Njaa Arusha; watu waanza kuiba hadi ugali Meru

Njaa Arusha; watu waanza kuiba hadi ugali Meru

Don Moen

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2020
Posts
1,636
Reaction score
3,142
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wananchi wa Meru Arusha wamepigwa na butwaa kwa vitendo vya udokozi na wizi wa vitu mbambali pamoja na vyakula vya aina mbalimbali vilivyoiva au vibichi.

Kumekuwa na malalamiko mengi ya watu kuibiwa hasa jikoni na kuibiwa vyakula kama ugali, ndizi, karoti na chochote kitakachopatikana.

Hali hii imekuwa gumzo hadi kupelekea mchungaji wa Pentekoste Kata ya Ambuereni aitwaye Merinyo
aliyekuwa anaongoza mazishi siku ya leo kuwataka waombolezaji wasimame na kuombea hali hiyo kwani inatishia usalama wa raia.

Hali sio nzuri, tunaibiwa hadi ugali? Hali ambayo haijawahi kutokea katika historia ya Meru...Alisika Mchungaji Merinyo.

Hali hiyo inajitokeza wakati vyakula na mafuta vimepanda bei kupindukia ambapo bei ya mchele imefikia sh.3,500/kg, unga 2,000/kg, mafuta ya kupikia ni 7,500/lita.

Mungu alete mvua hali inatisha.
 
Arusha mafuta lita 7500/= mmh
Wiki iliyopita nimenunua lita 5 shilingi 22500 sawa na 4500/= kwa lita tena Alizet hapahapa arusha

Hii stori imekaa kimbea sana
We muongo
Labda ni yale mafuta wanayosindika wakulima wa alizeti ya viwango vya chini ambayo hayajathibitishwa na na tbs ambayo ni hatari pia kwa mlaji.
Sundrop lita 5 ni 36000 tena kwenye maduka ya jumla.
 
Ungalimtd kuna Mama alikuwa anapika ugali jikoni mida ya mchana kweupe vibaka wakaja wakamkwapulia simu aliyokuwa ameshika ugali na mboga wakapita na mia
 
We muongo
Labda ni yale mafuta wanayosindika wakulima wa alizeti ya viwango vya chini ambayo hayajathibitishwa na na tbs ambayo ni hatari pia kwa mlaji.
Sundrop lita 5 ni 36000 tena kwenye maduka ya jumla.
Kama uko arusha fika majengo asubuhi alizeti safi inakamuliwa ukiona ni 4500 na mimi situmii mafuta mengine...
Hayo unayosema hata sijaui..
Hivi kinachodhibitishwa ni mafuta au ni mbegu zinazokamuliwa?
 
We muongo
Labda ni yale mafuta wanayosindika wakulima wa alizeti ya viwango vya chini ambayo hayajathibitishwa na na tbs ambayo ni hatari pia kwa mlaji.
Sundrop lita 5 ni 36000 tena kwenye maduka ya jumla.
Na bei za mafuta zinatofautiana mkoa na mkoa hasa mikoa inalima alizeti ni chini zaidi mfano singida kuna wakati ni 16500 lita 5 ila sasa sijui
 
mtoa mada hana uongo wowote..

wamasai wanatoka huko njia ya longido wanakuja kuomba chakuka kwenye mageti ya watu....ukiwapa hata unga nusu kl wanapiga goti kushukuru...

pengine hali bado haijawa mbya zaidi kwenye eneo unaloishi..
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wananchi wa Meru Arusha wamepigwa na butwaa kwa vitendo vya udokozi na wizi wa vitu mbambali pamoja na vyakula vya aina mbalimbali vilivyoiva au vibichi.

Kumekuwa na malalamiko mengi ya watu kuibiwa hasa jikoni na kuibiwa vyakula kama ugali, ndizi, karoti na chochote kitakachopatikana.

Hali hii imekuwa gumzo hadi kupelekea mchungaji wa Pentekoste Kata ya Ambuereni aitwaye Merinyo
aliyekuwa anaongoza mazishi siku ya leo kuwataka waombolezaji wasimame na kuombea hali hiyo kwani inatishia usalama wa raia.

Hali sio nzuri, tunaibiwa hadi ugali? Hali ambayo haijawahi kutokea katika historia ya Meru...Alisika Mchungaji Merinyo.

Hali hiyo inajitokeza wakati vyakula na mafuta vimepanda bei kupindukia ambapo bei ya mchele imefikia sh.3,500/kg, unga 2,000/kg, mafuta ya kupikia ni 7,500/lita.

Mungu alete mvua hali inatisha.
Acha ku-generalise
 
hivi mbona sijaona huo mchele wa 3500 mpka sasa au nyie mnanunua mchele kwenye super market nn maana nanunua mchele umenyooka 2200 huo wa 3500 ni wakupikia mbinguni nn
 
We muongo
Labda ni yale mafuta wanayosindika wakulima wa alizeti ya viwango vya chini ambayo hayajathibitishwa na na tbs ambayo ni hatari pia kwa mlaji.
Sundrop lita 5 ni 36000 tena kwenye maduka ya jumla.
tumekuzwa na mafuta ya kukamua alizeti wenyewe tena nakumbuka zilikuepo mashine maalumu mnaenda kukamua alizeti iweje leo useme tbs kukamua alizeti kunahitaji vipi tbs au ukisasa unawasomba vibaya
 
Mtoa mada mmbea or else ni huko Arumeru kwao ndio kuna shida.. ama ni mimi sijichanganyi sana…

Me naona Arusha City tuko kawaida tu, ukiondoa suala la mchele.. unga sijui, huu mwaka wote sijawahi nunua unga dukani.
Asee mkuu wewe na Smart911 mbona avatar picha zenu zinafanana?
 
Back
Top Bottom