Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimeishia kusoma Hadi kati ila wewe ni MPUMB.AVU na ni MSHAMBAHii ni mimi huyu Sonko sio mwingine,,
Short story huko nyuma nyuma hivi nikiwa kijana.
* * *
Miaka imeenda sana,,
Kwa jadi ya kabila letu wanaona nimepaa sana age halafu sieleweki.
Zingatia sieleweki yaani,
Hawasikii Sonko kuwa na demu,
wala zile kesi za ajabu ajabu.
Kifupi mtaani nimechill sana.
Sina urafiki na vijana,
Bali wazee ndio natumia time kubwa kukaa nao
Napenda kuwafuata wazee hasa nikiona yule anaependa kukaa peke yake.
Kuna vitu nafyonza kwao.
Lakini hawanishauri kuhusu mahusiano maana hawana uhakika kama upande nautazama sana.
Na mimi sioni kama kuna umuhimu kuulizia hizo mambo.
Lakini kumbe laiti ningejua ningebase huko pengine ningepata maarifa ya kutisha..
Kwenye simu za hapa na pale na maza,
Ni kelele tu za hivi utaoa lini huoni unazeeka?
Nazeeka vipi sasa wakati niko 23?
Presha ikazidi nikahisi bi mkubwa anaweza kuwa sawa mi ndio nikawa navurunda eti.
Nikaanza kufukuzia visichana hapa na pale,, kumbuka mi mgeni kwenye gemu sijawahi kuwamo kabisa.
So hata walipokuwa wakifanya flirtings zao sikuwa nikielewa lolote yaani.
Ugumu unakuja maana nawinda watoto ambao ni hotcake za mujini.
Tena muji wenyewe ndio huu huu niliokulia wa Daslama?
sio kweli, hapa ni full kuliwa nauli na salio,
Wale wanaoshoboka nawaona sio ndoto yangu.
Nataka nipate mtoto ambae nikimsimamisha na Nikki Minaji watoke droo.
Kitu sikujua ni kwamba nawinda kupata mke ndani ya makahaba,, na ukicheki nilivyokomaa utadhani nina status ya pull factor kumbe ni Ngoswe tu aliyezamia Daslam.
Likaja wazo la kiwaki,, sijui hata lilitoka wapi maana uvunguni hamna kitu na kusafi daily.
Nikampata binti mmoja wa Mbagala nikampa dili kuwa anizalie watoto wawili nampa m2. Akakubali akazidisha mawasiliano sasa.
Usiku kuanzia saa tatu hadi sa saba ni mwendo wa kuongea sasa mi ni introvert naona ananikera yaani akipiga simu nawaza nitaongea nae nn?
Kama ni maneno nahisi nishamaliza yote.
Magetoni nina mwamba wangu mmoja yeye anasoma St Joseph unvst.
Nikamshirikisha hili wazo maana ni mwanangu since wayback na tulishaapa kujenga nyumba zetu sehemu moja.
Mwana akaniambia homeboy, unafeli hivi hivi nakuona.
Mbona una presha kubwa hivi? Sijakuzoea hivi ujue..
Namuuliza why nafeli?
Ananijibu utapigwa.
Namuuliza how?
Ananiuliza je huyo binti akitaka umuoe utamuoa?
Namjibu siwezi kumuoa maana mkataba wetu hausemi nimuoe.
Tumekubaliana anizalie watoto tu then maisha mengine yaendelee.
Jamaa ananiuliza je ana mtoto kwanza?
Namuambia hajaniambia kama ana mtoto.
Ananiambia, muulize kwanza.
Napiga simu hapo hapo nakuuliza halafu kitu iko loud speaker.
Binti anatomboka vya kutosha.
Lastly hana mtoto.
Jamaa yangu ananiambia,, utapigwa halafu utaachiwa maumiv na watoto wako hutakuwa na access ya kuwa nao maaan wao ndio source ya mkataba.
Namuuliza how?
Anasema ushamuonyesha kuwa yeye humuhitaji bali watoto tu.
Unadhan kama yeye anakuhitaj atatumia njia gan kujimilikisha kwako?
Hapo sasa naanza kumpata vyema homeboy anachomaanisha.
Ananiambia kuwa mimba ni kweli atakubebea lakini hatokupa watoto maana wanawake huupenda sana uzao wao wa kwanza hata kama mtoto atatoka taahira niamini mimi kitinda mimba anaweza akanyimwa kitu akapewa kifungua mimba.
Nikamcheki homeboy kwa sekunde kadhaa huku nikijiwazia,, now this is a worth friend.
Hilo likapita Sonko nikabaki salama.
Lakini kumbe ibilisi alikuwa na mipango ya kuniweka spana sio poa
Jamaa akanishauri kwanini usimuoe fulani akifanya reference ya mabinti nilioskuli nao, nikampinga maana niliona viatu vile na safari yangu nitaburuza sana njiani sitafika.
Siku zikasonga nikiwa job nikakutana na kabinti kamoja raia ya singi, nyaturu moja Omufanga,, wajo fingijo fingijo.
Manzi nikamnoki ile sana but sijui kama nae alininoki sielewi si unajua moyo wa mtu kichaka.
Nikaanzisha nae mawasiliano tena kwa tahadhari ili nisijekumkera akasepa,,
Maana nishamunoki( mpenda) sana.
Ikapita like miezi miwili nikamtongoza kawaida tu nikamwambia nataka nimmiliki mazima, akatishia kunizimia fegi hata pafu sijapiga.
Nikaona nishawakosa kibao sana tena ambao nilitamani kuwa nao.
Kama anazima fegi sio dhambi pia sitakufa.
Mara time ilivyoenda akaniambia anataka kuja kupaona geto napokaa
Kwasababu nilikuwa na mwanangu geto sikutaka kuchanganya maisha kabisa nikamkatalia nikamwambia nina mwamb naish nae na ni mwanangu sana so sio picha nzuri.
akasema sawa.
Siku moja akaniambia nije au kila siku mmegandana magetoni tu?
Nikamwambia njoo leo mwana yuko chuo na kaniaga atakaa kwa manzi yake walau siku tatu.
Manzi akaja akakuta nimepika wali na kibua wa nazi za bahkresa.
Tukala tukakaa kupiga stori.
Nikaweka muvi tukawa tunaangalia tu kumbuka mimi sijawahi kusex na manzi yoyote so siichukulii kwa uzito huo uwepo wake geto kwamba anaweza akaniruhusu nimpige ukuni.
Manzi mara akanishika shingo akataka mate.
Na mimi nikampokea tukaanza romance hapo mlango wa geto uko wazi.
tunaanza kuzama kwenye feeling mara anakuja mjukuu wa mwenye nyumba kijana mdogo miaka like ten years anatukata stimu anaomba kitu fulan katumwa na bibi yake nampa then nalock kabisa mlango maana kaliingia hadi nditch kalishazoea kanakuja hata muvi tunaangalia na vitoto vingine
Vinakaaga kwenye kapeti unyoya.
Mikiki mikiki inaanza tena,, this time tunaenda hadi ndani ndani humo sipajui jina lakini nasikia kuna kumwaga.
But nagundua kumbe ngono kwa mara ya kwanza kwa mwanaume huwa haina ladha kabisa but as time goes ndio anaanza kuenjoy na kuitaka pengine zaidi ya msosi?
Aniambia tupige cha pili tena nawaza sasa kama ladha yenyewe hamna sasa narudia ili iweje anauchukua ukuni ambao kitendo cha kuuwekea mkono tu unakuwa mnara juu.
Anaukalia anafanya yake mi nampa kampani kiasi tu maana siko mchezoni kabisa.
Baada ya muda anaondoka anarudi alipotoka.
Ananiacha nikitafakari sasa inakuwaje watu hadi wanapiga makelele vile wakati hakuna cha ajabu?
Muda na shetani vinaniambia subiri tu we mwana usie na hatia utatufahamu tu tutakupa vingi bado hujajua.
Baada ya siku kadhaa anakuja tena tunafanya tena ila awamu hii mimi ndio naupata ule utamu na ladha so ninafanya na kufanya tena namuomba tena ananipa na kunipa tena nanogewa.
Mwanangu kesho yake anarudi na kuniambia kuwa ameshapata mwanae mmoja hivi pale pale chuo so anahamia pale ili kupunguza gharama za nauli
Naumia sana maana ni mwana ambae nimemzoea sana.
Nabaki mpweke. Napiga simu kwa manzi yangu namuunganisha waongee mshikaji anamuambia manzi yangu yeye anaenda mbali kidogo so siku akitukuta atamuona wala haina kabaya.
Manzi anapata taarifa rasmi kuwa nitakuw mwenyewe so ananiambia kama vipi aje tukae wote wakati wetu huu wa uchumba nasema sio mbaya.
Kesho yake baada ya mwamba wangu kuondoka manzi anakuja mida ya jioni na mabegi yake.
Anajimilikisha gheto la Sonko.
Anafanya makaratee kibao vitu ambavyo sikuwa navyo ananinunulisha
Hapo ndio naamini kweli nyumba ni mwanamke..
Mazungumzo baina ya yeye na maza yanashamiri muunganishaji nikiwa ni mimi hapo.
Linakuja seke seke jingine, wanawake hawatosheki yaani,, Mama anadai nimpeleke nikamtambulishe bush.
Manzi anasema hapana tuanzie kwao Singida kwanza.
Ninamwambia hapana tuanzie kwetu kwanza hapa dar Mshua akuone maana nimelelewa na mshua.
Then tukitoka kwa mshua twende kwao Singida mwisho tumalizie kwetu Tarime kwa Maza.
Maana wazazi wangu walitengana miaka kibao iliyopita kiasi nimekuwa dingi sikuwahi kumuona mpaka nimefika miaka tisa.
Then mvuum!! Mshua huyu hapa hataki maelezo kanipitia kama kipanga.
Tukaenda kwa mshua kisha nikaenda kwao.
Kwao sikwenda nae nilienda mwenyewe zingatia hapa kwenye kwenda mwenyewe bila yeye ndipo kiini na usumbufu wa hii stori ùlipo.
Nilienda mzee akanikabidhi mtu wake wa mkono tukaenda ukweni.
Na jamaa ndie aliniambia tusiende na binti kule kwao.
Huyu jamaa ni mwamba sana
Yaani ukimuona huwez kuidhania akili kubwa aliyonayo hata kidogo.
Baadae ndio nilielewa ni kwanini mshua alimteua huyu mtu.
na hapa ndipo niliacha kumunderate mshua.
Iko hivi
Jamaa aliniuliza ukiniangalia labda nina miaka mingapi?
Kwakuwa nilikuwa 23 na nikimuangalia jamaa namuona kama mchizi moksi fulani nikamuambia nakukadiria kwenye miaka 32.
Akakaa kimya kidogo kisha akaniambia nina miaka 48.
Nikashituka sana, amenizidi miaka 25? How?
Jamaa akaniuliza huko tunakoenda mke wetu yupo huko ?
Nikamwambia hapana.
Akauliza yuko wapi nikamuambia niko nae geto. Ila jibu hili nililitoa nikiwa sijiamini sana maana nilihisi labda jamaa ataona nishavuruga taratibu tayari.
Jamaa akakaa kimya kidogo akiwa ananitazama kiaina.
Kisha akaniuliza nani alikuambia umtunze gheto kwako ilihali hujamlipia mahali?
Nikamjibu amekuja mwenyewe na tunaishi hii sasa wiki ya nne.
Jamaa akasema vizuri hata kama angekuwa Singida ningekwambia umuite aje gheto kwako umuache gheto kwako then ndio sisi twende kwao Maadamu tayari yuko kwako basi haina shida.
Sikumuelewa maana yake mpaka tulipotoka huko ukweni,, nitaelezea huko mbeleni.
Safari ilianza na tulifika saa kumi na moja jioni tukapokelewa na wenyeji wetu..
Tulilala palipopambazuka taratibu zote zilifuatwa tukatozwa faini ya kimtindo maana tayari tulihesabika kama wezi kulingana na taratibu za huko Singida na jamii nyingi tu Afrika.
Basi tulitoa kishika uchumba,, lakini Jamaa akaniuliza uko vizuri? Nikamjibu ndio akaniuliza una bei gani nikamuonyeshea vidole viwili akaelewa akaomba udhuru tukatoka nje akaniambia lete bahasha nikatoa maana aliniambia mapema tukiwa Dar kuwa nihakikishe nakuwa na bahasha ndogo zisizopungua 30 basi nami nilikuwa nazo kwenye mifuko ya koti lote la suti yale makoti marefu maarufu kama Obama.
Nikatoa bahasha kumi kisha kila bahasha nikawekamo elfu kumi kumi kisha akaniambia chukua bahasha mbili wekamo elfu 30 kila moja ila zitenganishe na zile za elfu kumi kumi.
Nikafanya hivyo akaniambia zile mbili ni kwaajili ya wazazi tu zile nyingine ni kwaajili ya wajumbe wengine.
Tukarudi kikaoni kikao kikaendelea
Jamaa akasema kuwa ni ombi la kijana wangu kuja kwenu amalize kila kitu leo
Kisha akanipa ishara nianze kuchapa bahasha mezani. Nikachapa bahasha nikaona kila mtu anachungulia yake kivyake.
Wazazi nao wakachapwa za kwao ukimya ukatanda.
Kikao kikaendelea wazee wakatetema wakiulizana suala la mahari wakaomba tuwapishe ili wajadili mahari ya binti wao.
Tulivyotoka nje Jamaa akaniuliza binti ana mtoto? Nikamjibu ndio ameniambia juzi hapa na hakuwahi kuniambia siku zote.
Jamaa akaniambia hakuna shida sisi ni wakurya.
Akaniambia chukua bahasha moja weka laki tano tu kisha tulia shughuli nyingine niachie mimi.
Nikabaki nimeduwaa wakati mimi nilikuwa nawaza hata milioni mbili hivi?
NIkamuuliza kwanini? Haoni kama itakuwa ni kidogo sana?
Akaniuliza unadhani baba yako alikosea kunituma huku?
Ipo siku utaelewa baba yako ni nani we tulia tu nimekwambia shughuli yote niachie mimi. Nikikupa nafasi tu utaharibu na mzee wako aliniambia nisikupe nafasi utaharibu.
Kauli ile ilianza kunitoa kwenye reli ghafla.
Nikijiangalia nina pesa na mwisho wa mwezi uhakika utaniambia nini umri wenyewe wa kwenda klabu kwanza halafu mimi ndio sijui hata hizo starehe zaid ya kuipambania shilingi.
Jamaa alinituliza tuli kumbuka ni mkubwa sana anaweza kunizaa kabisa lakini tunabonga kihuni ile mbaya.
Tukarudi ndani wakatutajia mahari ambayo niliona ni wazi hapa tumekuja kudhalilika mimi na Mshenga wangu.
Nikabaki nina mshangao wa ndani japo mdomo haukufunguka lakini machoni tu ungeweza kuusoma mshangao wangu.
Yaani sio hata ile niliyokuwa naiwaza sembuse hii tuliyoweka kwenye bahasha?
Nikawatazama machoni wale watu kasoro mama mkwe.
Nikawaona wametulia wanatusubiri sisi tutoe jibu.
Nikamtazama mshenga wangu nae akawa ananitazama tu kama ananiuliza unasubiri nini?
NIkabaki dilemma sielewi nahisi kuchanganyikiwa.
Tutaendelea.....
Acha nipumzishe vidole kwanza ninywe na kajuice maana maisha haya..
Kwann mkuu hebu fafanua kidogo..Nim
Nimeishia kusoma Hadi kati ila wewe ni MPUMB.AVU na ni MSHAMBA
...........Soma nyuzi zote za jamaa Natafuta Ajira .....hapo utajifunza zaidi ya SoMo la wazazi
Naona povu tu linakutoka kwan na wewe ni mnyaturu? Au ndio umekuja humu na hii ID ili kunishambulia?Nim
Nimeishia kusoma Hadi kati ila wewe ni MPUMB.AVU na ni MSHAMBA
...........Soma nyuzi zote za jamaa Natafuta Ajira .....hapo utajifunza zaidi ya SoMo la wazazi
Tisa kwa tano wa kiume na wa kike respectively.Hao watoto wana miaka mingapi? Kwa nini usiwachukue uwapeleke kwa bibi yao? ( mama yako)
Huwa nawaambia wanaume makamo fulani kuwa fainali uzeeni. Unavuna ulichopanda kwa watoto wako wakiwa bado wadogo. Wakishakuwa hauna nafasi hiyo tena, hujui mama yao amewalea vipi ukiwa haupo kwenye picha. Baadae uzeeni malalamiko yanakuwa mengiMuendelezo,,
Baada ya kuona Jamaa yangu ananiangalia nilibaki nawaza tu nikamuonyeshea ishara ya macho tutoke nje akaomba udhuru tukatoka nje, nikamuuliza nikiwa nimejawa na kiwewe
Sasa hapa tunafanyaje?
Akaniambia nilikuambia ufanyeje?
Niakamwambia sasa kweli gharama hizo kama milioni kumi mi naenda kukopa wapi?
Akaniambia nilijua tu unataka kuharibu.
Hebu nipe hiyo bahasha.
Tujaingia ndani nilipigwa butwaa kwa kile alichokifanya jamaa.
Aliongea maneno machache sana akiutetea muda wetu kuwa tuko nje ya muda hata hivyo makazini tumejiiba kwa umuhimu na ulazima wa tukio hili akakabidhi bahasha kwa baba mkwe na kusema maandalizi yetu na dhamira vimefikia hapo huvyo ikiwapendeza kwa hekima na busara watukabidhi binti kwa gharama hizo.
Akafunga mjadala na kuwaachia jukumu la kukubali au kukataa na angalizo lilikuwa kwamba kama hawataafiki basi bahasha zote zilizokwisha kutangulia itabidi zirudi na hiyo ya mahari.
Wakawa wanahesabu na kupokezana mpaka mtu wa mwisho huku wakiongea kinyaturu sisi hatuelewi.
Yakatokea mazungumzo marefu sana baina yao lakini kwa kinyaturu tusielewe wanchojadili
Mwishoni ikawekwa tiki suala likaishia pale wakadai masuala ya koti la mzee bibi sijui kikoi mama na mjomba.
Jamaa akanitoa nje tena akaomba bahasha tano kulingana na idadi ya wahusika tukawekamo 40 kila bahasha tukarudi ndani wakakabidhiwa mchezo ukaisha ikabaki tafrija ndogo iliyokuwa ineandaliwa na wenyeji wetu kwa utaratibu.
Baadae tulipata muda wa kumtembelea bibi kwa upande wa baba mkwe.
Tuliongea nae vizuri na alikuwa mcheshi pia alitufahamisha kuwa ndie amemlea mke wangu
Jamaa akaniambia baadae kuwa macho sana japo hahisi uhatari huo kwenye familia hii lakini kwa machache tuliyoyasikia aliyatumia na kuniambia kuwa mji ule mama ana nguvu sana tofauti na vile tunavyomuona amekaa kimya.
Sikuelewa
Ila baadae nilikuja kuelewa kiufasaha zaidi kutokana na stori za binti mwenyewe.
Tulirudi Daslam kuendelea na maisha mengine.
Mchumba alipewa taarifa zote na yeye akaonyesha kufurahi.
Baada ya muda tulitia maguu kambi ya wazito.
Ninaposema kwa wazito namaanisha wazito haswa maana hata binti kwao ni kuzito lakini baada ya kuingia kambini kwetu alikiri wazi hakuficha alisema mbona kwenu ni kuzito sana?
Nikamzuga tu kuwa hata sijui wala hakuna uzito wowote maana wakati huo sikuwa najua chochote ukizingatia nimekulia mujini Daslam.
Sasa siku ya kwanza tunaingia tu picha niliyomuona nayo mama haikuakisi furaha hata kidogo kama walivyokuwa wanawasiliana kwenye simu.
Maza aliweka ile sura ya kiancient Vampire juu akaweka tabasamu lakini mimi ni damu yake niliuhisi ubaya moja kwa moja uliopo ndani ya mama.
Nikanyong'onyea maana nilijua kuna mziki mzito tena mno
Mwanamke nimempenda na meno yangu yote na kucha zangu zote lakini nishaihisi hatari kubwa kuninyemelea maana kutenganishwa nae sipo tayari lakini naliona likija kabisa ila sipo tayari linikute sijui kama mnanielewa?
Mama alipopata muda aliniambia mwanangu una uhakika umempenda huyu mwanamke?
Nikamuambia ndio nimempenda mama tena sana.
Mama akashika tumbo akaniambia basi ukaishi kwa utashi wako. Nakuamini hutaniangusha.
Akanisihi pia usije ukamtesa hata siku moja maana atakonda abaki kashingo tu hiyo itakuondolea uhakika wa kupata mwanamke mwingine hata ikitokea mmeachana.
Hili neno kuachana liliuchana moyo wangu ile vibaya mno. Sikuwa tayari kulisikia kabisa.
Tukakaa siku tatu
Mama akanifuata akaniambia mwanangu nikushauri tafuta mwanamke mwingine uoe.
Nikamuuliza kwanini? Akanijibu mimi ni mama yako na wewe ni mwanangu mimi tu ndie naweza kukushauri hilo hakuna mwingine.
Akaniambia nimeoa mwanamke mzuri mno tena mno yaani wa kila kitu hivyo nitafute mzuri mwingine pengine anaemzidi au kulingana na huyu nimuoe yaani wawe wawili sio kwamba nimuache huyu.
Kwakuwa nilishakuwa brainwashed na tantalila za watu kwa udhamini wa magharibi, tulibishana na mama mpaka tukatofautiana kabisa hata kipindi tulichopanga kukaa pale kijijini hakikutimia nikabeba vilivyo vyetu tukarudi jiji la wamba.
Maisha yakaanza mke wangu akamleta mtoto wake kutoka kwao lakini mikunjo na visa vya hapa na pale
Mwishowe akafanya maamuzi ya kuwa nimrudishe mtoto Singida
Mimi huyo hadi Ubungo nikampeleka mpaka Singida.
Nikarudi jijini kuendelea na maisha.
Pale nilipokuwa naishi mke wangu akaanza kusema sio watu wa pale hawaeleweki
Nikaona nihame
Nikaenda zangu bahari beach kuke mitaa fulan ya ubaridi.
Nikaanza life kule.
Sababu ya kutokwenda na wife kwao ilikuwa ni mimba
Mke alinasa mimba ndio maana ikabidi nikimbie mapema kwenda kwao.
So baada ya kuhamia bahari beach mimba ikazidi kuwa kubwa..
Lakini kuna dosari ilikuja mapema sana yaani siku ya tatu tangu tuhamie bahari beach nikakamata text kwenye simu ya wife namba ya jirani yangu wa huku huku tulikohamia anajaribu kuweka mazingira ili ajiweke nikamuuliza wife mwamba kapataje namba kiwepesi hivyo?
Akaniambia alimuomba tu wala yeye hakuwaza kama kuna nia mbaya yoyote ile.
Nikajiwazia tu so unahisi umepata bwege umpange eti
Twende tu maana najua kama ni kuliwa utaliwa tu sijakukuta bikra so sina haja ya kuacha majukumu ya taifa nije nikuchunge wewe.
Mitaa hii ni wanajeshi tupu raia wachache sana.
Sasa hawa wanajeshi wakawa wakinicheki wanamuambia wife kuwa kuna sehemu washaniona ila hawakumbuki infact ni wapi so nimewapotea.
Wakawa wanamuuliza wife mume wako anafanya kazi gani?
Wife anawaambia huyu anafanya biashara tu ndogo ndogo wale jamaa wanambishia..
Wakawa wana uhakika kabisa mimi nazijua kazi zao hadi vyeo lakini wao hawanijui ikawa ni tatizo.
Huyu jamaa aliyekuwa anamuwinda wife akajaribu kujenga ujaribu na mimi nikaishia kumuweka pending tu
Kisha siku moja naenda kupanda piki piki jamaa akaja nyuma nyuma ananiita swahiba swahiba. Nikasimama akanisalimia huku akiniuliza unakwenda kazini?
Nikamjibu hapana nasafiri naenda kwetu mara moja tu nitarudi siku sio nyingi.
Akasema sorry nilikuwa na maongezi na wewe vipi unarudi lini?
Nikamjibu nikirudi nikakukuta nitakutaarifu kuwa nimerudi.
Akauliza labda huwa unapiga tungi? Nikamjibu hapana
Vipi labda kumoka?
Nikamjibu hapana sivuti bangi.
Akasema sawa.
Nikasepa kazini.
Usiku nikarudi nikamkuta huyo jirani yangu kafungulia mziki mkubwa sana hadi kero sasa ile nataka kuingua ndani kwangu mara akaniita akanitambulisha manzi yake mmoja hivi sikujali nikamjibu short tu nikazama ndani
Akamtuma manzi kuja kunigongea
Nikatoka akanipa maelekezo kwamba jamaa yule kule anataka mkazungumze.
Kuicheki tembea ya demu nikajua nae ni mjeshi pia.
Nikamfata jamaa tukawa tunaongea japo jamaa alitaka anitoe mazingira ya pale home ila mi sikutaka kabisa
Basi akaishia kuongelea pale pale.
Aliongea vitu vingi ikiwemo kuulizia mishe zangu nikamjibu lakini alikuwa na mashaka kidogo.
Nikamwambia je anampenda sana wife kiasi isingetokea mimi kumuoa yeye angemuoa au anataka tu aonje ladha iliyomo ndani ya ule uzuri apite hivi?
Jamaa akabaki ameduwaa huku akisema aisee broo mbona umeenda mbali sana angalia tusijetukatoleana bastola kizembe.
Nikamuambia ningekuwa hivyo angekuwa futi sita chini tayari.
Jamaa akafurahi sana pia akanisifu kuwa sikai na kinyongo hivyo ni rafiki wa kweli akaniuliza kama natumia wine nikamuuliza anamaanisha nini
Akasema anataka twende tukanywe kidogo maana hajawahi kumpata mtu genuine kama mimi
NIkamjibu sihitaji wala.
Nikarudi zangu ndani.
Baadae nilimsafirusha mwanamke kwao baada ya siku za kujifungua kukaribia.
Mwamba sasa akaona ndio chance ya kujiweka karibu na mimi
Lakini kila alipojaribu nilimzuia maana kwa hilo nina mbinu zote wala sio shida.
Akaanza kufuatilia taarifa zangu popote alipohisi kuwa anaweza kuzipata hata kwa baadhi ya watu waliokuwa wananitembelea.
Lakini hakuna alichoambulia maana hata hao marafiki hawakuwa wakinijua kihivyo sembuse majukumu yangu?
Baadae nilihama pale nikiwa na taarifa zote juu ya watu wengi wa pale
Na wonderful ni kwamba huyu jamaa yeye alikuwa ni mwanajeshi wa nyota moja lakini jambazi la mbali sana ambapo matukio alikuwa anayapiga kwa raketi za simu then yeye ndiye mshika mtutu aliyeiva
Yalipita hayo na pale Nilihama wife akiwa bado hajarudi.
To cut the story..
Kule ukweni baba mmwe aliniulizaga swali hili lini utfunga ndoa na kufanya harusi?
Nikamjibu kuwa ngoja nifanye maandalizi nikikamilisha mipango yote nitaweka tarehe rasmi.
Lakini imepita miaka na binti yake tumepata mtoto wa pili tabia ikabadilika kabisa misuguano imeanza ndani nyumba
Maneno yamekuwa mengi kumekuwa na changamoto za hapa na pale maisha yakikaza pesa ikikosekana tu binti anakuwa mwiba mara anatoroka anakwende ambako anajua kuna ndugu zake hata kama wako Dodoma anaenda anakaa hata miezi sita nikikaa vizuri kiuchumi anarudi.
Nikaona huyu nikifunga nae ndoa halafu nikawa nimejenga vijumba kadhaa si atanivuruga huyu maana atataka aondoke mazima akijua mali tunagawana?
Lakini pia suala la unyumba lilifika baadhi ya miaka likawa linasua sua kabisa yaani mfano mimi hupenda nikikaa na mwanamke nimchezee maziwa na makalio yeye kwake ni noo.
Nikaona hapa nina picha tu ya kuku rosti huwezi kumla.
Nikaanza kumkumbuka mama kwa hili.
Kuna muda anakwambia hamu ya tendo la ndoa imekata kumbe alienda kwenye uzazi wa mpango akaweka vijiti.
Sasa huu mwaka mwanzoni ndio akasepa na kusema anarudi kwao nilikuta tu mtu keshasepakarudishia tu mlango kwakuwa nina madog nayafuga usalama ulikuwepo.
Sasa baadae ukweni wananiuliza kwanini nimeishi na binti yao kihuni sana kwa muda wote huo?
Mara kwanini sikumfungulia biashara binti yao muda wote huo hadi nimefulia?
Wakaenda mbali na kusema ni kweli ulilipa mahari lakini hukufunga nae ndoa hivyo ana haki ya kurudi pale nyumbani na akapata mwanaume mwingine akamuoa na hautakuwa na haki ya kudai chochote.
Nikakaa kimya hapo nikiwa naongea na kaka mtu akaenda mbali zaidi na kusema kuwa nimemnyanyasa mdogo wao.
Mambo mengi tu na biti juu.
Nikamjibu kuwa nimepiga simu nataka mke wangu arudì tuendelee na maisha maana mimi sijamuacha bali ameondoka mwenyewe.
Kaka mtu ananiambia kuwa ukipata pesa hunsikilizi mdogo wangu lakini ukifulia unaanza kumuona mtu wa maana.
Akanichimba biti kuwa aisee akirudi kwako tena ukapata pesa ukamnyanyasa labda niwe nimekufa
Nikamuuliza mnaposema alikuwa ananyanyaswa nilikuwa naishi na nyie wote?
Akawaka nikamuwashia moto maana anataka kutengeneza mazingira ya kunitawala mara oo umfundishe mkeo biashara unazofanya.
Nikamjibu tu kuwa wewe hujaoa,, Oa kwanza tuongee lugha moja. Akapanik akatema shiti nikazikusanya mara tano nikampa akakata simu.
Nikakaa kimya nikaazimia kumpelekea mwanamke watoto wake huko huko kwao.
Watu wakanitonya kuwa hakwenda kwao bali ndugu zake walimpa pesa akaenda kupanga mitaa fulani hapa hapa Mwanza.
Nikapeleleza hadi nikafika alipo kimya kimya baada ya kuhakikisha ni yeye nikachukua watoto nikampelekea akashangaa sana
Halafu mimi huyo.
Baadae ndugu zake wanasema nimeenda nimemtelekezea watoto mara ooh kama nataka yaishe mke wangu arudi home nikusanye wazee wangu twende pale Singida tukakae kikao nikawaambia hilo halipo kwenye bajeti yangu kama ingekuwa ni kurudi nilishamuomba na kuwaomba wamshauri binti arudi kwake lakini hola mwezi wa sita huu
Na mimi nimeamua kuhama mkoa kabisa yaani hata hivi vitu vilivyobaki nishamuambia nampelekea vyote tukakubaliana
So sasa huwa naenda tu pale alipopanga kuwaona madogo then nageuka
Maana yeye hajui kama nikiondoka mkoa huu ndio itakuwa mwisho wa mimi kuongea na yeye na hao watoto.
Anadhani nitaendelea kuhudumia kama vile yuko kwangu.
Wakuu ni jibu gan lilifaa kuwapa hawa wa ukweni ambalo litaacha mwanya baada ya miaka saba nikachukue watoto wangu
Maana najua atawapeleka tu kwao yeye arudi kudanga mujini.
Jana tu ndio nimetoka kuwaona wananilalamikia kuwa mama yao anawaambia awapeleke Singida lakini hawatakiHuwa nawaambia wanaume makamo fulani kuwa fainali uzeeni. Unavuna ulichopanda kwa watoto wako wakiwa bado wadogo. Wakishakuwa hauna nafasi hiyo tena, hujui mama yao amewalea vipi ukiwa haupo kwenye picha. Baadae uzeeni malalamiko yanakuwa mengi
Napita tu 🏃♀️
Obhoene kimwi mura weitoMura kazaliwa mjini, amekuwa mwanaume wa dar anavaa makoti marefuu marefu wenyewe wanayaita obama
Hakikisha wanajua baba yupo, anatujali na kutuhudumia. Baadae wakiwa wakubwa kidogo na huru zaidi lazima watakutafuta wakiona ni kweli unawajali.Jana tu ndio nimetoka kuwaona wananilalamikia kuwa mama yao anawaambia awapeleke Singida lakini hawataki
Nikawaambia waende baada ya muda naenda kuwachukua wakakubali kinyonge sana.
Kwa point hii utasababisha kesho nikampore watoto tena yaani mbona ni balaa hili?Hakikisha wanajua baba yupo, anatujali na kutuhudumia. Baadae wakiwa wakubwa kidogo na huru zaidi lazima watakutafuta wakiona ni kweli unawajali.
Malaika hao wakienda singida huenda wataambiwa (si kwa maana ya kuambiwa, lakini kusikia kwenye mazungumzo ya watu wazima) baba yao ni mtu wa ovyo aliyewakimbia. Maana wanaona mama yao anavyohangaika kila kukicha na baba anakuja kwa kuchungulia.
Inasikitisha lkn wanawake akili zetu saa nyingine tunazijua, sana sana akiwa na maumivu moyoni. Matokeo hautaona sasa hivi, miaka baadae
Mtafute yule mubaba mshenga anaweza namna ya busara kukushauri, anakufahamu ana amewafahamu wale pia kwa kiasi fulani.Kwa point hii utasababisha kesho nikampore watoto tena yaani mbona ni balaa hili?
Siku nyingine mahali unayotaniwa sio halisi kivile halisi ni ile uliyotunza mwenyew au sio babuHii ni mimi huyu Sonko sio mwingine,,
Short story huko nyuma nyuma hivi nikiwa kijana.
* * *
Miaka imeenda sana,,
Kwa jadi ya kabila letu wanaona nimepaa sana age halafu sieleweki.
Zingatia sieleweki yaani,
Hawasikii Sonko kuwa na demu,
wala zile kesi za ajabu ajabu.
Kifupi mtaani nimechill sana.
Sina urafiki na vijana,
Bali wazee ndio natumia time kubwa kukaa nao
Napenda kuwafuata wazee hasa nikiona yule anaependa kukaa peke yake.
Kuna vitu nafyonza kwao.
Lakini hawanishauri kuhusu mahusiano maana hawana uhakika kama upande nautazama sana.
Na mimi sioni kama kuna umuhimu kuulizia hizo mambo.
Lakini kumbe laiti ningejua ningebase huko pengine ningepata maarifa ya kutisha..
Kwenye simu za hapa na pale na maza,
Ni kelele tu za hivi utaoa lini huoni unazeeka?
Nazeeka vipi sasa wakati niko 23?
Presha ikazidi nikahisi bi mkubwa anaweza kuwa sawa mi ndio nikawa navurunda eti.
Nikaanza kufukuzia visichana hapa na pale,, kumbuka mi mgeni kwenye gemu sijawahi kuwamo kabisa.
So hata walipokuwa wakifanya flirtings zao sikuwa nikielewa lolote yaani.
Ugumu unakuja maana nawinda watoto ambao ni hotcake za mujini.
Tena muji wenyewe ndio huu huu niliokulia wa Daslama?
sio kweli, hapa ni full kuliwa nauli na salio,
Wale wanaoshoboka nawaona sio ndoto yangu.
Nataka nipate mtoto ambae nikimsimamisha na Nikki Minaji watoke droo.
Kitu sikujua ni kwamba nawinda kupata mke ndani ya makahaba,, na ukicheki nilivyokomaa utadhani nina status ya pull factor kumbe ni Ngoswe tu aliyezamia Daslam.
Likaja wazo la kiwaki,, sijui hata lilitoka wapi maana uvunguni hamna kitu na kusafi daily.
Nikampata binti mmoja wa Mbagala nikampa dili kuwa anizalie watoto wawili nampa m2. Akakubali akazidisha mawasiliano sasa.
Usiku kuanzia saa tatu hadi sa saba ni mwendo wa kuongea sasa mi ni introvert naona ananikera yaani akipiga simu nawaza nitaongea nae nn?
Kama ni maneno nahisi nishamaliza yote.
Magetoni nina mwamba wangu mmoja yeye anasoma St Joseph unvst.
Nikamshirikisha hili wazo maana ni mwanangu since wayback na tulishaapa kujenga nyumba zetu sehemu moja.
Mwana akaniambia homeboy, unafeli hivi hivi nakuona.
Mbona una presha kubwa hivi? Sijakuzoea hivi ujue..
Namuuliza why nafeli?
Ananijibu utapigwa.
Namuuliza how?
Ananiuliza je huyo binti akitaka umuoe utamuoa?
Namjibu siwezi kumuoa maana mkataba wetu hausemi nimuoe.
Tumekubaliana anizalie watoto tu then maisha mengine yaendelee.
Jamaa ananiuliza je ana mtoto kwanza?
Namuambia hajaniambia kama ana mtoto.
Ananiambia, muulize kwanza.
Napiga simu hapo hapo nakuuliza halafu kitu iko loud speaker.
Binti anatomboka vya kutosha.
Lastly hana mtoto.
Jamaa yangu ananiambia,, utapigwa halafu utaachiwa maumiv na watoto wako hutakuwa na access ya kuwa nao maaan wao ndio source ya mkataba.
Namuuliza how?
Anasema ushamuonyesha kuwa yeye humuhitaji bali watoto tu.
Unadhan kama yeye anakuhitaj atatumia njia gan kujimilikisha kwako?
Hapo sasa naanza kumpata vyema homeboy anachomaanisha.
Ananiambia kuwa mimba ni kweli atakubebea lakini hatokupa watoto maana wanawake huupenda sana uzao wao wa kwanza hata kama mtoto atatoka taahira niamini mimi kitinda mimba anaweza akanyimwa kitu akapewa kifungua mimba.
Nikamcheki homeboy kwa sekunde kadhaa huku nikijiwazia,, now this is a worth friend.
Hilo likapita Sonko nikabaki salama.
Lakini kumbe ibilisi alikuwa na mipango ya kuniweka spana sio poa
Jamaa akanishauri kwanini usimuoe fulani akifanya reference ya mabinti nilioskuli nao, nikampinga maana niliona viatu vile na safari yangu nitaburuza sana njiani sitafika.
Siku zikasonga nikiwa job nikakutana na kabinti kamoja raia ya singi, nyaturu moja Omufanga,, wajo fingijo fingijo.
Manzi nikamnoki ile sana but sijui kama nae alininoki sielewi si unajua moyo wa mtu kichaka.
Nikaanzisha nae mawasiliano tena kwa tahadhari ili nisijekumkera akasepa,,
Maana nishamunoki( mpenda) sana.
Ikapita like miezi miwili nikamtongoza kawaida tu nikamwambia nataka nimmiliki mazima, akatishia kunizimia fegi hata pafu sijapiga.
Nikaona nishawakosa kibao sana tena ambao nilitamani kuwa nao.
Kama anazima fegi sio dhambi pia sitakufa.
Mara time ilivyoenda akaniambia anataka kuja kupaona geto napokaa
Kwasababu nilikuwa na mwanangu geto sikutaka kuchanganya maisha kabisa nikamkatalia nikamwambia nina mwamb naish nae na ni mwanangu sana so sio picha nzuri.
akasema sawa.
Siku moja akaniambia nije au kila siku mmegandana magetoni tu?
Nikamwambia njoo leo mwana yuko chuo na kaniaga atakaa kwa manzi yake walau siku tatu.
Manzi akaja akakuta nimepika wali na kibua wa nazi za bahkresa.
Tukala tukakaa kupiga stori.
Nikaweka muvi tukawa tunaangalia tu kumbuka mimi sijawahi kusex na manzi yoyote so siichukulii kwa uzito huo uwepo wake geto kwamba anaweza akaniruhusu nimpige ukuni.
Manzi mara akanishika shingo akataka mate.
Na mimi nikampokea tukaanza romance hapo mlango wa geto uko wazi.
tunaanza kuzama kwenye feeling mara anakuja mjukuu wa mwenye nyumba kijana mdogo miaka like ten years anatukata stimu anaomba kitu fulan katumwa na bibi yake nampa then nalock kabisa mlango maana kaliingia hadi nditch kalishazoea kanakuja hata muvi tunaangalia na vitoto vingine
Vinakaaga kwenye kapeti unyoya.
Mikiki mikiki inaanza tena,, this time tunaenda hadi ndani ndani humo sipajui jina lakini nasikia kuna kumwaga.
But nagundua kumbe ngono kwa mara ya kwanza kwa mwanaume huwa haina ladha kabisa but as time goes ndio anaanza kuenjoy na kuitaka pengine zaidi ya msosi?
Aniambia tupige cha pili tena nawaza sasa kama ladha yenyewe hamna sasa narudia ili iweje anauchukua ukuni ambao kitendo cha kuuwekea mkono tu unakuwa mnara juu.
Anaukalia anafanya yake mi nampa kampani kiasi tu maana siko mchezoni kabisa.
Baada ya muda anaondoka anarudi alipotoka.
Ananiacha nikitafakari sasa inakuwaje watu hadi wanapiga makelele vile wakati hakuna cha ajabu?
Muda na shetani vinaniambia subiri tu we mwana usie na hatia utatufahamu tu tutakupa vingi bado hujajua.
Baada ya siku kadhaa anakuja tena tunafanya tena ila awamu hii mimi ndio naupata ule utamu na ladha so ninafanya na kufanya tena namuomba tena ananipa na kunipa tena nanogewa.
Mwanangu kesho yake anarudi na kuniambia kuwa ameshapata mwanae mmoja hivi pale pale chuo so anahamia pale ili kupunguza gharama za nauli
Naumia sana maana ni mwana ambae nimemzoea sana.
Nabaki mpweke. Napiga simu kwa manzi yangu namuunganisha waongee mshikaji anamuambia manzi yangu yeye anaenda mbali kidogo so siku akitukuta atamuona wala haina kabaya.
Manzi anapata taarifa rasmi kuwa nitakuw mwenyewe so ananiambia kama vipi aje tukae wote wakati wetu huu wa uchumba nasema sio mbaya.
Kesho yake baada ya mwamba wangu kuondoka manzi anakuja mida ya jioni na mabegi yake.
Anajimilikisha gheto la Sonko.
Anafanya makaratee kibao vitu ambavyo sikuwa navyo ananinunulisha
Hapo ndio naamini kweli nyumba ni mwanamke..
Mazungumzo baina ya yeye na maza yanashamiri muunganishaji nikiwa ni mimi hapo.
Linakuja seke seke jingine, wanawake hawatosheki yaani,, Mama anadai nimpeleke nikamtambulishe bush.
Manzi anasema hapana tuanzie kwao Singida kwanza.
Ninamwambia hapana tuanzie kwetu kwanza hapa dar Mshua akuone maana nimelelewa na mshua.
Then tukitoka kwa mshua twende kwao Singida mwisho tumalizie kwetu Tarime kwa Maza.
Maana wazazi wangu walitengana miaka kibao iliyopita kiasi nimekuwa dingi sikuwahi kumuona mpaka nimefika miaka tisa.
Then mvuum!! Mshua huyu hapa hataki maelezo kanipitia kama kipanga.
Tukaenda kwa mshua kisha nikaenda kwao.
Kwao sikwenda nae nilienda mwenyewe zingatia hapa kwenye kwenda mwenyewe bila yeye ndipo kiini na usumbufu wa hii stori ùlipo.
Nilienda mzee akanikabidhi mtu wake wa mkono tukaenda ukweni.
Na jamaa ndie aliniambia tusiende na binti kule kwao.
Huyu jamaa ni mwamba sana
Yaani ukimuona huwez kuidhania akili kubwa aliyonayo hata kidogo.
Baadae ndio nilielewa ni kwanini mshua alimteua huyu mtu.
na hapa ndipo niliacha kumunderate mshua.
Iko hivi
Jamaa aliniuliza ukiniangalia labda nina miaka mingapi?
Kwakuwa nilikuwa 23 na nikimuangalia jamaa namuona kama mchizi moksi fulani nikamuambia nakukadiria kwenye miaka 32.
Akakaa kimya kidogo kisha akaniambia nina miaka 48.
Nikashituka sana, amenizidi miaka 25? How?
Jamaa akaniuliza huko tunakoenda mke wetu yupo huko ?
Nikamwambia hapana.
Akauliza yuko wapi nikamuambia niko nae geto. Ila jibu hili nililitoa nikiwa sijiamini sana maana nilihisi labda jamaa ataona nishavuruga taratibu tayari.
Jamaa akakaa kimya kidogo akiwa ananitazama kiaina.
Kisha akaniuliza nani alikuambia umtunze gheto kwako ilihali hujamlipia mahali?
Nikamjibu amekuja mwenyewe na tunaishi hii sasa wiki ya nne.
Jamaa akasema vizuri hata kama angekuwa Singida ningekwambia umuite aje gheto kwako umuache gheto kwako then ndio sisi twende kwao Maadamu tayari yuko kwako basi haina shida.
Sikumuelewa maana yake mpaka tulipotoka huko ukweni,, nitaelezea huko mbeleni.
Safari ilianza na tulifika saa kumi na moja jioni tukapokelewa na wenyeji wetu..
Tulilala palipopambazuka taratibu zote zilifuatwa tukatozwa faini ya kimtindo maana tayari tulihesabika kama wezi kulingana na taratibu za huko Singida na jamii nyingi tu Afrika.
Basi tulitoa kishika uchumba,, lakini Jamaa akaniuliza uko vizuri? Nikamjibu ndio akaniuliza una bei gani nikamuonyeshea vidole viwili akaelewa akaomba udhuru tukatoka nje akaniambia lete bahasha nikatoa maana aliniambia mapema tukiwa Dar kuwa nihakikishe nakuwa na bahasha ndogo zisizopungua 30 basi nami nilikuwa nazo kwenye mifuko ya koti lote la suti yale makoti marefu maarufu kama Obama.
Nikatoa bahasha kumi kisha kila bahasha nikawekamo elfu kumi kumi kisha akaniambia chukua bahasha mbili wekamo elfu 30 kila moja ila zitenganishe na zile za elfu kumi kumi.
Nikafanya hivyo akaniambia zile mbili ni kwaajili ya wazazi tu zile nyingine ni kwaajili ya wajumbe wengine.
Tukarudi kikaoni kikao kikaendelea
Jamaa akasema kuwa ni ombi la kijana wangu kuja kwenu amalize kila kitu leo
Kisha akanipa ishara nianze kuchapa bahasha mezani. Nikachapa bahasha nikaona kila mtu anachungulia yake kivyake.
Wazazi nao wakachapwa za kwao ukimya ukatanda.
Kikao kikaendelea wazee wakatetema wakiulizana suala la mahari wakaomba tuwapishe ili wajadili mahari ya binti wao.
Tulivyotoka nje Jamaa akaniuliza binti ana mtoto? Nikamjibu ndio ameniambia juzi hapa na hakuwahi kuniambia siku zote.
Jamaa akaniambia hakuna shida sisi ni wakurya.
Akaniambia chukua bahasha moja weka laki tano tu kisha tulia shughuli nyingine niachie mimi.
Nikabaki nimeduwaa wakati mimi nilikuwa nawaza hata milioni mbili hivi?
NIkamuuliza kwanini? Haoni kama itakuwa ni kidogo sana?
Akaniuliza unadhani baba yako alikosea kunituma huku?
Ipo siku utaelewa baba yako ni nani we tulia tu nimekwambia shughuli yote niachie mimi. Nikikupa nafasi tu utaharibu na mzee wako aliniambia nisikupe nafasi utaharibu.
Kauli ile ilianza kunitoa kwenye reli ghafla.
Nikijiangalia nina pesa na mwisho wa mwezi uhakika utaniambia nini umri wenyewe wa kwenda klabu kwanza halafu mimi ndio sijui hata hizo starehe zaid ya kuipambania shilingi.
Jamaa alinituliza tuli kumbuka ni mkubwa sana anaweza kunizaa kabisa lakini tunabonga kihuni ile mbaya.
Tukarudi ndani wakatutajia mahari ambayo niliona ni wazi hapa tumekuja kudhalilika mimi na Mshenga wangu.
Nikabaki nina mshangao wa ndani japo mdomo haukufunguka lakini machoni tu ungeweza kuusoma mshangao wangu.
Yaani sio hata ile niliyokuwa naiwaza sembuse hii tuliyoweka kwenye bahasha?
Nikawatazama machoni wale watu kasoro mama mkwe.
Nikawaona wametulia wanatusubiri sisi tutoe jibu.
Nikamtazama mshenga wangu nae akawa ananitazama tu kama ananiuliza unasubiri nini?
NIkabaki dilemma sielewi nahisi kuchanganyikiwa.
Tutaendelea.....
Acha nipumzishe vidole kwanza ninywe na kajuice maana maisha haya..
Yap wew piga bahasha mezan baada ya kuwa umetanguliza bahasha za wajumbe hakikisha bahasha zilizotangulia zinaenda kama laki tatu hiviSiku nyingine mahali unayotaniwa sio halisi kivile halisi ni ile uliyotunza mwenyew au sio babu
Kwa sasa mimi siwezi kuishi nao maana ni traveller simu ikiita nachukua mission ndio maana nikaamua nimkabidhi yeye awalee popote atakapokuwa nitafika hata baada ya miezi miwili kutegemea na mission itakapoisha hata ikichukua miezi mitano bado nitaweza kufika kuwaona..Chukua watoto wako piga chini hao ndugu na mama yao. Watoto usiwapeleke kwa bibi yao(mama yako) komaa nao kwa bibi uwe unaenda nao kusalimia. Mkuu hili ni gumu ila ni fundisho zuri kwa watoto wako na hutafanya makosa tena katika kuwatafutia watoto mama bora.
Basi wapeleke kwa bibi yao. Hiyo familia hujui watakupaka tope gani kwa watoto.Kwa sasa mimi siwezi kuishi nao maana ni traveller simu ikiita nachukua mission ndio maana nikaamua nimkabidhi yeye awalee popote atakapokuwa nitafika hata baada ya miezi miwili kutegemea na mission itakapoisha hata ikichukua miezi mitano bado nitaweza kufika kuwaona..
Kuna Jamaa mmoja yeye alioaga dada mtù way back huko kamchukua mwanae juz hapa baada ya kumaliza la saba.Basi wapeleke kwa bibi yao. Hiyo familia hujui watakupaka tope gani kwa watoto.
Muhimu umlee mtoto wako. Unaweza kuta mtoto analelewa ovyo mwisho linatoka toto ya ajabu under your nameKuna Jamaa mmoja yeye alioaga dada mtù way back huko kamchukua mwanae juz hapa baada ya kumaliza la saba.
Hii nayo point ya msingi sana etiMuhimu umlee mtoto wako. Unaweza kuta mtoto analelewa ovyo mwisho linatoka toto ya ajabu under your name