Nilijitambua kuwa mimi ni SIMBA mwaka 1982, almost miaka 41 hivi iliyopita.. Ni shabiki kindakindaki wa SIMBA sports club. Mimi si shabiki maandazi.
SIMBA ni timu kubwa sana Tanzania, Afrika na duniani kote.. Simba imekuwa role model kwa timu nyingi kwa mengi mazuri iliyoyafanya. Ina mafanikio mengi kitaifa na kimataifa. Inaheshimika na kutambulika sana kuliko hata mpinzani wetu.. Ni mojawapo ya timu maarufu popote uendapo.
Kwa sifa zote hizo
Kwa mafanikio yote hayo
Kwa ukongwe wote huo
Kwa umaarufu wote huo.. Nitaanzaje kuichukia timu yangu hii kwa changamoto ndogo ndogo za kupita?
Kwenye maisha kuna kupata na kuna kukosa
Kuna nyakati za mafanikio na kuna nyakati za maanguko
Kuna nyakati za furaha na kuna nyakati za huzuni pia
SIMBA tunapitia kipindi kigumu lakini si kama maadui zetu wanavyoaminisha watu mitandaoni.. Ni changamoto za muda hazitakuwepo milele.. Ni nyakati za nzige.. Tunazitafakari...hatukati tamaa tunapambana tutazishinda na kuwa imara zaidi.. Washindi zaidi wakubwa zaidi na zaidi
Soka lina matokeo matatu
Kushinda
Kushindwa
Kutoa suluhu
Kwasasa sisi ni washindwa wa muda. Tunaachia nafasi za furaha kwa wengine wanaokua. Ni muhimu kufanya hivi pia.. Huwezi kuwa mshindi daima. Maisha yana pande mbili nasi kwasasa tuko upande wa pili.
Acha kwasasa adui afurahi lakini hili nalo litapita kama mengine yote yalivyopita.
Viva SIMBA.... Viva Forever.[emoji173]
View attachment 2525426