Njaa inanukia, mvua zimegoma. Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi

Njaa inanukia, mvua zimegoma. Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi

The Sunk Cost Fallacy

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
19,582
Reaction score
14,167
Habari za mida..

Kuna dalili za njaa mwaka ujao kutokana na Hali ya ukame inayoendelea Nchini kwa sasa.

Sio jambo la kawaida kwa mwezi huu wa disemba mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutokuwa na mvua.Sehemu nilipo wananchi bado hawajaotesha Mazao kwa sababu mvua hazipo.

Hali ya hewa ni jua,joto,upepo na manyunyu tuu huku nzi wakitamalaki.

Chonde chonde Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi maana hivi tunavyoongea bei za Mazao zimeanza kupanda.Hata wale wa mahindi waliokuwa wanalia saizi wanauza kwa bei ya Kati ya 45,000-55,000 kwa gunia huku mikoani.

Ili kunusuru chakula kilichopo,nashauri serikali ipige marufuku exports ya Mazao yote ya chakula.

Kama Hali hii itaendelea ,Wananchi tujiandae kisaikolojia.Ukame umeeneo si tu Tanzania bali Hali ni mbaya zaidi Ethiopia,Kenya na Somalia.

Watu wa Hali ya hewa walitabiri hali hii toka mwezi wa tatu,wakarudia mwezi Juni na mwezi November.

Mwenzako akinyolewa zako tia maji 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220603-163731.png
    Screenshot_20220603-163731.png
    179.7 KB · Views: 11
Una wazo zuri lakini usiseme tu serikali ipige marufuku kuuza mazao nje, muhimu serikali pia iangalie namna ya kumsaidia mtumiaji wa mwisho asije kuuziwa kwa bei ya juu japo nashauri pia wakulima waangaliwe ili wafidie gharama zao walizoingia kwenye pembejeo, kusema kweli tunapoelekea hali itakuwa mbaya sana, nauona mfumuko wa bei ukiongezeka mara mbili.
 
Una wazo zuri lakini usiseme tu serikali ipige marufuku kuuza mazao nje, muhimu serikali pia iangalie namna ya kumsaidia mtumiaji wa mwisho asije kuuziwa kwa bei ya juu japo nashauri pia wakulima waangalie ili wafidie gharama zao walizoingia kwenye pembejeo, kusema kweli tunapoelekea hali itakuwa mbaya sana, nauona mfumuko wa bei ukiongezeka mara mbili.
Hakuna namna ya kumsaidia zaidi ya kuzuia Ili supply isipungue.
 
Njaa?

Hebu nenda vijijini huko ndanindani, watu vyakula vimejaa hadi vinawashinda. Kiasi kwamba mgeni ukija na kurudi mjini wanakufungashia mizigo ya maana wapungukiwe kidogo tu. Na wana akiba ya kula mwaka mzima ila bado wanalima, tatizo hawafanyi biashara kama ilivyo wengine.

Balaa la mjini na gharama za maisha visikufanye uamini hivyo
 
Njaa?

Hebu nenda vijijini huko ndanindani, watu vyakula vimejaa hadi vinawashinda. Kiasi kwamba mgeni ukija na kurudi mjini wanakufungashia mizigo ya maana wapungukiwe kidogo tu. Na wana akiba ya kula mwaka mzima ila bado wanalima, tatizo hawafanyi biashara kama ilivyo wengine.

Balaa la mjini na gharama za maisha visikufanye uamini hivyo
Wapi huko tuje kuwatembelea kama kunafikika..

Kama hakufikiki ndio shida.
 
Wapi huko tuje kuwatembelea kama kunafikika..

Kama hakufikiki ndio shida.
Tembeeni ndugu mjionee mengi, mjini ni kutokana na mfumuko wa bei na pia gharama za kusafirisha ndiyo maana bei ipo juu. Kuna jamaa yangu alikuwa shinyanga huko ndanindani, anasema watu wamevuna vitu mpaka pa kuziweka kumejaaa.

Kaka yangu alienda kijijini kwa mama yake kwa wandamba, alipewa magunia ya mchele hadi alishindwa kuyasifirisha kwenda stesheni. Watu ugali hawaujui huko ni mchele tu na bado akiba wanayo kubwa
 
Ulinisaidia kununua mbolea mbegu aunkuniletea bwana shamba anishauri juu ya ulimaji wang

Mnaona Hal mbaya mnataka kutuzuia tusiuze nje


Ningekuona wa maana ungesema serikali iongeze Bei ya mahind na inunue kwa Bei itakayo mnufaisha mwnanchi

pembejeo zimepanda Wala hushupaz shingo kututetea kuwa serikal itoe ruzuku.

Tubadilike jaman tusiwe wabinafsi

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Habari za mida..

Kuna dalili za njaa mwaka ujao kutokana na Hali ya ukame inayoendelea Nchini kwa sasa.

Sio jambo la kawaida kwa mwezi huu wa disemba mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutokuwa na mvua.Sehemu nilipo wananchi bado hawajaotesha Mazao kwa sababu mvua hazipo...
Serikali ndo iliwalimia na kuwatunzia mazao? Achana na wakulima wafanikiwe.
 
Mkuu unawazo zuri sana Ila Kuna ubinafsi ndani yake. Ninayasema haya Kama mkulima pia, hoja ya kuzuia mazao kutoka nje ni ya ukandamizaji kwa wakukima tabu tunazopata na bei za pembejeo mbona hamuisemi serikali iweke luzuku kwenye mbolea? Bei ya mbolea mwaka huu haikamatiki mbona mpo kimya?
 
Mkuu unawazo zuri sana Ila Kuna ubinafsi ndani yake. Ninayasema haya Kama mkulima pia, hoja ya kuzuia mazao kutoka nje ni ya ukandamizaji kwa wakukima tabu tunazopata na bei za pembejeo mbona hamuisemi serikali iweke luzuku kwenye mbolea? Bei ya mbolea mwaka huu haikamatiki mbona mpo kimya?
Mkuu nchi ya ajabu hii

Unaweza kuta huyu ndio mtunga Sera Tena wizara ya kilimo

Nchi ina ombwe la watu kuwa na fikra pevu wamejaa ubinafsi tu

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom