Niulize swali lolote kuhusu Geology na field zote zinazohusuhiana na Jiolojia

inasemekana eti chini ya ardhi kuna mwamba mgumu ambao chini yake kuna bahari, hii ipoje mkuu? 2. Je ni majani gani yakiota ktk ardi huashiria eneo hlo kuna maji karibu,(unaweza chimba kisima)?
 
Kwa level ya certificate kwa kutumia cheti cha form four inawezekana
Hakuna certificate ya Geology, au Exploration and Mining Geology mkuu.
It means hiyo certificate ni lazima upite humu NTAL 4, NTAL 5, then NTAL 6 ambayo kwa pamoja huitwa Diploma.

Huwezi ukasoma NTAL 4 pekee na ukapewa certificate.
 
from Rock Mechanics knowledge, naomba unielekeze jinsi ya kusoma ratings za dip and strike of discontinuity orientations katika Rock Mass Rating (RMR)Table ya Bieniawski.......especially kweye part ya Tunnels
 
inasemekana eti chini ya ardhi kuna mwamba mgumu ambao chini yake kuna bahari, hii ipoje mkuu?

Mkuu structure au cross section ya dunia haioneshi uwepo wa kitu kama hicho. Kuanzia juu ya ardh mpaka kilometer kadhaa ni layer inaitwa continental crust. Na chini ya bahari ni layer inaitwa oceanic crust, hizi zote ni solid.

Ila kitokana na joto linavyoongezeka kuelekea katikat ya dunia. Kuna layer ya pili inaitwa mantle ambayo ni liquid/molten.

Kwahiyo hii solid layer inaelea juu ya hiyo layer ya pili ndo maana wanasema kuna bahari

 
2. Je ni majani gani yakiota ktk ardi huashiria eneo hlo kuna maji karibu,(unaweza chimba kisima)?


Katika elimu niliyoipata sijaona kitu kama hicho,

Na katika uzoefu wangu nimeona maji yanapatikana hata jangwani ambapo hakuna hata majani au yapo kidogo sana.

Mfano mzuri ni dodoma
Sehemu kubwa ya dodoma chini kuna maji (ground water table)

Unakuta juu kuna michongoma tu ila chini maji yanapatikana ya kutosha.

Kipindi nakua ndo ilikuwa source of water kabla ya hawa duwasa.
 
Hakuna certificate ya Geology, au Exploration and Mining Geology mkuu.
It means hiyo certificate ni lazima upite humu NTAL 4, NTAL 5, then NTAL 6 ambayo kwa pamoja huitwa Diploma.

Huwezi ukasoma NTAL 4 pekee na ukapewa certificate.
Hasante kwa kuchanganua.

Maana hizo njia me sijazipitia mkuu
 
inasemekana eti chini ya ardhi kuna mwamba mgumu ambao chini yake kuna bahari, hii ipoje mkuu? 2. Je ni majani gani yakiota ktk ardi huashiria eneo hlo kuna maji karibu,(unaweza chimba kisima)?
Labda iwe hivi, Ardini kuna mwamba kitaalam unaitwa aquifer huu mwamba kunasehemu ambayo unauwezo wa kupitisha maji labda kwa mf. yanayotokana na mvua, pili unauwezo wakushikilia maji hayo (underground water).

Hii bahari uisemayo wewe sio bahari kama bahari ilivyo bahari ya hindi/mediteranian, ila ni maji yalioshikiliwa katika huu mwamba, endapo kupata kisima giolojisti anatakiwa kufanya vipimo katika eneo husika ku locate huo mwamba na ukitobolewa ndio tunapata visima,

Kuna njia za kienyeji wanazozitumia watu hii niliionaga nyumbani kwetu, tuliweza kuchimba mita kadhaa tu hazizidi hata hamsini natukaweza kupata maji, maeneo ya kigamboni daraja la nyerere, hapo pia unawezaona ni jinsi gani mwamba una play part kubwa katika kuhakikisha maji yanakuepo katika quality na quantity nzuri,. LICHA ya
Eneo lenyewe kuwa mita kama 800/900 kutokea baharini ila maji yalikua ya baridi, yalifaa katika kazi zote za kinyumbani.

Kwa maelezo hayo unaweza kupata picha na kujijibu swali lako kuhusu hiyo bahari kama mnavoiita.. Nawe ukawasahihishe majirani na jamaa zako.

Asante.
 
from Rock Mechanics knowledge, naomba unielekeze jinsi ya kusoma ratings za dip and strike of discontinuity orientations katika Rock Mass Rating (RMR)Table ya Bieniawski.......especially kweye part ya Tunnels
Wataalam watapita mkuu[emoji6]
 
So sad msomi huwezi ku translate hii lugha yamzungu bhanaa
 
Wataalam watapita mkuu[emoji6]
Tunakaribisha mchango wako mkuu
Nimefurahi kuuona huu uzi mageo wenzangu
from Rock Mechanics knowledge, naomba unielekeze jinsi ya kusoma ratings za dip and strike of discontinuity orientations katika Rock Mass Rating (RMR)Table ya Bieniawski.......especially kweye part ya Tunnels

Huu UZI tungeomba kwa mode 4 au Reserved uwe sticky katika jukwaa hili.
Njia pekee ya kuifanya Tanzania ipige hatua katika maendeleo ni pamoja na vijana wanaotarajia kusoma masomo haya ya Jiolojia ya Madini na Mafuta kutambua kwamba sekta hii ni muhimu katika Taifa letu Kiuchumi hivyo kuwapa motisha vijana wengi wazawa waingie katika uwanja huu ili hapo baadae wafaidi rasilimali zao na si ma Expert toka nje ya nchi kuja kutafuna mapesa yanayotokana na sekta hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…