Nitajie viongizi watatu tu wa Upinzani waliopigana vita ya Kagera kwa namna yoyote ile ukimuondoa mzee Mrema!

Kwenda tu vitani hizo ni akili za kiccm ccm
Upinzani ungekuwa unatawala kusingekuwa na vita ya Uganda
 
Hussein Mwinyi rais wa Zanzibar alikacha kwenda JKT kwa mujibu wa sheria.
Kwa hiyo na yeye sio mzalendo?.
 
Ni viongozi wangapi wa CCM waliopiga hiyo vita? anza na CCM kwanza
 
Tungekutajia tatizo umeshawaondoa.Hata CCM ukiondoa wale waliopigana Vita ya Kagera sidhani Kama utapata waliopigana Vita ya Kagera
 

Ndege john umekula maharage ya wapi.
Kupingana sio moja ya ticket za uzalendo,
 

Mungu uwalaani wasiotenda haki
 
ohoo ohooo nyie ma CCM tena msijaribu kabisa kuchoza vita nyingine, for sure nyie ndiyo mtakua wa kwanza kukimbia na kuiacha nchi ikichakazwa, mwishoni sisi vijana ( nadhan mnaelewa vijana tuko chama lipi) ndiyo tutakao iokoa nchi kama ilivyo kuwa 1978 -1979...
 
Vita ya kujitakia...Amin alimpindua Obote rafiki wa Nyerere...akafichwa Oyster bay...Nyerere akakataa kumtambua Amin kama raisi wa Uganda...Chokochoko vita ikaanza...Tulikuwa na uchumi bora sana 70s sawa na nchi nyingi za Asia...vita ikaharibu kila kitu
 
Acha kufikiri kufupi. Mtu yeyote aliekuwa mtu mzima wa kupigana vita vya Kagera wakati huo kwa sasa ni mzee sana au alishakufa.

Uliza Tulia kazaliwa mwaka gani na vita vya Kagera vilikuwa mwaka gani, labda utapata akili angalau ya kuweka post JF
 
Ameandika thread ya kipumbavu sana, nashangaa imepata comments nyingi hivi. Shule kweli mali.
 
Mambo mengine Ujinga tu, hivi unataka Mnyika aliyezaliwa 1980s awe na historia ya kupigana Vita vya Kagera?
 
Ama kweli Tanzania wamejaa mambumbu kama wewe.
 
Maalim, Safari, Rungwe, Mtei nk?
Maalim na Rungwe- walikuwa mwanaCCM kindakindaki
Mtei - alikuwa Waziri wa Fedha

Ingawa mtoa post anaonyesha Kama Ni kigezo Cha Uzalendo Basi miaka yetu sie hakuna wazalendo tena sijui tusubirie vita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…