Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

Narudia Tena

Me : tar 20/8 jina J

Ke: tar 3/11 jina S

Tupo kwenye mahusiano
Mkuu ugomvi?

Anyway,
Mtizamo unaonyesha wewe na yeye ni watu wawili tofauti sana na hamuendani kwa nafasi kubwa kwa maana wewe ni moto wa mkaa na yeye ni maji ya moto wewe ni rahisi sana kumchemsha yeye na yeye akichemka ni rahisi sana kukuzima means kwenu mnaendana kwa asilimia 25 sikushauri kuwa nar na kama mahusiano yenu hayana u serious wowote jaribu kutafuta wa size yako haijalishi ni miaka mingapi ataficha makucha lakini ipo siku tu atayaonyesha na ndoa moja kwa moja huwa ni mkolezo wa moto wa nyota za watu na ni tendo la kukamilisha nusu ya dini au ibada kwa imani yoyote uliyonayo.

Haijarishi mtaelewana kwa muda gani any second moto huwa unawaka na kila mtu hutizamia nafsi yake na mara nyingi kwa nafasi kubwa kibri chako na ufalme wako au utawala ndio huwa unaleta shida kwa maana asili yako ni simba wa nyika ambaye hahitaji kuwa pinned down na yoyote sasa kwa yeye unakuwa umepamia kwa maana ni Mfalme wa vita na hakubali kushindwa no matter what uwe umemzidi umri,akili,maarifa,au pesa kitakachozidi kushikiria mahusiano yenu ni roho ya huruma na moyo wa imani ulionao.
Yawezekana ukawa na huruma kwa machozi anayokuonyesha na lawama anazotoa lakini nyuma ya shilingi huyu ni nge no matter how utacheza nae atakung'ata tu.

Kukusaliti kwake ni jambo la kawaida na halionei tabu na anaweza kukuumiza roho kwa nafasi kubwa bila kujali na ukitaka kuhoji atakwambia I'm being honest au mimi naongea kwa uwazi na siwezi kuficha nakwambia yaishe lakini katika moyo wake ni kwamba anakwambia ili siku nyingine tena na tena aje akwambie.

Mwenye uwezo wa kuishi na huyu mwenye asili ya maji ya moto ni mtu aliyeshika sana imani ya dini na Bushoke.
na kwa wewe moto wa nyasi dini ni sawa unaweza kuwa nayo lakini kuwa bushoke wenye moto wa mkaa katika milioni 10 labda mmoja.

MTIZAMO WA PILI:
Katika maswala ya ngono na chumbani hakuna mtu kama wewe atakuona ni mtu mwenye kumridhisha sana na hata anaweza kukwambia katika wazinifu wote niliozini nao hakuna kama wewe you are the best unanipatika
Lakini taratibu utaanza kujikuta katika wakati mgumu wa kuendana na tabia zake za wivu kupindukia na kutaka kutawala mahusiano yenu yaani atakutega kila kitu anakusikiliza wewe lakini kiuhalisia utaona bila kujificha kuwa anataka akupande kichwani na usiwe na lakusema ukiwa unaongea nae utaona anakukatisha na kutaka yeye ndio akueleweshe kitu
Ukali na hasira za karibu ni tabia na asili yake no matter how mbele za watu atajionyesha mpole lakini huyu ni short fuse kwako time yoyote bomu inalipuka.
Wakati wewe ni moto mkali zaidi kuliko yeye ni ukali wako ni sawa na gas inayosubiri kiberiti tu ili iweze kulipuka any second akileta udambwi dambwi unaweza kulipuka vibaya na kama unashetani basi hapo hapo hupanda 🙂
Pia fikra yako ni moja kwa moja utakuwa unamtizama kama kichwa ngumu na mwenye hasira.
Hali ya kuwa wewe anakuchukulia kama mwongo na hupenda kujionyesha.
Hawezi kukuelewa tabia yako ya kupenda kuzungukwa na watu na ataendelea kukudhania kuwa ni mtu mwenye kupenda kujionyesha.
Yeye ni mtu wa kupenda kutawala kuliko kujionyesha na wewe ni mwenye kupenda kujionyesha (kujisifu) na kutawala hata kufaa huyu.
Ingawa kwa ngono mtafurahiana lakini Sex isn’t everything.

Rakims
 
Rakims

mimi wangu kazilwa 14/8
mimi nimezaliwa 14/3

majina lake linaanza na V
jina langu linaanza na S.




hembu chambuaaaaaa
Kifupi hamuendani na hamna maelezo marefu kwenye nyie ni moja kati ya couple iliyokosea njia au pa kwenda no matter how she is wewe kwake ni sawa na moto wa mkaa ukautupe kisimani utegemee uendelee kuwaka tafuta mwingine maana mtazamo unaonyesha wewe ni mkali,mwenye kutawala;
Yeye ni mtu asiyependa kutawaliwa na ni wa mambo ya miujiza au kichawi(Mshika dawa)
Mtajikuta ni wenye kufanyiana fitina kwa sababu mpo tofauti sana hapo ni sawa na kama sio wewe mwenye mambo ya waganga na vidawa dawa vya kuroga mapenzi basi ni yeye huna tofauti na mtu aliyeoa mchawi halafu hamjui ni level imejaa mauza uza ikikutana na wewe uongo mwingi na imani nyingi ana pande mbili za shiringi kama sio mshirikina basi ni mtibu ushirikina imani yake imebase katika mambo ya kichawi au kiroho kama sio black magic basi ni white.
Japokuwa kasoro au tofauti zenu wewe hazikuumizi kichwa lakini tabia zako na zake haziendani kabisa endelea kuwa nae utajua nazungumzia nini,
Kupenda kwako kutoka na kuenjoy maisha na kujifunza dunia inasema nini kwake yeye ni vitu vya ajabu na yeye ni mtu wa kujificha ndani au msiri msiri mambo yake sasa wewe tabia yako ya kujionyesha kwake sio na wewe unamove fast while she is slow,
Nyote mnatabia ya kuchukua zaidi ya kurejesha kitu ambacho kwenye mapenzi huwa ni nipe nikupe sasa wote mkiwa ni nipe cha kupewa kitakosekana.
Usiri wake ni kitu ambacho hutaweza kuvumilia.
Muda hautakuwa mrefu wewe utaanza kusaka nje.

Rakims
 
NIMEISHIA KWAKO MKUU NITARUDI KUENDELEA.......................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mwanamke : tarehe 20/11 jina linaanza na S

Mwanaume : tarehe 20/11 jina linaanza na J

Tupo kwenye mahusiano kuelekea uchumba
 
NIMEISHIA KWAKO MKUU NITARUDI KUENDELEA.......................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mwanamke : tarehe 20/11 jina linaanza na S

Mwanaume : tarehe 20/8 jina linaanza na J

Tupo kwenye mahusiano kuelekea uchumba
 
Mwanamke : tarehe 20/11 jina linaanza na S

Mwanaume : tarehe 20/8 jina linaanza na J

Tupo kwenye mahusiano kuelekea uchumba
 
mkuu Rakims naomba usiniruke please Mimi ni Mwanaume sijaoa
mimi me: heruf J tarh 10/january
mpenz ke:heruf A tarh 29/july.
mahusiano yetu ni wapenzi na pia vp atanifaa kumuoa na vp hisia zake kwangu
 
ahsante mkuu
 
sijakupa maelezo ya kutosha au hatuna maelewano ya kutosha.

ila umesema vizuri . Rakims
 
NIMEISHIA KWAKO MKUU NITARUDI KUENDELEA.......................!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Mkuu naomba usiniruke

Mimi mwanaume kuzaliwa 17/05 jina ( I )
Mwanamke wangu kazaliwa 21/05 jina ( H )

Uhusiano ni mpenzi tu bado uchumba haujawa rasmi..

Mkuu Rakims naomba unichambulie kwenye nyanja zote muhim tafadhari..
 
Mtu wa kwanza kbs kumpost
Mmoja ana nyota ya maji mwingine udongo ila umesema watakua na mifarakano..
Nyota zipo 12 katika nyota hizo kumi na mbili kuna makundi manne ya nyota yanayoziunganisha ukiona nyota kundi moja mfano nyota za maji sio zote ni maji aina moja kuna maji aina tatu ambayo ni Kaa,Nge na samaki zote ni maji na pia sio zote ni maji ya namna moja hapo kuna maji ya bahari,maji ya kisima na maji ya moto hivyo ni vitu vitatu tofauti sio watu wote wenye nyota za udongo wataendana na nyota hizi za maji mfano mchanga mweupe wa baharini huwezi kuupata kwenye maji ya moto maji ya moto utayapata kwenye chuma au chombo cha moto ndio huyabeba na maji ya bahari mwenzie ni mchanga wa bahari mkuu usisome kitabu kimoja au viwili na google kisha ukaweka hoja nzuri kwenye thread ya jambo usilojua ni bora ungeuliza kuliko kuhukumu.

Ungesema kwa ninavyoelewa mimi ni kwamba hao wanaendana kisha ungeeleweshwa sio kufanya ujuaji sehemu ambayo hujui ndani zaidi ndio maaa napenda kutumia jukwaa la intelligence maana pale watu hujibu kwa nguvu ya hoja na fact za kutosha huku mpo shalo sana kwenye Quotes.

Rakims
 
mkuu
Ikiwa unahitaji maelekezo ya ziada mkuu ongeza details na weka hoja ndugu yangu.
mkuu Rakims umeniruka post namba 386 ujanichambulia details mimi mwanaume sijaoa
mimi me:tareh 10/1 herufi J
mpenz ke:tareh 29/7 heruf A
uhusiano ni wapenzi
nahitaji kumuoa je imekaaje na vp hisia zake kwangu na yote kumuhusu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…