Niulize kuhusu mapishi ya futari mbalimbali

Niulize kuhusu mapishi ya futari mbalimbali

MAHITAJI

*Boga 1
*Tui La Nazi 2 Vikombe
*Sukari 1 kikombe
*Hiliki 1/2 kijiko cha chai



UTAYARISHAJI NA UPIKAJI:

1.Unamenya maboga kiasi ukipendacho.

2.Unayakata kata vipande vidogo vidogo.

3.Unayachemsha na tui la pili mpaka yawive lakini yasije kuvurugika.

4.Maji yakishaanza kukauka unatia sukari kiasi ukipendacho na hiliki.

5.Kisha unamimina tui la nazi.

6.Unaiwacha ichemkie na kabla kukauka tui unaepuwa na tayari kuliwa.
Tamu sana☺️
 
Back
Top Bottom