Futar ya boga inapikwaje?
Hakuna futari nayoipenda kama hii ila zikiwa na maharagwe pembeni, ila kwenye mapishi ndio yalikuwa yananishinda, hongera kwako.Mahitaji
Tambi (spaghetti 1/2 ya packet)Mafuta (vegetable oil)Sukari (sugar 1/2 kikombe cha chai)Hiliki (cardamon 1/2 kijiko cha chai)Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)Tui la nazi (coconut oil 1 kikombe cha chai)Maji kiasi
Matayarisho
Tia mafuta kiasi kwenye sufuria kisha ibandike jikoni (katika moto wa wastani) yakisha pata moto kiasi tia tambi na uanze kuzikaanga kwa kuzigeuzageuza kila mara mpaka zitakapokuwa za yangi ya light brown. baada ya hapo ipua na umwage mafuta ya kwenye tambi (bakiza kidogo sana kwani usipofanya hivyo tambi zitakuwa na mafuta sana) Baada ya hapo zirudishe jikoni na kisha utie hiliki, chumvi, sukari, tui la nazi na maji kiasi. Zifunike kisha ziache zichemke mpaka maji yakauke. Baada ya hapo zigeuze na uzipike mpaka ziive. Nahapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Futar ya boga inapikwaje?
Zote zinaitwa Tambi tu bana. Acha kukomplicate mamboMy dear, tambi hizi zinaitwa pasta.
Spaghetti ni zile ndefu kama vijiti na mara nyingi zinapikwa za chumvi na mchuzi kama macaroni.
Zote zinaitwa Tambi tu bana. Acha kukomplicate mambo
Natamani sana kupika ili biriani, ila nimekutana na vitu humu ndani hata sijawahi visikia sehemu, hiyo giligilani ndio kitu gani?Mahitaji
1 kilo mchele wa basmati
1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.
1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)
1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana
1/2 lita ya mafuta ya kupikia
1/2 kilo ya samli au mafuta yeyote ya kupikia
2 maggi chicken soup cubes
3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu
1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari
3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (giligilani)
2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa
korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima robo kikombe
majani ya girigilani kichanga kimoja
mbegu za nzima ya hiriki kiasi
Pili pili manga nzima kiasi
Chumvi kiasi
Jinsi ya kuanda
Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)
Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.
Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.
Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.
Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, korosho funika kwa dakika 10 i, kisha weka mchele wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto
Kwa darasa hili Kachori naweza kupika bila wasi wowote ule, kwasababu Mama alikuwa anapika KATLESI akawa ananielekeza kwa vitendo.Mahitaji:
Viazi ,Kitunguu saumu(galic) na Tangawizi iliosagwa,Chumvi,Pilipili ya kusaga kutegemea na unavyoipenda,Ndimu,Mafuta ya kupikia,Unga wa dengu au Ngano Kiasi.
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Chemsha viazi mpaka viiive, kisha vitoe maganda na uviweka ndani ya bakuli.
2. Vipondeponde kwa mkono mpaka viwe laini(viponde kabla ya kupoa)
3. Saga vitunguu saumu na tangawizi kisha changanya na viazi .
4. Weka chumvi, ndimu na pilipili ya unga kisha uonje, unaweza kuongeza viungo hivi kwa kadri ya mapenzi yako.
5. Tengeneza madonge ya duara uyapange katika tray.
6. Vuruga unga wa dengu au ngano kwa maji uwe mwepesi kidogo.
7. Weka mafuta ya kupikia ndani ya karai na uliweke kwenye moto.
8. Chovya madonge kwenye unga na uyatose kwenye mafuta ya moto. (Uchomaji wake ni kama kuchoma bajia)
9. Wacha kachori zibadilike rangi kuwa ya njano na uzitoe kwenye mafuta.
10. Weka Kachori kwenye sahani zipoe tayari kwa kuliwa na chatne na juice au chai.
Almost sawa tofauti ni mahitaji (ingedients)Kwa darasa hili Kachori naweza kupika bila wasi wowote ule, kwasababu Mama alikuwa anapika KATLESI akawa ananielekeza kwa vitendo.
Maandalizi yake, na mapishi yake yanafanana kwa kiasi fulani, tofauti KATLESI madonge yake unachovya kwenye Mayai badala ya Unga
Kata boga menya kisha lipange sufuriani. Kuna na uchuje matui 2 ya nazi la kwanza zito na la pili jepesi lile jepesi weka kwenye boga na chumviFutar ya boga inapikwaje?