Unajua umri nao unakuwaga tatizo sana nakumbuka nilikuwa kama na miaka 20 hivi,naye alikuwa sister du fulani wa miaka hiyoMasaa yote 9 ulikua umeweka kinyongo why huyo dada hakukusalimia na alivyokusalimia ndio kinyongo kikafunguka mkaanza kuongea duuh nyie wababa mnashida aiseee, wakati kitendo cha kukutana tena kwenye landlover ungemwambia "ooh kumbe bado tupo njia moja.... unaenda wapi?" from there mngeendeleza stories,
Jando la porini muhimu😄
Nina visa vingi,hii ilikula kwangu,Nilikuwa nimetoka Maputo napitia Lilogwe to Dar,sasa nilipofika lilogwe kulikuwa na Mabasi ya kampuni ya Taqwa yanayokwenda Dar,na hapo lilongwe palikuwa na wabongo wengi sana wake kwa waume,yaani ukifika kwenye mtaa mmoja unaitwa devil street ni kiswahili tu,
Basi nikapata basi mapema tu,ilikuwa kama saa moja usiku na basi linaondoka saa mbili,baada ya mda akaja dada mmoja wa kitanzania akaniambia umekaa kwenye siti yangu,nilikuwa nimekaa dirishani,nikamwambia siti yangu,akataja namba yake ya siti na mimi nikaitaji hiyoyo kwa kumzingua,ikabidi akamuite konda,alipokuja konda nikampisha,lakini nikamwambia huko ndiko mabasi yanakopigwagwa pasi,
Safari ikaanza kila mtu kamchunia mwenzake,dada mzuri,si unajua wafanya biashara,basi baada ya kama masaa matatu nakaanza kujisikia homa natetemeka mpaka yule dada ananisikia,akaniuliza vipi unaumwa,nikamwambia ndiyo,una dawa hapana,akatoa dawa akanipa,nikawa nimezishika tu,niakulizwa tena unamaji sina,akanipa niakanywa hapo hali ikatulia nikapata usingizi,bado tuko kimya na usiku kama saa tano hivi,
Niasema basi ikifika mji mmoja unaitwa Mzuzu nitaenda kumnunulia maji yake nimrudishie,kweli niakanunua maji kumpa akakataa,niliona aibu sana hapo milango kama ya saa nane,tukafika borde ya Malawi Songwe alfajiri saa 12 ikabidi tuanze storie sasa na kupiga supu wote,kugonga paspoti hapo tukaanza safari ya Kasumulu tu.Dar kalibu masaa 15 tulipiga storie sana mpaka safari ilikuwa fupi kulaliana ruksa,dada akaishia kunipa namba yake ya simu,kipindi hicho simu za mkononi,call box, alikuwa anakaa sinza mimi nafikia Guest,kutokana na protocol ya biashara yangu sikumtafuta tukaishiana hivyo ilikuwa mwaka 1998 kama sikosei