na kupelekea umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa. Njia nzuri na nafuu ni kuhifadhi umeme kupitia nishati ya hydrojeni. Ili kuzuia umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa, umeme utakaozidi utatumika kuzalisha gesi ya hydrojeni na kuhifadhiwa. Umeme utakapopungua kwenye gridi gesi hiyo itatumika kuzalisha umeme na kurudishwa kwenye gridi kwa ajili ya kuepusha kukatika/mgao wa umeme.

Uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme unavyofanyika;
Zipo njia kuu mbili za kuzalisha nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme ambazo ni rafiki wa mazingira.
  • Kuvunjavunja maji (hydrolysis of water) na kupata hewa ya oksijeni na hydrojeni (H2O = H2 + O2)
Njia hii hutumia umeme kuvunja maji ya kawaida na kupata gesi ya hydrojeni na gesi ya oksijeni ambapo zote zinaweza kuvunwa na kuhifadhiwa.
Ili kupata kilo moja (1kg) ya hydrojeni kupitia njia hii inahitajika kilowati 50 hadi 55 za umeme (50-55kWh).
  • Kuvunjavunja amonia (NH3) (ammonia electrolysis) inayopatikana kwenye majitaka, mabaki na vinyesi vya viumbe hai na kupata hewa ya naitojeni (N2) na Hydrojeni (H2).
Njia hii inahitaji kilowati 1.55 (1.55kWh) ili kupata kilo moja ya gesi ya hydrojeni (1kg). Njia hii inatumia umeme mdogo zaidi ukilinganisha na ya kutumia maji ya kawaida.

1715351373929.png

Uzalishaji wa nishati ya hydrogeni kwa kutumia ammonia (Picha kutoka mtandaoni)

Kiasi cha umeme kinachotokana na nishati ya hydrojeni
Kwa makadirio kilo moja (1kg) ya hydrojeni inauwezo wa kuchakatwa na kuzalisha umeme kilowati 23 (23kWh). Ili kupata megawati 100 (100mWh) itahitajika walau tani 4.3 za nishati ya hydrojeni.

Faida za kutumia nishati ya hydrojeni kuhifadhi umeme;
Urahisi na unafuu kuzalisha
Ni rahisi kuzalisha nishati ya hydrojeni kutokana na mahitaji yake (maji, majitaka, mabaki ya viumbe hai na vinyesi vya wanyama) kupatikana kwa urahisi. Pia ni nafuu kutokana umeme utakaotumika kuzalisha nishati ya hydrojeni utakua ni ule uliozidi kutoka kwenye vyanzo vingine vya umeme (maji, jua, upepo na jotoardhi ‘geothermal’)
Rafiki wa mazingira.
Mabaki yanayotakana na uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati ya hydrojeni ni maji na joto, vyote hivi huweza kutumika kwa matumizi mengine. Njia hii haizalishi uchafu au hewa chafu kwenye mazingira.
Matumizi mbadala
Nishati ya hydrojeni ina matumizi mengine kama kuendeshea vyombo vya usafiri (magari n.k) na mitambo ya viwandani. Hii ni faida kwani endapo uzalishaji wa umeme usiposhuka chini ya kiwango nishati hii itaweza kuuzwa na kutumika kwenye matumizi mengine.
Usafishaji wa maji na hewa
Uzalishaji wa nishati ya hydojeni kwa kuchakata amonia inayopatikana kwenye majitaka itasaidia kusafisha maji na kuzalisha maji safi yatakayofaa kwa matumizi ya binadamu. Pia kituo cha uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kinaweza kutumika kusafisha hewa kwa kuchuja na kuondoa vumbi linalopatikana kwenye hewa.

Ili jambo hili kufanya kazi kwa ufanisi ni vyema kufanya mambo haya;
  • Kuhakikisha kila kanda inakua na kituo walau kimoja kwa ajili ya mchakato huu,
Itasaidia uzalishaji na uhifadhi mkubwa wa nishati ya hydrojeni. Pia itasaidia kua kama mbadala (backup) pindi itakapotokea hitilafu kubwa kwenye gridi ya taifa jambo ambalo litaepusha nchi nzima kukosa umeme.
Tanzania bara na visiwani kuna jumla ya kanda 10, kila kanda ikiwekewa kituo kimoja chenye uwezo wastani wa kuzalisha umeme megawati 150 kutokana na nishati ya hydrojeni itakayokua imehifadhiwa kwenye vituo hivyo, jumla itawezekana kuzalisha megawati 1500 ambazo zitamaliza kabisa changamoto ya upungufu wa umeme nchini.
  • Kufanya marekebisho kwenye gridi za umeme,
Hii ni kwa ajili ya kuhakikisha kila gridi ya umeme inabeba kiwango cha umeme inachostahili na kuepusha kubeba kiwango kikubwa cha umeme kuzidi uwezo wake jambo ambalo hupelekea kutokea kwa hitilafu za mara kwa mara kwenye gridi za umeme.

Hivyo; uhakika na utoshelezi wa umeme utafanikiwa endapo umeme unaozalishwa utatumika ipasavyo kwa kuhakikisha uwepo wake hata endapo uzalishaji utakaposhuka. Ili kufanikisha hili itahitajika kuhifadhiwa kwa umeme unaozalishwa hasa kwa kutumia njia nafuu na yenye ufanisi mkubwa. Uhakika na utoshelezi wa umeme ni chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmojammoja.
 
Upvote 740
Kongole mkuu.. kula vote yangu. Ila nna maswali mawili:

1. Kutoa Hydrogen kutoka kwenye maji [hydrolysis] hauoni kama kutaleta vita kwenye water resources? Yaani makampuni yaanzs kuchimba visima kwaajili ya maligafi maji so competition itakua kubwa?

2. Kwenye iyo njia ya pili, End product ya Ammonia umesema ni Nitrogen gesi, vipi haitakua na madhara kwa binadamu na mazingira?
 
Chapisho makini , vipi kuhusu kulinda vyanzo vya maji, je mchakato huu ni salama kwa mazingira na vyanzo vya maji?
Ni salama kabisa, Ukipitia vizuri andiko hili utaona hydrojeni inaweza kuzalishwa kutoka kwenye maji taka, kwaiyo inasaidia pia kwenye kusafisha maji. Ina maana maji taka yanasafishwa wakati wa kuzalisha hydrojeni yanakua safi kwaajili ya matumizi ya binadamu.

Pia hata yakitumika maji safi, athari haitokua kubwa kutokana na kwamba wakati wa kuzalisha umeme, maji pia yanazalishwa kwaiyo ni kama maji yanarudishwa kwenye mazingira.
 
Kongole mkuu.. kula vote yangu. Ila nna maswali mawili:

1. Kutoa Hydrogen kutoka kwenye maji [hydrolysis] hauoni kama kutaleta vita kwenye water resources? Yaani makampuni yaanzs kuchimba visima kwaajili ya maligafi maji so competition itakua kubwa?

2. Kwenye iyo njia ya pili, End product ya Ammonia umesema ni Nitrogen gesi, vipi haitakua na madhara kwa binadamu na mazingira?
Asante sana mkuu,
Naomba nikujibu kama ifuatavyo;
1. Umeme unazalishwa kwa wingi kipindi mvua zikiwa nyingi, kwaiyo mito, mabwawa na vyanzo vingine vya maji vinakua vimefurika na ndio wakati muafaka wa kutumia umeme unaozidi kuzalisha hydrojeni. Kwaiyo hakutokua na athari yoyote ya kupunguza maji .
Ina maana ikifika wakati wa kiangazi au ukame ile hydrojeni iliyoifadhiwa itaanza kutumika kuzalisha umeme kama kutatokea upungufu wa umeme. Na wakati wa kuzalisha umeme kwa kutumia hydrogeni maji pia yanazalishwa na yanaweza kutumika kwa matumizi ya binadamu.

2. Gesi ya nitrojeni haina madhara kwenye mazingira bali ina faida pia. Nitrojeni inaweza kutumika kwenye viwanda vya mbolea kwaajili ya kutengenezea mbolea za mazao.
Lakini pia kama utakua unafahamu mimea ya miharage kwenye mizizi yake kuna bacteria ambao wanatumia hewa ya nitrojeni wanaibadilisha kwenda kwenye nitrate ambayo inaongera rutuba kwenye udongo. Kwaiyo haitaleta madhara kwenye mazingira.
 
Asante sana mkuu,
Naomba nikujibu kama ifuatavyo;
1. Umeme unazalishwa kwa wingi kipindi mvua zikiwa nyingi, kwaiyo mito, mabwawa na vyanzo vingine vya maji vinakua vimefurika na ndio wakati muafaka wa kutumia umeme unaozidi kuzalisha hydrojeni. Kwaiyo hakutokua na athari yoyote ya kupunguza maji .
Ina maana ikifika wakati wa kiangazi au ukame ile hydrojeni iliyoifadhiwa itaanza kutumika kuzalisha umeme kama kutatokea upungufu wa umeme. Na wakati wa kuzalisha umeme kwa kutumia hydrogeni maji pia yanazalishwa na yanaweza kutumika kwa matumizi ya binadamu, hapa inakua tumeua ndege wawili kwa jiwe moja.

2. Gesi ya nitrojeni haina madhara kwenye mazingira bali ina faida pia. Nitrojeni inaweza kutumika kwenye viwanda vya mbolea kwaajili ya kutengenezea mbolea za mazao.
Lakini pia kama utakua unafahamu mimea ya miharage kwenye mizizi yake kuna bacteria ambao wanatumia hewa ya nitrojeni wanaibadilisha kwenda kwenye nitrate ambayo inaongeza rutuba kwenye udongo. Kwaiyo haitaleta madhara kwenye mazingira.
 
Asante sana mkuu,
Naomba nikujibu kama ifuatavyo;
1. Umeme unazalishwa kwa wingi kipindi mvua zikiwa nyingi, kwaiyo mito, mabwawa na vyanzo vingine vya maji vinakua vimefurika na ndio wakati muafaka wa kutumia umeme unaozidi kuzalisha hydrojeni. Kwaiyo hakutokua na athari yoyote ya kupunguza maji .
Ina maana ikifika wakati wa kiangazi au ukame ile hydrojeni iliyoifadhiwa itaanza kutumika kuzalisha umeme kama kutatokea upungufu wa umeme. Na wakati wa kuzalisha umeme kwa kutumia hydrogeni maji pia yanazalishwa na yanaweza kutumika kwa matumizi ya binadamu.

2. Gesi ya nitrojeni haina madhara kwenye mazingira bali ina faida pia. Nitrojeni inaweza kutumika kwenye viwanda vya mbolea kwaajili ya kutengenezea mbolea za mazao.
Lakini pia kama utakua unafahamu mimea ya miharage kwenye mizizi yake kuna bacteria ambao wanatumia hewa ya nitrojeni wanaibadilisha kwenda kwenye nitrate ambayo inaongera rutuba kwenye udongo. Kwaiyo haitaleta madhara kwenye mazingira.
Pamoja mkuu. Impressed
 
Uzalishaji wa umeme unapokidhi mahitaji nchini unachangia kwenye ukuaji wa uchumi kutokana na shughuli nyingi za viwanda vikubwa na vidogo kuendeshwa kwa utegemezi wa umeme Umeme unapokua wa uhakika uzalishaji wa bidhaa huongezeka na gharama za uendeshaji hupungua.

Wananchi waliojiajiri kupitia shughuli zinazotegemea umeme huepuka hasara ya kuharibikiwa na bidhaa, na kwa kushindwa kuendesha shughuli zao kwa ufanisi. Jambo ambalo huwakatisha tamaa na kuwarudisha nyuma kiuchumi.

Changamoto kubwa kwenye uzalishaji wa umeme ni kwamba umeme unahitajika kuwepo kwa kiwango sahihi kwenye gridi. Kiwango kilichopo kwenye gridi kisizidi au kupungua kiwango cha matumizi.

Hivi sasa Tanzania baada ya kuwasha baadhi ya mashine za kuzalisha umeme kwenye bwawa la Nyerere tumeshuhudia umeme ukizalishwa kupita kiasi hali inayopelekea kuzima baadhi ya mashine kuepuka changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa.

Bwawa la nyerere linaweza kuzalisha megawati 2115, kwa mwaka 2023 uhitaji wa umeme nchini ilikua ni megawati 1363.94. Ingawa uhitaji wa umeme huongezeka kadiri siku zinavyokwenda kutokana na matumizi kuongezeka.

Uzalishaji wa umeme wa maji huathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Uzalishaji kupungua yanapotimu majira ya kiangazi na kipindi cha ukame kutokana na mabwawa kupungua kina hivyo nguvu ya maji inayozungusha mashine za kuzalisha umeme kupungua.

Changamoto kubwa nyingine ni hitilafu za mara kwa mara zitokeazo kwenye gridi ya taifa jambo ambalo hupelekea ukosefu wa umeme kwa saa kadhaa kwenye maeneo mengi nchini.

Nishati ya hydrogeni suluhisho la upungufu/kuzidi umeme na hitilafu kwenye gridi ya taifa;
Ingawa changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa inaweza kutatuliwa kwa kuuza umeme nchi jirani, lakini swali la kujiuliza ni Je, umeme huo utakua wa uhakika kwa kipindi chote? Hii ni ili kuepuka kushindwa kusambaza umeme wa uhakika pindi itakapotokea upungufu wa uzalishaji au hitilafu kwenye gridi ya taifa au kuongeka kwa matumizi ya umeme nchini.

Kuepuka changamoto hii ni vizuri kuchagua njia nzuri na sahihi ya kukabiliana na changamoto za umeme nchini. Njia ambayo itaweza kutumika kwenye matumizi mengine endapo hakutotokea upungufu wa umeme.

Njia nzuri ni kuhifadhi umeme unaozalishwa na kuweza kuutumia pindi uzalishaji utakapokua mdogo. Itafanyika endapo uzalishaji wa umeme utazidi kiwango cha matumizi na kupelekea umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa. Njia nzuri na nafuu ni kuhifadhi umeme kupitia nishati ya hydrojeni. Ili kuzuia umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa, umeme utakaozidi utatumika kuzalisha gesi ya hydrojeni na kuhifadhiwa. Umeme utakapopungua kwenye gridi gesi hiyo itatumika kuzalisha umeme na kurudishwa kwenye gridi kwa ajili ya kuepusha kukatika/mgao wa umeme.

Uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme unavyofanyika;
Zipo njia kuu mbili za kuzalisha nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme ambazo ni rafiki wa mazingira.
  • Kuvunjavunja maji (hydrolysis of water) na kupata hewa ya oksijeni na hydrojeni (H2O = H2 + O2)
Njia hii hutumia umeme kuvunja maji ya kawaida na kupata gesi ya hydrojeni na gesi ya oksijeni ambapo zote zinaweza kuvunwa na kuhifadhiwa.
Ili kupata kilo moja (1kg) ya hydrojeni kupitia njia hii inahitajika kilowati 50 hadi 55 za umeme (50-55kWh).
  • Kuvunjavunja amonia (NH3) (ammonia electrolysis) inayopatikana kwenye majitaka, mabaki na vinyesi vya viumbe hai na kupata hewa ya naitojeni (N2) na Hydrojeni (H2).
Njia hii inahitaji kilowati 1.55 (1.55kWh) ili kupata kilo moja ya gesi ya hydrojeni (1kg). Njia hii inatumia umeme mdogo zaidi ukilinganisha na ya kutumia maji ya kawaida.

View attachment 2986898
Uzalishaji wa nishati ya hydrogeni kwa kutumia ammonia (Picha kutoka mtandaoni)

Kiasi cha umeme kinachotokana na nishati ya hydrojeni
Kwa makadirio kilo moja (1kg) ya hydrojeni inauwezo wa kuchakatwa na kuzalisha umeme kilowati 23 (23kWh). Ili kupata megawati 100 (100mWh) itahitajika walau tani 4.3 za nishati ya hydrojeni.

Faida za kutumia nishati ya hydrojeni kuhifadhi umeme;
Urahisi na unafuu kuzalisha
Ni rahisi kuzalisha nishati ya hydrojeni kutokana na mahitaji yake (maji, majitaka, mabaki ya viumbe hai na vinyesi vya wanyama) kupatikana kwa urahisi. Pia ni nafuu kutokana umeme utakaotumika kuzalisha nishati ya hydrojeni utakua ni ule uliozidi kutoka kwenye vyanzo vingine vya umeme (maji, jua, upepo na jotoardhi ‘geothermal’)
Rafiki wa mazingira.
Mabaki yanayotakana na uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati ya hydrojeni ni maji na joto, vyote hivi huweza kutumika kwa matumizi mengine. Njia hii haizalishi uchafu au hewa chafu kwenye mazingira.
Matumizi mbadala
Nishati ya hydrojeni ina matumizi mengine kama kuendeshea vyombo vya usafiri (magari n.k) na mitambo ya viwandani. Hii ni faida kwani endapo uzalishaji wa umeme usiposhuka chini ya kiwango nishati hii itaweza kuuzwa na kutumika kwenye matumizi mengine.
Usafishaji wa maji na hewa
Uzalishaji wa nishati ya hydojeni kwa kuchakata amonia inayopatikana kwenye majitaka itasaidia kusafisha maji na kuzalisha maji safi yatakayofaa kwa matumizi ya binadamu. Pia kituo cha uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kinaweza kutumika kusafisha hewa kwa kuchuja na kuondoa vumbi linalopatikana kwenye hewa.

Ili jambo hili kufanya kazi kwa ufanisi ni vyema kufanya mambo haya;
  • Kuhakikisha kila kanda inakua na kituo walau kimoja kwa ajili ya mchakato huu,
Itasaidia uzalishaji na uhifadhi mkubwa wa nishati ya hydrojeni. Pia itasaidia kua kama mbadala (backup) pindi itakapotokea hitilafu kubwa kwenye gridi ya taifa jambo ambalo litaepusha nchi nzima kukosa umeme.
Tanzania bara na visiwani kuna jumla ya kanda 10, kila kanda ikiwekewa kituo kimoja chenye uwezo wastani wa kuzalisha umeme megawati 150 kutokana na nishati ya hydrojeni itakayokua imehifadhiwa kwenye vituo hivyo, jumla itawezekana kuzalisha megawati 1500 ambazo zitamaliza kabisa changamoto ya upungufu wa umeme nchini.
  • Kufanya marekebisho kwenye gridi za umeme,
Hii ni kwa ajili ya kuhakikisha kila gridi ya umeme inabeba kiwango cha umeme inachostahili na kuepusha kubeba kiwango kikubwa cha umeme kuzidi uwezo wake jambo ambalo hupelekea kutokea kwa hitilafu za mara kwa mara kwenye gridi za umeme.

Hivyo; uhakika na utoshelezi wa umeme utafanikiwa endapo umeme unaozalishwa utatumika ipasavyo kwa kuhakikisha uwepo wake hata endapo uzalishaji utakaposhuka. Ili kufanikisha hili itahitajika kuhifadhiwa kwa umeme unaozalishwa hasa kwa kutumia njia nafuu na yenye ufanisi mkubwa. Uhakika na utoshelezi wa umeme ni chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmojammoja.
Wazo la nishati mbadala--nishati itokanayo na gesi ya haidrojeni ni shauri maridhawa kabisa.

Ahsante kwa kukumbusha...

Uwezekano wa matumizi ya gesi hii kuleta mapinduzi ya kimaendeleo na ustawi yanafahamika vema kabisa na baadhi 'wataalam' kote duniani; na wala siyo kwamba 'haliwezekani'; ni jambo lenyekuwezekana, >na tena kwa hata gharama ndogo mno ama utalaam<-- hata kupitiliza modalti unayopendekeza.

SASA, >ni vema udadisi zaidi, inawezekanaje/inakuwaje 'nishati mbadala' ni suala linaloratibiwa 'kisiasa-uchumi zaidi'<(?)

Vina sahihi vya uono, tafsiri na dhamira ndivyo vinaweza kuleta mapendekezo sahihi/maridhawa/muafaka ya mabadiliko ya mifumo ya kisiasa-uchumi duniani.

Hili litukumbushe jambo moja, usiamini sana mifumo iliyopo leo duniani kuhusiana na 'uchumi' ama 'siasa' kama ndiyo sahihi sana ama vile kudhani: 'ni kamilifu'.

Mifumo ya leo ya uchumi, siasa na maendeleo ni >'mushkeli'<--japo hutafundishwa hivi kiukweli hasa; ama tuseme: moja kwa moja kwa ELIMU 1.0--elimu inayofanyika kwa misingi ya kutengeneza 'watawala' na 'watawaliwa'.

Ni jitihada binafsi katika Elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo itakayomletea mtu 'busara na mwangaza wa kweli' kwa mintarafu ya kuyafikia 'maisha kwa kujichagulia'.

Maisha kwa misingi ya kujichagulia--dhana halisi ya >'Uhuru wa Ndani'< ndiyo kile hasa Mwalimu Nyerere na wadau wa utu na maendeleo duniani, walipambania 'taifa la Tanzania kufanyikia hivyo.

Kwenye mifumo ya ki-leo ya kiuchumi na siasa, dhana halisi ya kuathirisha misingi ya 'utu na Kujichagulia' ndiyo hugumbikwa na ngendembwe za 'utashi wa kisiasa'; kwamba ili mtu/jamii/taifa/dola iwe huru basi itahitaji 'watu/viongozi bora' wenye 'utashi bora wa kisiasa'...

Kwa minajili hii, jamii yeyote ni pembe tatu ya Mosi, 'Ontolojia ya Taaasisi', Pili, Uono na Tatu, Sura na Mienendo ya Jamii.

UONO ndiyo pembe inayokutanisha 'Siasa za Jamii/Nchi/Taifa' na 'Mipango ya Utekelezaji'.

Kwa namna hii, mifumo ni kiunganishi cha 'Siasa za Jamii/Nchi/Taifa' na 'Mipango ya Utekelezaji'.

Kwa namna hii, mifumo huenda sambamba na miundo ya utendaji na matendo ya wanajamiii.

UONO ndiyo hufafanuliwa kwa misingi ya 'Elimu'; kwamba 'Elimu ndiyo humpatia mwanajamii' mwangaza wa maisha.

Sasa, kwa ulimwengu wa sasa, 2024, elimu si shughuli ya kuleta hasa ule 'Uhuru kwa Kujichagulia' katika mtu/mwanajamii/nchi/dola; bali 'utumwa wa kiakili' ili kunufaisha wale wenye 'kuidhibiti mifumo yenyewe'; kuidhibiti kitaasisi, kupitia 'maoni yanayoratibiwa' na 'malingishiano ya mali'... Ikumbukwe >'Uhuru' ni moja ya tunu nne za taifa, ukiachia 'Haki', 'Udugu' na "Amani'<.

Nishati ni suala mtambuka lenye kuhusiana na 'Malingishiano ya Mali' hapa Duniani. Kwa mintarafu ya hili, nishati ni suala ya usalama wa mataifa--isemwe wazi ama isisemwe wazi.

NIshati ni suala mtambuka linaloweza kumaliza siasa zote za utawala, mabavu ama diplomasia hapa Duniani. Kwa mintarafu ya haya, yote unayoyashuhudia yakiendelea kuhusu upatikanaji wa nishati safi/salama/jadidifu n.k huenda yakawa ni 'michezo inayoratibiwa' hata miongoni mwa wanajamii ama hata watawala--watawala ama/na wasomi... Yanayoratibiwa na >'Vibopa'< wa tawala za duniani.

Nishati ni suala mtambuka linalotumika kuendesha siasa/uchumi wa dunia kwa sheria na sera mbalimbali za kitaifa na mataifa; kwa msingi huu, hali za maisha na maendeleo ya watu zinadhibitiwa kwa sheria na sera zinatafsiria hatua za kuchukua kimipango na utekelezaji wake...

Usihadaike pia na siasa za maazimio ya kimataifa juu ya maendeleo endelevu ya watu duniani; yana utundu wake uliofichiwa kwa ndani wa mataifa yaliyoendelea ama kutokana na wadau 'wakimataifa' wa 'maendeleo-kifedha'...

Kwa minajili ya hili la 'maendeleo-kifedha', nishati ya haidrojeni ni tishio kwa 'uratibu wa maendeleo' kwa matumizi ya sarafu za fedha duniani... >Wapo wadau wa kimataifa ambao wanatekinolojia na maarifa mbali kuzidi 'mtama kwa watoto' wa elimu iliyotamalaki kote duniani --juu ya yote: 'siasa, uchumi na jamii'<....

Hili ndilo litukumbushe jambo moja makini, tusiwe washamba wa visomo vya mchongo vya dunia ama/na elimu za kuhitimu.

Inatupasa 'Kujiongeza na Kujiongoza' ili tuufafafanue na kuupambanua ukweli wa muktadha ulio kwamba >'Maendeleo ni Kujichagulia kupitia kazi'<; ambavyo kazi ndiyo hutegemea nishati, maarifa/ujuzi/tekinolojia na >miundombinu muafaka ya kuhudumia uhitaji wa kibinadamu<.

Kabla ya mashauri ya nishati na mapinduzi ya kitekinolojia, kinachohitajika hasa ni UONO FASAHA miongoni mwa wanajamii wote na dhamira ya dhati ya kujinasibu na mapinduzi hayo.

Serikali na watendaji wake wote hawawezi 'kuyaleta mapinduzi' ya namna hii; kwa kuwa 'kufumua na kuifuma upya' kuna gharama yake--gharama ambayo kwa demokrasia ya kiliberali ni vigumu kulimudu hilo.

Viongozi wa kuja kwa mifumo ya madaraka ya 'miaka mitano mitano' hawaliwezekani hili--ndiyo maana kwa Tanzania, jambo hili liliasisiwa sambamba na harakati za kisiasa-->mwanzo wa Chama cha Mapinduzi, 1977<...

Kiufundi, unalopendekeza--japo laonekana kana vile linawezekana kwa sura ya mikakati ya kimaendeleo; linalonafasi ikiwa wanajamii wengi watarejea katika misingi ya nchi na tawala kadiri ambavyo kile kilichokusudiwa hasa Kikatiba ya Nchi na tena vivyo hivyo katika ya Chama Tawala, Chama cha Wanachi--Chama cha Mapinduzi --kitaeleweka kwa umma wa wengi--maarifa ya >'Mwenge wa Uhuru'<.

'Mwenge wa Uhuru' ni fumbo la imani juu ya >'Nuru ya Ufahamu'<.

Ikiwa kila mwananchi atafahamu kuwa yeye ndiye yeye, >zao la kumea kwa 'Uhuru wa Ndani';< kwamba hatima ya maisha na ustawi wake hautegemei mtu mwingine yeyote kama 'Mtukufu'/'Mheshimiwa/Mkulu/Bwana Mkubwa/Mama la mama/Bosi--mambo yote yanayoweza kuzaa 'mazoea ya uchawa ama/na unafiki' basi, basi nuru ya ufahamu ndiyo ufunguo wa kuzigeuza taasisi zote za 'ulinzi' na 'ustawi' kuwa 'Chachu na Nuru' ya kiutendaji kwa ajili ya yale tunayoweza kuyabaini ni Udugu, Haki na Amani.

Kujitegemea ni dhana iliyo ni zao la 'Nuru ya Ufahamu' katika UTU wa Wanajamii.

"Nuru ya Ufahamu' ikifanyika kwa idadi fulani wanajamii, wenye kuzungumza kwa lugha ya Kiingereza kulitaja hili kama >'Critical Mass'< basi ndiyo tunaweza kuwa na Mageuzi makubwa na ya kweli ya Jamii--Mapinduzi ya Kweli. Hili litukumbushe, Unafiki na Uchawa, ni sumu kwa 'Mapinduzi ya kweli'...

Mapinduzi ya kweli yanatuletea muktadha wa ukweli wa 'Kazi ni Kipimo cha Utu'... Ili kazi iwe ni kipimo cha Mtu, mtu mwenyewe hana budi kuwa ni yule mwenye kujitambua... Mwenge wa Uhuru ni alama ya Utu wenye Kutafuta Kujitambua ama pia kusema 'Kujua Ilivyobora'... Mwenye kujua ilivyobora, huchagua ilivyobora na tena hutenda ilivyobora.

Kutafuta manufaa ya mbadala wa NIshati na Maendeleo ni 'Chaguo'--Zao la 'Kujichagulia' kulingana na kujua ilivyobora. Kujua ilivyobora kunakofanyika na 'mtu aliyezaliwa upya kidhamira za UTU'--mtu 'aliyejivua gamba'...

Ikiwa 'idadi muafaka' ya watu itafanyika hapa Tanzania, mapenzi yako yatatimia kupitia wadau na harakati za wadau wa 'Chama cha Mapinduzi'...

Ujasiri wa wadau wa Chama hichi bado unayofunguo ya >'Tumaini'<...

Kinachochelewesha 'mapinduzi' ni >'Uwele kuchanganyikana na Pumba'<...

Hmmm
 
Wazo la nishati mbadala--nishati itokanayo na gesi ya haidrojeni ni shauri maridhawa kabisa.

Ahsante kwa kukumbusha...

Uwezekano wa matumizi ya gesi hii kuleta mapinduzi ya kimaendeleo na ustawi yanafahamika vema kabisa na baadhi 'wataalam' kote duniani; na wala siyo kwamba 'haliwezekani'; ni jambo lenyekuwezekana, >na tena kwa hata gharama ndogo mno ama utalaam<-- hata kupitiliza modalti unayopendekeza.

SASA, >ni vema udadisi zaidi, inawezekanaje/inakuwaje 'nishati mbadala' ni suala linaloratibiwa 'kisiasa-uchumi zaidi'<(?)

Vina sahihi vya uono, tafsiri na dhamira ndivyo vinaweza kuleta mapendekezo sahihi/maridhawa/muafaka ya mabadiliko ya mifumo ya kisiasa-uchumi duniani.

Hili litukumbushe jambo moja, usiamini sana mifumo iliyopo leo duniani kuhusiana na 'uchumi' ama 'siasa' kama ndiyo sahihi sana ama vile kudhani: 'ni kamilifu'.

Mifumo ya leo ya uchumi, siasa na maendeleo ni >'mushkeli'<--japo hutafundishwa hivi kiukweli hasa; ama tuseme: moja kwa moja kwa ELIMU 1.0--elimu inayofanyika kwa misingi ya kutengeneza 'watawala' na 'watawaliwa'.

Ni jitihada binafsi katika Elimu 2.0 na Elimu 3.0 ndiyo itakayomletea mtu 'busara na mwangaza wa kweli' kwa mintarafu ya kuyafikia 'maisha kwa kujichagulia'.

Maisha kwa misingi ya kujichagulia--dhana halisi ya >'Uhuru wa Ndani'< ndiyo kile hasa Mwalimu Nyerere na wadau wa utu na maendeleo duniani, walipambania 'taifa la Tanzania kufanyikia hivyo.

Kwenye mifumo ya ki-leo ya kiuchumi na siasa, dhana halisi ya kuathirisha misingi ya 'utu na Kujichagulia' ndiyo hugumbikwa na ngendembwe za 'utashi wa kisiasa'; kwamba ili mtu/jamii/taifa/dola iwe huru basi itahitaji 'watu/viongozi bora' wenye 'utashi bora wa kisiasa'...

Kwa minajili hii, jamii yeyote ni pembe tatu ya Mosi, 'Ontolojia ya Taaasisi', Pili, Uono na Tatu, Sura na Mienendo ya Jamii.

UONO ndiyo pembe inayokutanisha 'Siasa za Jamii/Nchi/Taifa' na 'Mipango ya Utekelezaji'.

Kwa namna hii, mifumo ni kiunganishi cha 'Siasa za Jamii/Nchi/Taifa' na 'Mipango ya Utekelezaji'.

Kwa namna hii, mifumo huenda sambamba na miundo ya utendaji na matendo ya wanajamiii.

UONO ndiyo hufafanuliwa kwa misingi ya 'Elimu'; kwamba 'Elimu ndiyo humpatia mwanajamii' mwangaza wa maisha.

Sasa, kwa ulimwengu wa sasa, 2024, elimu si shughuli ya kuleta hasa ule 'Uhuru kwa Kujichagulia' katika mtu/mwanajamii/nchi/dola; bali 'utumwa wa kiakili' ili kunufaisha wale wenye 'kuidhibiti mifumo yenyewe'; kuidhibiti kitaasisi, kupitia 'maoni yanayoratibiwa' na 'malingishiano ya mali'... Ikumbukwe >'Uhuru' ni moja ya tunu nne za taifa, ukiachia 'Haki', 'Udugu' na "Amani'<.

Nishati ni suala mtambuka lenye kuhusiana na 'Malingishiano ya Mali' hapa Duniani. Kwa mintarafu ya hili, nishati ni suala ya usalama wa mataifa--isemwe wazi ama isisemwe wazi.

NIshati ni suala mtambuka linaloweza kumaliza siasa zote za utawala, mabavu ama diplomasia hapa Duniani. Kwa mintarafu ya haya, yote unayoyashuhudia yakiendelea kuhusu upatikanaji wa nishati safi/salama/jadidifu n.k huenda yakawa ni 'michezo inayoratibiwa' hata miongoni mwa wanajamii ama hata watawala--watawala ama/na wasomi... Yanayoratibiwa na >'Vibopa'< wa tawala za duniani.

Nishati ni suala mtambuka linalotumika kuendesha siasa/uchumi wa dunia kwa sheria na sera mbalimbali za kitaifa na mataifa; kwa msingi huu, hali za maisha na maendeleo ya watu zinadhibitiwa kwa sheria na sera zinatafsiria hatua za kuchukua kimipango na utekelezaji wake...

Usihadaike pia na siasa za maazimio ya kimataifa juu ya maendeleo endelevu ya watu duniani; yana utundu wake uliofichiwa kwa ndani wa mataifa yaliyoendelea ama kutokana na wadau 'wakimataifa' wa 'maendeleo-kifedha'...

Kwa minajili ya hili la 'maendeleo-kifedha', nishati ya haidrojeni ni tishio kwa 'uratibu wa maendeleo' kwa matumizi ya sarafu za fedha duniani... >Wapo wadau wa kimataifa ambao wanatekinolojia na maarifa mbali kuzidi 'mtama kwa watoto' wa elimu iliyotamalaki kote duniani --juu ya yote: 'siasa, uchumi na jamii'<....

Hili ndilo litukumbushe jambo moja makini, tusiwe washamba wa visomo vya mchongo vya dunia ama/na elimu za kuhitimu.

Inatupasa 'Kujiongeza na Kujiongoza' ili tuufafafanue na kuupambanua ukweli wa muktadha ulio kwamba >'Maendeleo ni Kujichagulia kupitia kazi'<; ambavyo kazi ndiyo hutegemea nishati, maarifa/ujuzi/tekinolojia na >miundombinu muafaka ya kuhudumia uhitaji wa kibinadamu<.

Kabla ya mashauri ya nishati na mapinduzi ya kitekinolojia, kinachohitajika hasa ni UONO FASAHA miongoni mwa wanajamii wote na dhamira ya dhati ya kujinasibu na mapinduzi hayo.

Serikali na watendaji wake wote hawawezi 'kuyaleta mapinduzi' ya namna hii; kwa kuwa 'kufumua na kuifuma upya' kuna gharama yake--gharama ambayo kwa demokrasia ya kiliberali ni vigumu kulimudu hilo.

Viongozi wa kuja kwa mifumo ya madaraka ya 'miaka mitano mitano' hawaliwezekani hili--ndiyo maana kwa Tanzania, jambo hili liliasisiwa sambamba na harakati za kisiasa-->mwanzo wa Chama cha Mapinduzi, 1977<...

Kiufundi, unalopendekeza--japo laonekana kana vile linawezekana kwa sura ya mikakati ya kimaendeleo; linalonafasi ikiwa wanajamii wengi watarejea katika misingi ya nchi na tawala kadiri ambavyo kile kilichokusudiwa hasa Kikatiba ya Nchi na tena vivyo hivyo katika ya Chama Tawala, Chama cha Wanachi--Chama cha Mapinduzi --kitaeleweka kwa umma wa wengi--maarifa ya >'Mwenge wa Uhuru'<.

'Mwenge wa Uhuru' ni fumbo la imani juu ya >'Nuru ya Ufahamu'<.

Ikiwa kila mwananchi atafahamu kuwa yeye ndiye yeye, >zao la kumea kwa 'Uhuru wa Ndani';< kwamba hatima ya maisha na ustawi wake hautegemei mtu mwingine yeyote kama 'Mtukufu'/'Mheshimiwa/Mkulu/Bwana Mkubwa/Mama la mama/Bosi--mambo yote yanayoweza kuzaa 'mazoea ya uchawa ama/na unafiki' basi, basi nuru ya ufahamu ndiyo ufunguo wa kuzigeuza taasisi zote za 'ulinzi' na 'ustawi' kuwa 'Chachu na Nuru' ya kiutendaji kwa ajili ya yale tunayoweza kuyabaini ni Udugu, Haki na Amani.

Kujitegemea ni dhana iliyo ni zao la 'Nuru ya Ufahamu' katika UTU wa Wanajamii.

"Nuru ya Ufahamu' ikifanyika kwa idadi fulani wanajamii, wenye kuzungumza kwa lugha ya Kiingereza kulitaja hili kama >'Critical Mass'< basi ndiyo tunaweza kuwa na Mageuzi makubwa na ya kweli ya Jamii--Mapinduzi ya Kweli. Hili litukumbushe, Unafiki na Uchawa, ni sumu kwa 'Mapinduzi ya kweli'...

Mapinduzi ya kweli yanatuletea muktadha wa ukweli wa 'Kazi ni Kipimo cha Utu'... Ili kazi iwe ni kipimo cha Mtu, mtu mwenyewe hana budi kuwa ni yule mwenye kujitambua... Mwenge wa Uhuru ni alama ya Utu wenye Kutafuta Kujitambua ama pia kusema 'Kujua Ilivyobora'... Mwenye kujua ilivyobora, huchagua ilivyobora na tena hutenda ilivyobora.

Kutafuta manufaa ya mbadala wa NIshati na Maendeleo ni 'Chaguo'--Zao la 'Kujichagulia' kulingana na kujua ilivyobora. Kujua ilivyobora kunakofanyika na 'mtu aliyezaliwa upya kidhamira za UTU'--mtu 'aliyejivua gamba'...

Ikiwa 'idadi muafaka' ya watu itafanyika hapa Tanzania, mapenzi yako yatatimia kupitia wadau na harakati za wadau wa 'Chama cha Mapinduzi'...

Ujasiri wa wadau wa Chama hichi bado unayofunguo ya >'Tumaini'<...

Kinachochelewesha 'mapinduzi' ni >'Uwele kuchanganyikana na Pumba'<...

Hmmm
Hakika
 
Uzalishaji wa umeme unapokidhi mahitaji nchini unachangia kwenye ukuaji wa uchumi kutokana na shughuli nyingi za viwanda vikubwa na vidogo kuendeshwa kwa utegemezi wa umeme Umeme unapokua wa uhakika uzalishaji wa bidhaa huongezeka na gharama za uendeshaji hupungua.
Naaam naaaam, hakika. Haiya twende kazi...

Njia nzuri ni kuhifadhi umeme unaozalishwa na kuweza kuutumia pindi uzalishaji utakapokua mdogo. Itafanyika endapo uzalishaji wa umeme utazidi kiwango cha matumizi na kupelekea umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa. Njia nzuri na nafuu ni kuhifadhi umeme kupitia nishati ya hydrojeni. Ili kuzuia umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa, umeme utakaozidi utatumika kuzalisha gesi ya hydrojeni na kuhifadhiwa. Umeme utakapopungua kwenye gridi gesi hiyo itatumika kuzalisha umeme na kurudishwa kwenye gridi kwa ajili ya kuepusha kukatika/mgao wa umeme.
Teknolojia nzitonzito hizi....

  • Kuvunjavunja amonia (NH3) (ammonia electrolysis) inayopatikana kwenye majitaka, mabaki na vinyesi vya viumbe hai na kupata hewa ya naitojeni (N2) na Hydrojeni (H2).
Njia hii inahitaji kilowati 1.55 (1.55kWh) ili kupata kilo moja ya gesi ya hydrojeni (1kg). Njia hii inatumia umeme mdogo zaidi ukilinganisha na ya kutumia maji ya kawaida.
Kama ulivyosema inahitaji nishati ndogo, zaidi lakini katika suala hili ni kwamba umeme unakuwa umezidia, hivyo labda tusichukue chaguo la umeme kidogo. Labda tuangalie usalama zaidi au unaonaje mtoa mada?

Yaani kugombana na maji kuyavunja ni salama kuliko kugombana na ammonia na kuivunja.

  • uhakikisha kila kanda inakua na kituo walau kimoja kwa ajili ya mchakato huu,
Itasaidia uzalishaji na uhifadhi mkubwa wa nishati ya hydrojeni. Pia itasaidia kua kama mbadala (backup) pindi itakapotokea hitilafu kubwa kwenye gridi ya taifa jambo ambalo litaepusha nchi nzima kukosa umeme.
Huwa ninalipenda wazo la kuwa na umeme ambao upo na backup ya kikanda, kweli bro kiusalama wa kitaifa suala la kuwa na sehemu moja tu inayotema umeme nchi nzima aio wazo zuri. Ahsante
Uhakika na utoshelezi wa umeme ni chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmojammoja.
Again, wazo murua sana hili👏
 
Pia hata yakitumika maji safi, athari haitokua kubwa kutokana na kwamba wakati wa kuzalisha umeme, maji pia yanazalishwa kwaiyo ni kama maji yanarudishwa kwenye mazingira.
Exactly....Na unaweza kukazia kwamba hilo ni betrii tu, mwisho wa siku tukiurudisha mchakato mwanzo tunayapata maji na mchakato unaoturudishia umeme uliohifadhiwa. Au mie ndo sijaelewa🤔🤔
 
Naaam naaaam, hakika. Haiya twende kazi...


Teknolojia nzitonzito hizi....


Kama ulivyosema inahitaji nishati ndogo, zaidi lakini katika suala hili ni kwamba umeme unakuwa umezidia, hivyo labda tusichukue chaguo la umeme kidogo. Labda tuangalie usalama zaidi au unaonaje mtoa mada?

Yaani kugombana na maji kuyavunja ni salama kuliko kugombana na ammonia na kuivunja.


Huwa ninalipenda wazo la kuwa na umeme ambao upo na backup ya kikanda, kweli bro kiusalama wa kitaifa suala la kuwa na sehemu moja tu inayotema umeme nchi nzima aio wazo zuri. Ahsante

Again, wazo murua sana hili👏
Asante sana
 
Exactly....Na unaweza kukazia kwamba hilo ni betrii tu, mwiaho wa siku tukiurudisha mchakato mwanzo tunayapata maji na mchakato unaoturudishia umeme uliohifadhiwa. Au mie ndo sijaelewa🤔🤔
Upo sawa kabisa, ni kama cycle hivi inafanyika, mwanzo umeme unatumika kuvunja maji tunapata gesi ya oksijeni na hydrojeni, na baadae hydrogen na oksijeni zinaungana kutengeneza maji wakati huo umeme unazalishwa.
 
Uzalishaji wa umeme unapokidhi mahitaji nchini unachangia kwenye ukuaji wa uchumi kutokana na shughuli nyingi za viwanda vikubwa na vidogo kuendeshwa kwa utegemezi wa umeme Umeme unapokua wa uhakika uzalishaji wa bidhaa huongezeka na gharama za uendeshaji hupungua.

Wananchi waliojiajiri kupitia shughuli zinazotegemea umeme huepuka hasara ya kuharibikiwa na bidhaa, na kwa kushindwa kuendesha shughuli zao kwa ufanisi. Jambo ambalo huwakatisha tamaa na kuwarudisha nyuma kiuchumi.

Changamoto kubwa kwenye uzalishaji wa umeme ni kwamba umeme unahitajika kuwepo kwa kiwango sahihi kwenye gridi. Kiwango kilichopo kwenye gridi kisizidi au kupungua kiwango cha matumizi.

Hivi sasa Tanzania baada ya kuwasha baadhi ya mashine za kuzalisha umeme kwenye bwawa la Nyerere tumeshuhudia umeme ukizalishwa kupita kiasi hali inayopelekea kuzima baadhi ya mashine kuepuka changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa.

Bwawa la nyerere linaweza kuzalisha megawati 2115, kwa mwaka 2023 uhitaji wa umeme nchini ilikua ni megawati 1363.94. Ingawa uhitaji wa umeme huongezeka kadiri siku zinavyokwenda kutokana na matumizi kuongezeka.

Uzalishaji wa umeme wa maji huathiriwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Uzalishaji kupungua yanapotimu majira ya kiangazi na kipindi cha ukame kutokana na mabwawa kupungua kina hivyo nguvu ya maji inayozungusha mashine za kuzalisha umeme kupungua.

Changamoto kubwa nyingine ni hitilafu za mara kwa mara zitokeazo kwenye gridi ya taifa jambo ambalo hupelekea ukosefu wa umeme kwa saa kadhaa kwenye maeneo mengi nchini.

Nishati ya hydrogeni suluhisho la upungufu/kuzidi umeme na hitilafu kwenye gridi ya taifa;
Ingawa changamoto ya umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa inaweza kutatuliwa kwa kuuza umeme nchi jirani, lakini swali la kujiuliza ni Je, umeme huo utakua wa uhakika kwa kipindi chote? Hii ni ili kuepuka kushindwa kusambaza umeme wa uhakika pindi itakapotokea upungufu wa uzalishaji au hitilafu kwenye gridi ya taifa au kuongeka kwa matumizi ya umeme nchini.

Kuepuka changamoto hii ni vizuri kuchagua njia nzuri na sahihi ya kukabiliana na changamoto za umeme nchini. Njia ambayo itaweza kutumika kwenye matumizi mengine endapo hakutotokea upungufu wa umeme.

Njia nzuri ni kuhifadhi umeme unaozalishwa na kuweza kuutumia pindi uzalishaji utakapokua mdogo. Itafanyika endapo uzalishaji wa umeme utazidi kiwango cha matumizi na kupelekea umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa. Njia nzuri na nafuu ni kuhifadhi umeme kupitia nishati ya hydrojeni. Ili kuzuia umeme kuzidi kwenye gridi ya taifa, umeme utakaozidi utatumika kuzalisha gesi ya hydrojeni na kuhifadhiwa. Umeme utakapopungua kwenye gridi gesi hiyo itatumika kuzalisha umeme na kurudishwa kwenye gridi kwa ajili ya kuepusha kukatika/mgao wa umeme.

Uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme unavyofanyika;
Zipo njia kuu mbili za kuzalisha nishati ya hydrojeni kwa kutumia umeme ambazo ni rafiki wa mazingira.
  • Kuvunjavunja maji (hydrolysis of water) na kupata hewa ya oksijeni na hydrojeni (H2O = H2 + O2)
Njia hii hutumia umeme kuvunja maji ya kawaida na kupata gesi ya hydrojeni na gesi ya oksijeni ambapo zote zinaweza kuvunwa na kuhifadhiwa.
Ili kupata kilo moja (1kg) ya hydrojeni kupitia njia hii inahitajika kilowati 50 hadi 55 za umeme (50-55kWh).
  • Kuvunjavunja amonia (NH3) (ammonia electrolysis) inayopatikana kwenye majitaka, mabaki na vinyesi vya viumbe hai na kupata hewa ya naitojeni (N2) na Hydrojeni (H2).
Njia hii inahitaji kilowati 1.55 (1.55kWh) ili kupata kilo moja ya gesi ya hydrojeni (1kg). Njia hii inatumia umeme mdogo zaidi ukilinganisha na ya kutumia maji ya kawaida.

View attachment 2986898
Uzalishaji wa nishati ya hydrogeni kwa kutumia ammonia (Picha kutoka mtandaoni)

Kiasi cha umeme kinachotokana na nishati ya hydrojeni
Kwa makadirio kilo moja (1kg) ya hydrojeni inauwezo wa kuchakatwa na kuzalisha umeme kilowati 23 (23kWh). Ili kupata megawati 100 (100mWh) itahitajika walau tani 4.3 za nishati ya hydrojeni.

Faida za kutumia nishati ya hydrojeni kuhifadhi umeme;
Urahisi na unafuu kuzalisha
Ni rahisi kuzalisha nishati ya hydrojeni kutokana na mahitaji yake (maji, majitaka, mabaki ya viumbe hai na vinyesi vya wanyama) kupatikana kwa urahisi. Pia ni nafuu kutokana umeme utakaotumika kuzalisha nishati ya hydrojeni utakua ni ule uliozidi kutoka kwenye vyanzo vingine vya umeme (maji, jua, upepo na jotoardhi ‘geothermal’)
Rafiki wa mazingira.
Mabaki yanayotakana na uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati ya hydrojeni ni maji na joto, vyote hivi huweza kutumika kwa matumizi mengine. Njia hii haizalishi uchafu au hewa chafu kwenye mazingira.
Matumizi mbadala
Nishati ya hydrojeni ina matumizi mengine kama kuendeshea vyombo vya usafiri (magari n.k) na mitambo ya viwandani. Hii ni faida kwani endapo uzalishaji wa umeme usiposhuka chini ya kiwango nishati hii itaweza kuuzwa na kutumika kwenye matumizi mengine.
Usafishaji wa maji na hewa
Uzalishaji wa nishati ya hydojeni kwa kuchakata amonia inayopatikana kwenye majitaka itasaidia kusafisha maji na kuzalisha maji safi yatakayofaa kwa matumizi ya binadamu. Pia kituo cha uzalishaji wa nishati ya hydrojeni kinaweza kutumika kusafisha hewa kwa kuchuja na kuondoa vumbi linalopatikana kwenye hewa.

Ili jambo hili kufanya kazi kwa ufanisi ni vyema kufanya mambo haya;
  • Kuhakikisha kila kanda inakua na kituo walau kimoja kwa ajili ya mchakato huu,
Itasaidia uzalishaji na uhifadhi mkubwa wa nishati ya hydrojeni. Pia itasaidia kua kama mbadala (backup) pindi itakapotokea hitilafu kubwa kwenye gridi ya taifa jambo ambalo litaepusha nchi nzima kukosa umeme.
Tanzania bara na visiwani kuna jumla ya kanda 10, kila kanda ikiwekewa kituo kimoja chenye uwezo wastani wa kuzalisha umeme megawati 150 kutokana na nishati ya hydrojeni itakayokua imehifadhiwa kwenye vituo hivyo, jumla itawezekana kuzalisha megawati 1500 ambazo zitamaliza kabisa changamoto ya upungufu wa umeme nchini.
  • Kufanya marekebisho kwenye gridi za umeme,
Hii ni kwa ajili ya kuhakikisha kila gridi ya umeme inabeba kiwango cha umeme inachostahili na kuepusha kubeba kiwango kikubwa cha umeme kuzidi uwezo wake jambo ambalo hupelekea kutokea kwa hitilafu za mara kwa mara kwenye gridi za umeme.

Hivyo; uhakika na utoshelezi wa umeme utafanikiwa endapo umeme unaozalishwa utatumika ipasavyo kwa kuhakikisha uwepo wake hata endapo uzalishaji utakaposhuka. Ili kufanikisha hili itahitajika kuhifadhiwa kwa umeme unaozalishwa hasa kwa kutumia njia nafuu na yenye ufanisi mkubwa. Uhakika na utoshelezi wa umeme ni chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi na uchumi wa mtu mmojammoja.
kazi nzuri!
 
Back
Top Bottom