Niulize chochote kuhusu Wilaya ya Sikonge Tabora

Niulize chochote kuhusu Wilaya ya Sikonge Tabora

Lukula na Kipanga ni vijiji vya zamani
Vipi maembe mwakaka huu yapo mengi? Enzi za utoto tukikuwa tunayafata Lukula na Kipanga,Tena tulikuwa tunatoka kwetu Usunga one tunayabeba kichwani,Ni mazito balaa.
 
Ngoja anaesumbua anajulikana kwa jina la Koboko (Cobra) ambao kwa maeneo ya wilaya ya Sikonge hupendela kuishi katika mashimo ya visuguu au katika mapango ya miti

Jwani cobra ndiye koboko! Na black mamba utamwitaje kwa kiswahili!
 
Mashamba ni mengi sana na uzuri siku hizi tumbaku inalimwa katika kijiji chochote tofauti na zamani ambayo ilikuwa inalimwa katika vijiji maalumu.
Ila sikushauri ulime Tumbaku
Kwanini haunishauri nilime tumbaku Mkuu?, au ni kilimo kigumu sana nini Mkuu?, Tujuzane.
 
Wilaya ya Sikonge ipo Kusini ya Mkoa wa Tabora, Wilaya hii inapakana na Wilaya ya Uyui Kaskazini na upande wa Mashariki inapatikana na Mkoa wa Singida.

Kusini inapakana na Mkoa wa Mbeya Kusini Magharibi inapatikana na Mkoa wa Katavi na upande wa Magharibi inapatikana na Wilaya ya Urambo.

Wenyeji wa Wilaya hii ni wanyamwezi huku shughuli zao zikiwa ni kilimo ufugaji na uwindaji.

Mazao yao makuu yakiwa ni Mahindi, Maharagwe, Karanga, Mhogo na Mpunga. Huku zao kubwa la biashara likiwa ni Tumbaku.

Wilaya hii inajishughulisha pia katika ufugaji wa nyuki na inasemekana kuwa asali ya Tabora ndiyo asali iliyobora kuliko maeneo mengine yote katika nchi yetu.
Inavituo shikizi vingapi au satellite skul ngapi?
 
Wilaya ya Sikonge ipo Kusini ya Mkoa wa Tabora, Wilaya hii inapakana na Wilaya ya Uyui Kaskazini na upande wa Mashariki inapatikana na Mkoa wa Singida.

Kusini inapakana na Mkoa wa Mbeya Kusini Magharibi inapatikana na Mkoa wa Katavi na upande wa Magharibi inapatikana na Wilaya ya Urambo.

Wenyeji wa Wilaya hii ni wanyamwezi huku shughuli zao zikiwa ni kilimo ufugaji na uwindaji.

Mazao yao makuu yakiwa ni Mahindi, Maharagwe, Karanga, Mhogo na Mpunga. Huku zao kubwa la biashara likiwa ni Tumbaku.

Wilaya hii inajishughulisha pia katika ufugaji wa nyuki na inasemekana kuwa asali ya Tabora ndiyo asali iliyobora kuliko maeneo mengine yote katika nchi yetu.
Kumbe Sikonge ni wilaya, mimi nilijua kijiji.
 
Waarabu wapo maeneo hayo ya Sikonge na Tutuo ila waarabu wanatabia ya kuoana wenyewe mtoto baba mkubwa na mtoto wa baba mdogo mtoto wa mama mdogo na mtoto mama mkubwa

Hakuna shida hapo, mbona hakuna mtu ambaye yupo hapa duniani ambaye hakuoa ndugu yake! Soma Biblia au Q’uruan ujue kuhusu Adam na Eva/ Hawa!
 
Tumbaku ni zao gumu sana ambalo unawajibika takribani mwaka mzima pia zao ambalo linaharibu manzingira sana
Kwanini haunishauri nilime tumbaku Mkuu?, au ni kilimo kigumu sana nini Mkuu?, Tujuzane.
 
Back
Top Bottom