Pre GE2025 Nitashiriki kuzuia maandamano ya CHADEMA Januari 24, 2024

Pre GE2025 Nitashiriki kuzuia maandamano ya CHADEMA Januari 24, 2024

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mimi nilikuwa sijui hata kama kuna maandamano labda kama yangezuiwa
Tanzania ni kimbilio la wakimbizi wanaokimbia hali mbaya huko kwao. chadema wamepoteza imani ya watu hasa baada ya tunaowachagua na kuwashabikia kurudi CCM kuunga juhudi (money mongers). Lema watoto wake wote na mkewe wako canada, anatudanganya sisi tusiokuwa na kwakwenda. Huwezi kuwadanganya watu wote kwa wakati mmoja mara zote. Wanafanya biashara ya siasi kutafuta maisha kwa kutumia mazuzu tangu enzi zile za akina Mrema, Lamwai, marando, Mtei, Slaa, Sumaye, Lowassa, Mkumbo, Tumbili, nasari, nk. wanatajirika kupitia migongo ya mazuzu. Akina Sugu, Msigwa, Mboye na wengine wamenufaika sana kupitia walalahoi wanaosukuma magari yao, kuwapigia kura, kuhesabu kura na kulinda kura zao. Taifa linaingia hasara kugharimia chaguzi za wanachadema walioacha ubunge na udiwani na kurudi ccm.
 
Maandamano hayasaidii, yanazidi kumpa sifa Mama kimataifa katika duru za demokrasia, kwakuwa inafahamika wazi dunia nzima kuwa:
1. mama amepokea kijitti kutoka kwa mtangulizi ambae alikuwa "dikteta" wa demokrasia. Sasa kuna nafuu kubwa kuliko huko nyuma.
2. Ughali wa maisha uko dunia nzima, ikiwemo Marekani.
3. Nchi imetulia, amani imetamalaki, hakuna hata sisiminzi anaepoteza uhai wake kwasababu ya siasa.
4. Vita vya Ukraine, Gaza, DRC, Sudan, Somalia, Ethiopia, Afrika ya kati na kule Niger, Burkina faso na Mali vinafuta malalamiko yote ya tz kuonekana kuna tatizo.
5. Inafahamika kuwa vyama vya upinzani vimejaa wahuni; waunga juhudi za chama tawala, walafi na money mongers. yaani wanatumia wananchi kisiasa kujipatia mahekalu, mahoteli, mashamba, magari makubwa na kusomesha watoto wao ng'ambo. Hapa tunazungumzia vyama vya upinzani kuwa na watu kama akina nassari, tumbili, akina Mdee, sugu, lema, sumaye, Slaa, Lipumba; Lowasa, Mrema, na Membe (RIP) na wengine wengi ambao wapenda mageuzi waliwaamini na kuwapa kura zao lakini hatimaye wakarudi na kwenda CCM na wengine kujenga vitega uchumi vyao binafsi badala ya kuimarisha vyama vya upinzani nchini.

6. Hawana hoja za msingi na zinazoeleweka za kulisogeza taifa mbele, ni watu wa matukio tu.
7, Waapinzani walihusika na kuvuruga mchakato wa kupata katiba mpya yenye afadhali kuliko iliyopo kwa kung'ang'ana na aina ya muungano kwenye katiba.

Wapinzani wanayo kazi kubwa ya kufanya kurejesha upinzani pahala pake. Mimi binafsi sijui nani kama nikimchangua hataenda CCM kuunga juhudi za mwenyekiti. Ni heri wananchi wote twende bure wenyewe tukaunge juhudi za Rais kuliko kumchangua mtu ambae atakwenda kuunga juhudi za rais kwa kupewa pesa nyingi.
 
Back
Top Bottom