Mimi ni Simba SC damu ila sijazoea Unafiki, Ujinga na Upumbavu na nitakuwa wa mwisho pia Kuuamini. CAF kubadili Waamuzi wa mchezo Kwangu Mimi si hoja kwamba Simba SC tunahujumiwa na nimeshtushwa pia kumuona Mwanasimba mmoja ambaye pia ni Mbunge na Mwanasiasa nae bila haya / aibu akiingia katika Upuuzi.
Hivi ni mara ngapi hapa hapa katika Ligi Kuu yetu Simba SC huwa tunabadilishiwa Waamuzi? Je Timu pinzani huwa zinatulalamikia kwa TFF? Kama tunadai kuwa hatua hii ya CAF ni ya Kuihujumu Simba SC yetu Sisi Simba SC tulishindwa nini nasi Kuwahujumu vilivyo ile majuzi?
Hivi TP Mazembe ndiyo waliifanya Miguu ya Nahodha Wetu John Boko ilione lango lipo juu akapaisha kule badala ya Kulilenga vyema? Hivi Simba SC nani alitufanya tushindwe kuzitumia zile ' clear chances ' tulizozipata matokea yake Wachezaji wetu wakawa wanarukaruka tu kama Maharage ya Mbeya?
Simba SC msitake kuwafanya Watanzania hasa Mashabiki wetu ( GENTAMCINE nikiwemo ) kwamba ni Wajinga au Wapumbavu au labda wengine hatujawahi Kucheza mpira au hatujui Kuuchambua vile vile. Hivi kuna nani hajui kuwa Simba SC hata kama hao Waamuzi wasingebadilishwa hivi bado Kuwafunga TP Mazembe Kwao Lubumbashi ilikuwa ni ngumu?
Hivi mmejua kuwa kwa Kitendo chenu hiki cha Kulalamikia Mabadiliko haya ya Waamuzi tayari Kiufundi mmeshawaharibu Wachezaji wetu Kisaikolojia? Mimi naamini kuwa kama Simba SC ikijipanga vyema kabisa pamoja na CAF kubadili hao Waamuzi bado tunaweza Kuwafunga TP Mazembe huko huko Kwao.
Uwezo wa Wachezaji wa Simba SC hasa hawa tulionao siyo wa Kushindana na Vilabu vikubwa na hata hii kufikia tu hapa ni Bahati tu ya Mwenyezi Mungu hivyo tusitake kujifanya kama vile Sisi ni Timu bora na ina Mapafu ya Kushindana na hawa Majabali wakubwa wa Kimpira Afrika.
Mkiambiwa kuwa tumieni vizuri Uwanja wenu wa Nyumbani muwe mnaelewa na nadhani mmewaona Mamelodi Sundowns walichowafanya Al Ahly hadi wakawafunga zile Goli Tano kwa Nunge ( 5 - 0 ) wakati Sisi huku Kipaumbele chetu Kikuu kikiwa ni Kuujaza tu Uwanja na kuwa na Tiketi za ' Platinums ' za Kutosha.
Najua wana Simba SC wengi kwa Uzi huu leo mtanichukia GENTAMYCINE ila huwa silei Ujinga na Upumbavu na Unafiki Kwangu ni mwiko bali nitakuwa nanyoosha tu pale ambapo naona panabidi kufanywa hivyo. Ushauri pekee ambao nautoa ni kwamba nawaomba Wachezaji wazawa wa Simba SC kama Mdogo wangu Mkude akina Ndemla, Tshabalaa, Dilunga na Muzamiri wautumie huu mchezo kama sehemu yao ya Kujiuza ili ikiwezekana basi TP Mazembe au Vilabu vingine vikubwa viwamulike na kuwasajili ili Tanzania iongeze idadi ya Wachezaji wake wanaocheza nje.
Ni Mpumbavu tu pekee na asiyejua Mpira vyema ndiyo alikuwa anajua na kujiaminisha kabisa kuwa eti Simba SC ina ubavu / uwezo wa Kumfunga TP Mazembe Kwao ' Machinjioni ' huko Lubumbashi. Twendeni tu tukapokee Magoli yetu ya Kutosha ili yatutie Ndimu / Hasira na tukirudi sasa Hasira zetu zote tuzihamishie katika Mechi zetu za Viporo na zile za muendelezo wa Ligi Kuu ili tulichukue tena hili Kombe kisha Mohammed Dewji na Kamati ya Usajili ya Simba SC bila kusahau benchi la Ufundi likae chini na lifanye Usajili ' Kabambe ' kwa ajili ya Michuano ijayo ya CAF Champions League ambayo GENTAMYCINE naamini kuwa kama Simba SC itashiriki tena na Kusajili ' Majembe ' ya maana basi kwa Msimu ujao tunaweza hata kufika Fainali na kwa Kudra zake Mwenyezi Mungu hata Kuchukua Kombe.
Tuacheni kutafuta Visingizio vya Kipuuzi vya Kulalamika Waamuzi Kubadilishwa. Na hapa nimewadharau Kidogo Viongozi wangu mtanisamehe sana katika hili. Cha kufanya tu sasa badala ya Kulalamika kubalishiwa hao Waamuzi nadhani tutumie tu muda huu Kuwaandaa na Kuwajenga vyema Kisaikolojia Wachezaji wetu kuwa wakiona Magoli yanaingia mfululizo kwa Golikipa Aishi Manula wasiwe wanashangaa bali wajue tu ya kwamba hao ndiyo TP Mazembe na hapo ni ' Machinjioni ' Lubumbashi.
Nawasilisha.