Elections 2015 Nitagombea Ubunge Kyerwa 2015 kwa tiketi ya CHADEMA

Elections 2015 Nitagombea Ubunge Kyerwa 2015 kwa tiketi ya CHADEMA

Nyami2010

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2009
Posts
227
Reaction score
50
WanaJamvi

Ninatangaza nia ya kugombea Ubunge kupitia CHADEMA 2015 katika Jimbo la Kyerwa-Kagera. Uwezo wa kuwa mbunge ninao na nia ninayo. Mbunge wetu wa sasa Mhe. Yustace Katagira, amekuwa mbunge tokea 1995 kwa tiketi ya CCM, japo 2000-2005 alipumzishwa na TLP, na akarejea tena 2005-2010 na 2010-2015. CCM kwetu haitusaidii hata kamwe. Mbunge wetu wetu ni mzee (70+), ni mfanya biashara wa kahawa(zao kuu la biashara jimboni kwake-imagine), na huwa haendi Bungeni(mtoro namba moja). Kyerwa nzima yenye wakazi takribani 400,000 haina shule hata moja ya A-level, haina hata Mita moja ya rami, maji ndo usiseme, haina hospitali, haina chuo chochote, hakuna hata nyumba moja yenye umeme, barabara ni tabu kuliko maelezo...ni shida tu. Ni Mzee ambae amekaa kimaslahi zaidi kuliko kuwatumikia wananchi.

Hivyo, wapendwa wanaJamvi nimeamua kwa dhati nijitose kupambana na Mzee huyu kigogo wa CCM ili CHADEMA ipeperushe bendera yake Kyerwa. Naombeni sala na dua zenu juu ya nia yangu ya kuwakomboa wananchi wetu.

Ninahitimisha
:israel:
 
Nani wewe mbona hatukujui kwenye ujenzi wa chama chetu. Lakini mda bado upo na nafurahi idadi ya wanotaka kugombea inaongezeka kwa kasi, cha muhimu Ujitokeze tukupime uwezo wako ,hatuitaji kubahatisha 2015.
 
Tunaomba tukufahamu kwanza. Weka CV yako. Hata hivyo naomba nikuahidi kura yangu endapo:

1. Una dhamira ya dhati ya kuwasaidia wananchi wa Kyerwa, ambao naona bado hawajapata uhuru wa kiuchumi na maendeleo hadi leo
2. Utagombea CDM, na siyo chama kingine chochote
 
Mkuu kinacho anagaliwa kwa sasa CHADEMA je mchango wako katika kujenga chama uko vipi? so anza sasa kujenga Chama huko kwenu Piga M4C za kutosha huko, na ukifanya hivyo hakika utafanikiwa. 2015 hakutakuwepo na wale wanao kurupuka tu na kusema nagombea, Wagombea wote walisha anza kazi majimboni mwao kupiga Darasa
 
Kyerwa, nakumbuka 2011 nilikuwa anga hizo duhhhhh....
Kutoka Kayanga kwenda Kyerwa ni vumbi zito, kazi ya CCM kwa miaka 50 ya Uhuru ni kuhakikisha barabara hiyo inakuwa mbaya kila uchao
 
Kila lakheri katika kuutafuta Uhuru na amani iliyo pokonywa na mkoloni mweusi.
 
Mkuu kinacho anagaliwa kwa sasa CHADEMA je mchango wako katika kujenga chama uko vipi? so anza sasa kujenga Chama huko kwenu Piga M4C za kutosha huko, na ukifanya hivyo hakika utafanikiwa. 2015 hakutakuwepo na wale wanao kurupuka tu na kusema nagombea, Wagombea wote walisha anza kazi majimboni mwao kupiga Darasa
Haswa, awasilishe jina kwa Katibu Mkuu, tumpime kwenye M4C. Sijui ana unit ngapi za M4C. Aangalie pia udiwani.
 
Kyerwa, nakumbuka 2011 nilikuwa anga hizo duhhhhh....
Kutoka Kayanga kwenda Kyerwa ni vumbi zito, kazi ya CCM kwa miaka 50 ya Uhuru ni kuhakikisha barabara hiyo inakuwa mbaya kila uchao

Mkuu kwenye Red hapo sio kutoka Kayanga ni kutoka Omurushaka Nyakasana, Rugalama, Ihanda hadi huko Kyerwa barabara ni Vumbi la kufa Mtu na Raia wa Jimbo hilo ni Masikini sana hata Kiswahili hawakijui kabisa.Huyu Mzee katagira ni Janga la Jimbo tena anawanyanganya Wanachi Mashamba yao.Kwa Ushahidi kama kuna Member humu yuko Kayanga aende Mahakama ya Wilaya pale atakutana na Kesi ya Katagira inayohusu Mashamba na Unyanganyaji wake wa kahawa kwa Wananchi.Last Month nilikuwa huko.Katagira na Blandesi Mbunge wa Karagwe ni Wezi na Majangili wa Pembe za Ndovu kule Omukaliro na Kimisi.Pia wana Nyavu haramu za kunasia samaki kwenye mito na Maziwa Madogo madogo yanayozunguka wilaya ya Karagwe.
 
Peleka jina kwa katibu mkuu tuanze kukupima.

Jina lipo tayari kwenye ROSTER ya CDM. CV yangu ni kubwa kiukweli na usiwe na shaka na hilo.

Hakika Kyerwa inatawaliwa kimabavu na Mhe. Katagira na kundi lake la wafanya biashara wa kahawa na wafugaji. Amehakikisha CCM imeikamata hadi NEC amemuweka Partner wake kwenye biashara ya kahawa ambaye ni STD II na raia wa Uganda. CCM Kyerwa ni janga la Jimbo na Taifa.
 
Nani wewe mbona hatukujui kwenye ujenzi wa chama chetu. Lakini mda bado upo na nafurahi idadi ya wanotaka kugombea inaongezeka kwa kasi, cha muhimu Ujitokeze tukupime uwezo wako ,hatuitaji kubahatisha 2015.

Wakuu,

Inapendeza kuona wenye nia ni wengi (nikiwa kwenye hiyo list pia). Naamini kazi kubwa ya kulikomboa Taifa ili kutoka mikononi mwa Mafisadi si kupitia ubunge tu. Tukiunganisha nguvu inawezekana.
 
Hongera!
Nimekaa huko kwa wiki kadhaa nimeona mwamko ni mkubwa kuna fursa nyingi za kiuchumi ila hakuna wakziamsha.Ndizi zinabebwa kwa baiskeli hadi mpakani Uganda zinauzwa kwa bei nzuri tu!Natumaini watu wa huko ni waelewa watakuunga mkono! Nimeona kila mahali kuna bendera za chadema ......Huo ni mwanzo mzuri
Sasa JAMAA kama anakaa huko mbona hoteli yake pale Kaisho ni chafu vile!
 
WanaJamvi

Ninatangaza nia ya kugombea Ubunge kupitia CHADEMA 2015 katika Jimbo la Kyerwa-Kagera. Uwezo wa kuwa mbunge ninao na nia ninayo. Mbunge wetu wa sasa Mhe. Yustace Katagira, amekuwa mbunge tokea 1995 kwa tiketi ya CCM, japo 2000-2005 alipumzishwa na TLP, na akarejea tena 2005-2010 na 2010-2015. CCM kwetu haitusaidii hata kamwe. Mbunge wetu wetu ni mzee (70+), ni mfanya biashara wa kahawa(zao kuu la biashara jimboni kwake-imagine), na huwa haendi Bungeni(mtoro namba moja). Kyerwa nzima yenye wakazi takribani 400,000 haina shule hata moja ya A-level, haina hata Mita moja ya rami, maji ndo usiseme, haina hospitali, haina chuo chochote, hakuna hata nyumba moja yenye umeme, barabara ni tabu kuliko maelezo...ni shida tu. Ni Mzee ambae amekaa kimaslahi zaidi kuliko kuwatumikia wananchi.

Hivyo, wapendwa wanaJamvi nimeamua kwa dhati nijitose kupambana na Mzee huyu kigogo wa CCM ili CHADEMA ipeperushe bendera yake Kyerwa. Naombeni sala na dua zenu juu ya nia yangu ya kuwakomboa wananchi wetu.

Ninahitimisha
:israel:

Utajenga barabara? utajenga shule? utapeleka umeme? jipime kwanza kabla hujaamua, pia ongea na mkurugenzi wa halmashauri akueleze kwa nini wameshindwa kutekeleza vyote hivyo? ukipata jibu the anza kazi ya kujijenga kwenye jimbo.
 
Ni vema kutangaza nia hasa kwa vijana ambao nina hakika wana nguvu kiakili na kimwili.
Lakini kwa sasa nguvu kubwa itumike kujenga chama kupitia kampeni zake za M4C, n.k. Ukiwa kama mdau ni vema ukaongoza kampeni hizo kwa kushirikiana na makamanda wengine wenye mapenzi mema na nchi hii ili uchaguzi utakapofika iwe ni kicheko tu. Na hapo utakuwa unajivunia kuvuna matunda ya kazi yako.
 
Hongera saaana kamanda, tuko pamoja. jitahidi uwe na mawasiliano ya karibu na makamanda wazoefu wakupe mbinu na mikakati ya kuhakikisha ndoto yako inatimia. Pipoooooooooooooooooooooooooz Pawaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!
 
Hongera kwa maamuzi yako, lakini ni vizuri nia yako ikijulikana kwa wananchi wako pia na uoneshe mchango wako kuanzia sasa hivi.... On the other side, nina wasiwasi na ujasiri wako. Kama umeshindwa kuweka jina lako kamili hapo, utapata wapi ujasiri wa kukabiliana wa mafisadi katika jimbo lako? Jipange ndugu ili usije ukatuangusha
 
Hongera kwa maamuzi yako, lakini ni vizuri nia yako ikijulikana kwa wananchi wako pia na uoneshe mchango wako kuanzia sasa hivi.... On the other side, nina wasiwasi na ujasiri wako. Kama umeshindwa kuweka jina lako kamili hapo, utapata wapi ujasiri wa kukabiliana wa mafisadi katika jimbo lako? Jipange ndugu ili usije ukatuangusha

Sidhani kama wote tuliopo hapa Jamvini tunaweka majina yetu. Mie naona kama Kamanda ameamua tumpe moyo ili kazi ya ukombozi wa nchi toka mikononi mwa mafisadi na watoto wao iwe rahisi.

Big up Kamanda, go ahead am praying for you!
 
Sidhani kama wote tuliopo hapa Jamvini tunaweka majina yetu. Mie naona kama Kamanda ameamua tumpe moyo ili kazi ya ukombozi wa nchi toka mikononi mwa mafisadi na watoto wao iwe rahisi.

Big up Kamanda, go ahead am praying for you!

Mimi nimeweka jina langu halisi, nina uhakika wengi wasioweka majina yao halisi bila sababu za msingi hawajiamini. Pia nafikiri ili aweze kusaidiwa ni vizuri akaweka jina lake halisi. Jina alilotumia litafanya wengine waone kuwa anafanya mzaha.
 
Back
Top Bottom