Niulize swali lolote kuhusu KUNENA KWA LUGHA nikufafanulie.

Ulipaswa useme huo uhusiano ukoje??
Je ndio lugha ya mungu kama ilivyo uislam na kiarab (quran)
Je mnenaji anaelewana yeye na mungu tuu??
 
Nabii gani au mtume wa Tanzania ambaye ni wa kweli unayemtambua?
 
Hiyo ni lugha ya roho mtakatifu, wanaelewa nae wanaoongea hiyo lugha.
Uongo mbona wao wenyewe wanaoongea hawaelewi nini wanaongea. Akiambiwa arudie alichokiongea ataweza? Hiyo sio lugha bana ni makelele
 
Nabii gani au mtume wa Tanzania ambaye ni wa kweli unayemtambua?
Tunapima roho kwa kutumia njia 2.
1.Kwa kumuuliza Mungu na Mungu kwa njia ya ROHO MTAKATIFU hutoa majibu
2. Kwa kupima uwiano wa neno na maisha au huduma ya mtu.
Kama una vitu hivyo viwili utawatambua tu.
Manabii wengi hapa Tanzania na kwingineko si wa kweli kwa kipimo cha neno.
Mfano
Nabii yeyote anayetoza pesa ili awatabirie au kuwawekea watu mikono huyo hajatumwa na MUNGU.
Yesu alisema mumepewa bure toeni bure
Sasa mtu akikutoza hata mia Tano kama gharama ya kumuona, kununua kifaa cha kiroho au kuonana naye huyo si nabii wa kweli.


Pia kipimo kingine ni matokeo ya unabii wao.
Mtu akisema jambo na lisitimie huyo hakutumwa na Mungu.

Njia ya tatu ni kutazama maisha ya huyo mtumishi anapokuwa nje ya kanisa.
Mtu ana kesi za kutia mimba wake za watu, kesi za kitapeli waumini.
Mtu ana ghorofa lakini hawezi kuishi hata na mtoto wa dada yake amsomeshe.
Mtu ana private jet, account ina bilioni 3 lakini anamwambia muumini alete elfu 10 ambariki apate mtaji au kazi badala ya kutoa yeye huo mtaji.
Matendo kama hayo ni ishara huyo nabii , mchungaji, Mtume, Mwinjilisti au mwalimu hana Mungu.
 
Kinachodaiwa kuwa ni kunena kwa lugha huwa ni upuuzi mtupu,

Imani ni shambulio la akili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…