Elections 2015 Nitagombea Ubunge Kyerwa 2015 kwa tiketi ya CHADEMA

Elections 2015 Nitagombea Ubunge Kyerwa 2015 kwa tiketi ya CHADEMA

Utajenga barabara? utajenga shule? utapeleka umeme? jipime kwanza kabla hujaamua, pia ongea na mkurugenzi wa halmashauri akueleze kwa nini wameshindwa kutekeleza vyote hivyo? ukipata jibu the anza kazi ya kujijenga kwenye jimbo.


jibu ni rahisi tu hapo , ni ufisadi uliokithiri wa chama cha mapinduzi na halmashauri zote zinazoongozwa na ccm.
 
Mkuu kwenye Red hapo sio kutoka Kayanga ni kutoka Omurushaka Nyakasana, Rugalama, Ihanda hadi huko Kyerwa barabara ni Vumbi la kufa Mtu na Raia wa Jimbo hilo ni Masikini sana hata Kiswahili hawakijui kabisa.Huyu Mzee katagira ni Janga la Jimbo tena anawanyanganya Wanachi Mashamba yao.Kwa Ushahidi kama kuna Member humu yuko Kayanga aende Mahakama ya Wilaya pale atakutana na Kesi ya Katagira inayohusu Mashamba na Unyanganyaji wake wa kahawa kwa Wananchi.Last Month nilikuwa huko.Katagira na Blandesi Mbunge wa Karagwe ni Wezi na Majangili wa Pembe za Ndovu kule Omukaliro na Kimisi.Pia wana Nyavu haramu za kunasia samaki kwenye mito na Maziwa Madogo madogo yanayozunguka wilaya ya Karagwe.

Mze ISI yaonekana wewe wa ihanda?kuna sehemu inaitwa ihanda rabarogi, rwenjoju,kitwekyenkura nk. Jitaid umung'oe katag,ata blandes ni wa kuondoka. Wasliana na daud kahangwa ili akupe mkakati wa kuwaondoa
 
Kila raheli, ila CCM wanaiba sana kura huko. Si uliona jirani zao karagwe walivyolizwa 2010. Saa ya ukombozi KYERWA IMEFIKA.
 
Hebu ona sugu alivyo shusha hadhi ya ubunge,kila mtu anautaka ubunge sasa.
 
Asante kwa kuonesha nia ya kuwa miongoni mwa watu wanaotaka kuhamasisha maendeleo katika jimbo hilo. Je unajua matatizo halisi ya wana Kyerwa? Je unazo njia mbadala za kuwawezesha wanachi kukabiliana na matatizo hayo? Kumbuka watu wengi sasa hawataki tena maneno ya kufikirika. Wanahitaji mtu mwenye solution ya matatizo yao na si mtu anayelist matatizo yao maana wanayajua. Nitafurahi kama utakuwa na solution zaidi kuliko maneno. Najua kuna matatizo ya elimu, hakuna shule ya serikali yenye bweni, maabara na library za maana. Ni majengo yasiyokidhi hata kuitwa ivyo. Mathalani nimeangalia kwa haraka haraka kwa shule za serikali 6 kwa matokeo ya sasa wanafunzi waliopata Divion one ni 1, Division two ni 2, Division three 12, Division four 141 na Zero 455 (Ibanda, Nwenda, Mabira, Kyerwa, Ntare na Rukulaijo) Sasa unamipngo gani kukabiliana na tatazi la elimu, same kwa afya, maji , barabara na mengiyo. Karibu tunawakaribisha mtatukuta.
 
Hivi hili ndio jimbo alilokuwa akiliwakilisha ndugu BENEDICTO MUTUNGIREHI kati ya mwaka 2000-2005?
 
Nyami2010,
Pongezi kwa kutangaza nia mapema. Ni jambo jema na la kuungwa mkono iwapo una nia ya dhati na Uwezo wa kutimiza kile wanachokihitaji wapiga kura. Pamoja na kukutakia mafanikio, hofu yangu ni moja; Wengi wa walio na nia ya kuutafuta Uongozi wa kipindi kijacho wanarudia makosa ya watangulizi wao katika kutangaza nia za kugombea nafasi mbalimbali. Wanazungumzia hatua ya pili kabla ya kufikiri watapitaje hatua ya kwanza.

Nina hakika mwaka 2015 ndani ya vyama vya upinzani hakutakuwa na uteuzi kama tulivyozoea huko nyuma bali kutakuwa na uchaguzi. Utakuwa uchaguzi wenye ushindani mkali sana katika baadhi ya majimbo. Hata baadhi ya walio wabunge wa upinzania kwa sasa, 2015 watapingwa ndani ya vyama vyao.

Nimekutana na watu mbalimbali katika nyakati na mazungumzo tofauti tofauti wakiwa tayari wanajitambulisha kama Wabunge wa Majimbo husika kwa kipindi kijacho 2015-2020! Na mara nyingi kama si mara zote hawa "wabunge" wanajinasibu kuupata Ubunge kupitia chama kile kile. Hata wakati mwingine nakutana na watu zaidi ya watatu kwa nyakati tofauti na wote wanajitambulisha ni Wabunge watarajiwa wa eneo lieliele kupitia chama kile kile kwa kipindi kilekile 2015-2020! Unaweza kubashiri toka leo hicho chama kitakuwa na hali ngumu kiasi gani muda ukifika wa kuwapata wagombea.

Rai yangu kwa "wabunge" watarajiwa wanaotangaza nia kuanzia sasa wafikirie upya juu njia sahihi ya kujitambulisha. Wasijiwekee akiba ya msongo pale watakapojikuta safari yao haikuvuka hata mzingiti wa mlango! Nadhani wengi hawako sahihi pale wanapojitangaza kama vile tayari wana tiketi za kuwakilisha vyama vyao. Badala ya kusema "Nitagombea Ubunge XXX 2015 kwa tiketi ya YYY" Labda watakuwa sahihi zaidi wakisema "Nitaomba ridhaa ya chama YYY kugombe Ubunge wa Jimbo XXX mwaka 2015". Ukilijua hili na kuliweka akilini, itakusaidia pia kujua kwamba vita yako haianzii hatua ya pili bali hatua ya kwanza. Itakupa fursa ya kujijenga mapema na kuweka mkakati wa kushinda kwanza hatua ya awali.

Vinginevyo nawatakia maandalizi mema.
 
Mi nshatangaza nia muhimu sana ni kupita kwenye kura za mchujo ndani ya chadema,nkipitishwa na chama bas kyerwa itakuwa na mbunge wa chadema maana mikakati ya ushindi nshaanza kuiweka,na naendelea.Nkipata ubunge bas kyerwa watakuwa wameramba dume.Hata ivo nisipopitishwa ndan ya chama,ntamuunga mkono mgombea wetu kwa nguvu zote.Kwahiyo,watu wa businde mjiandae kumpigia debe kijana wenu ili aweze kuhamasisha maendeleo ktk jimbo letu.
 
Hivi hili ndio jimbo alilokuwa akiliwakilisha ndugu BENEDICTO MUTUNGIREHI kati ya mwaka 2000-2005?

Huyo huyo Mtungirehi ndie alimwangusha Katagira then Katagira nae baadae akamwangusha kwa wizi wa kura.
 
Mze ISI yaonekana wewe wa ihanda?kuna sehemu inaitwa ihanda rabarogi, rwenjoju,kitwekyenkura nk. Jitaid umung'oe katag,ata blandes ni wa kuondoka. Wasliana na daud kahangwa ili akupe mkakati wa kuwaondoa
Hiyo Mitaa nimezungungikia sana enzi za ujana wangu hadi Nkwenda Kijiji kinaitwa Songambele nimefika.Kaisho, Kituntu,Bushangaro, Nyakaiga,Nyabiyonza, Kibondo,Kayungu,Nyakabanga,Nyakakika,Kandegesho Akitoma,Nyabweziga,hadi Matara Mpakani na Rwanda Mkuu wangu.Ngoja nikamtafute huyu jamaa yangu Mbunge Mdhurumiwa wa Karagwe Bw.Deusdedith Kahangwa Bw. Massawe alimdhurumu hivi hivi.Nilikuwepo kipindi yanatangazwa Police walitutawanya kwa Mabomu ya Machozi na Risasi za Moto.Ila 2015 hatutakubaliana na Magamba.
 
Una uhuru wa kugombea ila uwezo wako nina wasi wasi nao.
Kwa kuangalia tu ulivyoandika mtu anaweza kujua uwezo wako.
Mfano wewe kama mbunge mtarajiwa hujui kuandika lami.Unaandika rami. Makosa mengine waache wengine wachambue.
Pima uwezo kabla.
 
Una uhuru wa kugombea ila uwezo wako nina wasi wasi nao.Kwa kuangalia tu ulivyoandika mtu anaweza kujua uwezo wako.Mfano wewe kama mbunge mtarajiwa hujui kuandika lami.Unaandika rami. Makosa mengine waache wengine wachambue.Pima uwezo kabla.

Malamssha,

Asante sana kwa kupima uwezo wangu kwa typo ya rami badala ya lami. Hivi ni vitu vidogo ndugu yangu. Ila naomba ubofye katika hizo linki uone neno lami linavyosumbua wengi nami nikiwepo: Dk.Bilal:ahidi barabara ya rami Mtwara - . AU https://www.jamiiforums.com/habari-...ai-rami-yayeyuka-kama-barafu-print.html.Labda kama una jingine, naomba uniambie ukweli ndugu yangu ila usinidharau kiasi hicho....au kama nawe una mpango katika jimbo hilo hilo tuambizane...

Ninakushukuru na ubarikiwe sana!
 
bado hujatueleza unasukumwa na nini kugombea ubunge ukijibu swali hili tutakuunga mkonop
 
bado hujatueleza unasukumwa na nini kugombea ubunge ukijibu swali hili tutakuunga mkonop

Mliberali,

Asante sana kwa swali lako zuri. Ninasukumwa na haya yafuatayo:

1. Tulipata Uhuru katika kipindi kimoja na nchi za kusini mwa Asia ya mbali zikiwemo Malasia, Singapore, n.k, iweje leo leo nchi hizo ni middle income earners wakati sisi ni miongoni mwa nchi masikini sana duniani?
2. Huduma za jamii kama umeme, maji, afya, elimu bora, bima, n.k ni haba sana miongoni mwetu. Iweje ziwe ni kwa baadhi ya watanzania wachache tena viongozi na wafanyakazi wa serikali ngazi za juu na familia zao? Asilimia kubwa ya wananchi tulio wengi hatupati huduma hizi
3. Tazama CCM na mfumo wake, hivi kweli katika hali hii tutafika? Eti Bunge lisionyeshwe live kulikoni? Hivi unadhani Mhe. Makinda na Job Ndugai wanalitendea haki taifa hili?
4. Tunahitaji team ya vijana pale mjengoni Dodoma, hata ikibidi zipigwe kwa kutetea hoja zenye maslahi ya taifa....
5. Hivi Tanzania tuna mfumo wa Elimu kweli? Au ni uozo tu na uhuni na ujanja wawachache bora liende kwa CCM ilopo madarakani?
6. Ni mabilioni mangapi yako mikononi mwa wevi wachache huko Uswiss, n.k? Tunafanyaje hayo Mabilioni yarudi ili yawekezwe kwenye elimu, afya, maji n.k hapa nchini?

Mkuu ninayo mengi na wewe ninajua unayo mengi ila tukiunganisha nguvu bila unafiki TUNAWEZA! Japan in 1950s walikuwa kama tulivyo sasa ila waliamua na WAMEWEZA kulikoni sisi? Watanzania tuamue kuitoa CCM madarakani na hakika tutaweza!
 
siukawambie hao watakaokupigia kura? sisi hatuna msaada. wengi wetu ni wabonyeza pads za key boards
 
Iangalie tena hiyo idadi ya watu. Hakuna jimbo lenye watu 400,000. Halafu jiulize, iwapo hata idadi ya wakazi huijui, je, unaweza kujua shida zao?
 
Iangalie tena hiyo idadi ya watu. Hakuna jimbo lenye watu 400,000. Halafu jiulize, iwapo hata idadi ya wakazi huijui, je, unaweza kujua shida zao?

Kwani majimbo kama Kawe, Ubungo yana wakazi wangapi? Kyerwa yaweza kuwa na wakazi 400,000 kwa sasabu idadi ya wapiga kura waliosajiriwa ni zaidi ya 70,000 kwa takwimu za 2010. Tafuta ripoti ya sensa 2012 itakupa majibu pia.
 
Kwani majimbo kama Kawe, Ubungo yana wakazi wangapi? Kyerwa yaweza kuwa na wakazi 400,000 kwa sasabu idadi ya wapiga kura waliosajiriwa ni zaidi ya 70,000 kwa takwimu za 2010. Tafuta ripoti ya sensa 2012 itakupa majibu pia.

Yaweza kuwa au inayo? Mgombea anatakiwa kuwa na figure sahihi. Sensa imefanyika 2012, kwanini utumie takwimu za 2010?
 
Hongera sana kamanda kwa kuthubutu kuonyesha nia yako njema ya ukombozi lakini umekijengaje chama "chadema" huko unakotegemea kwenda kugombea kwa kiasi gani na sio kwenda kujaribu kama utashinda au la!
 
Back
Top Bottom