Nje ya Arusha Mjini na Mbeya Mjini kuna miji gani mingine wazawa wa asili wameziachia sana fursa ziende kwa majirani zao?

Nje ya Arusha Mjini na Mbeya Mjini kuna miji gani mingine wazawa wa asili wameziachia sana fursa ziende kwa majirani zao?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Arusha Mjini - wazawa asili Kuna Wameru na Waarusha, niliwahi kuishi hapo miaka mitano, cha ajabu kilichonishangaza ni kwamba Mji huu kwenye mambo ya fursa upo kwa majirani zao Wachaga wa Moshi, niliweza kufanya uchunguzi kwenye mambo kama hotel nyingi sana za Wachaga, Kampuni nyingi za utalii za Wachaga, biashara nyingi hapo mjini za Wachaga mpaka siasa hao kina Lema ni Wachaga.

Mbeya Mjini - wazawa asili wa hili eneo ni kabila la Wasafwa, Kwa bahati mbaya kabila hili machifu walikuwa na itikadi za kuzuia kuchanganyikana na wageni kwa kuamini ni kulinda tamaduni zao, matokeo yake wageni walipoanza kuja Wasafwa wanasogea pembeni, mema ya mji kuanzia Elimu, Biashara, Kazi, Siasa, n.k. wanufaika wakawa ni kabila la wilaya jirani ya Tukutu kwa Wanyakyusa, kwa sasa Wakinga ndio wameshikilia zaidi biashara, Ila kwa siku hizi angalau zile fikra za machifu zimeanza kufutika nao Wasafwa tunajimix nao.
 
Kwa Arusha sidhani kama ni kweli kwa sehemu kubwa

Wachaga wana mafanikio kila mahali nchi hii hata Arusha...lakini kwa Arusha kuna kampuni nyingi sana za Utalii na Madini yanayomililiwa na Wenyeji Waarusha na Wameru pia

Kwa Biashara ni kweli ukitoa Biashara ya kuuza nyama (Butchery) na Nafaka inayomilikiwa na Waarusha, Biashara zingine nyingi kubwa hasa za kuimport bidhaa ni za Wahindi na Wachaga
 
Kuna kabila linaitwa waarusha?

Asili ya hili kabila ni ipi? Nna mashaka sana hili kabila halipo ni watu wamekua wavivu tuu kufikiria

Nnachojua Arusha ina makabila mawili

Wamasai
Wameru
 
Kwa dar je..
Ungefanya utafit vizuri kwa arusha kwa biashara ya uchuuzi uenda kuna usawa kwani kina laizer, nyari, massawe, mollel, unafikir hao ni wageni wanamiliki biashara kubwa tu za madini...
Ukienda Kilimanjaro utaona pia kuna wageni ndio wanaishi mjini wenjeji wachache...
Kwa ujumla ni ngumu kutoboa eneo unalokulia kuna vikwazo vingi kwa watu wanaokuzunguka
 
Kuna kabila linaitwa waarusha?

Asili ya hili kabila ni ipi? Nna mashaka sana hili kabila halipo ni watu wamekua wavivu tuu kufikiria

Nnachojua Arusha ina makabila mawili

Wamasai
Wameru
Waarusha ni wamasai advanced
Hilo swali nilijiuliza kwa miaka kadhaa

Ila kabila la Waarusha lipo, Kwanza neno ARUSHA limetokana na neno LARUSA ambao ni Ukoo uliopo Kibosho mpaka hivi

Pia kuna Waarusha wengi ambao kiasili ni Wakibosho na sio Wamasai, hasa Sanawari mpaka Mianzini waliokuwa wanafanya biashara ya ngozi kisha Bucha tangu kama karne 1 au 2 zilizopita, japo Wamasai pia wapo

Ukienda ARUSHA BOMA pale nyuma ya jengo la Mkuu wa Mkoa utapata historia zote kiundani na picha pamoja na maandishi
 
Kwanza hamna kabila linaitwa waarusha!

Dar es salaam pia wenyeji wake wamekimbia na kiwaachia fursa watukuja, wanadaslam wapo bize na Nyerere kawasnitch
 
Kwanza hamna kabila linaitwa waarusha!

Dar es salaam pia wenyeji wake wamekimbia na kiwaachia fursa watukuja, wanadaslam wapo bize na Nyerere kawasnitch
Kwenye vitabu vyenu ni kweli hamna Wa Arusha.. ila ukienda Arusha, Wa Arusha wapo!
 
Kwa dar je..
Ungefanya utafit vizuri kwa arusha kwa biashara ya uchuuzi uenda kuna usawa kwani kina laizer, nyari, massawe, mollel, unafikir hao ni wageni wanamiliki biashara kubwa tu za madini...
Ukienda Kilimanjaro utaona pia kuna wageni ndio wanaishi mjini wenjeji wachache...
Kwa ujumla ni ngumu kutoboa eneo unalokulia kuna vikwazo vingi kwa watu wanaokuzunguka

Kwamba moshi mjini wenyeji(Wachagga ) ni wachache?
Itakuwa hujawahi kufika Moshi.
 
Hilo swali nilijiuliza kwa miaka kadhaa

Ila kabila la Waarusha lipo, Kwanza neno ARUSHA limetokana na neno LARUSA ambao ni Ukoo uliopo Kibosho mpaka hivi

Pia kuna Waarusha wengi ambao kiasili ni Wakibosho na sio Wamasai, hasa Sanawari mpaka Mianzini waliokuwa wanafanya biashara ya ngozi kisha Bucha tangu kama karne 1 au 2 zilizopita, japo Wamasai pia wapo

Ukienda pale ARUSHA BOMA utapata historia zote kiundani na picha pamoja na maandishi
Asili ya jina Arusha ni neno la kimasai lenye maana ya eneo linalotoa maji , au mahali pa kijani.
 
Arusha Mjini - wazawa asili Kuna Wameru na Waarusha, niliwahi kuishi hapo miaka mitano, cha ajabu kilichonishangaza ni kwamba Mji huu kwenye mambo ya fursa upo kwa majirani zao Wachaga wa Moshi, niliweza kufanya uchunguzi kwenye mambo kama hotel nyingi sana za Wachaga, Kampuni nyingi za utalii za Wachaga, biashara nyingi hapo mjini za Wachaga mpaka siasa hao kina Lema ni Wachaga.

Mbeya Mjini - wazawa asili wa hili eneo ni kabila la Wasafwa, Kwa bahati mbaya kabila hili machifu walikuwa na itikadi za kuzuia kuchanganyikana na wageni kwa kuamini ni kulinda tamaduni zao, matokeo yake wageni walipoanza kuja Wasafwa wanasogea pembeni, mema ya mji kuanzia Elimu, Biashara, Kazi, Siasa, n.k. wanufaika wakawa ni kabila la wilaya jirani ya Tukutu kwa Wanyakyusa, kwa sasa Wakinga ndio wameshikilia zaidi biashara, Ila kwa siku hizi angalau zile fikra za machifu zimeanza kufutika nao Wasafwa tunajimix nao.
Vijana Bukoba Mjini, fursa nyingi wameachiwa Majirani.
 
Kuna kabila linaitwa waarusha?

Asili ya hili kabila ni ipi? Nna mashaka sana hili kabila halipo ni watu wamekua wavivu tuu kufikiria

Nnachojua Arusha ina makabila mawili

Wamasai
Wameru
Kwa taarifa yako kiasili wameru sio kabila. Ila nao ni wachaga wa meru japo meru ipo arusha..
Ni kama ilivyo kwa (wakibosho, wamarangu, wamachame, wauru, wameru n.k) hawa wote ni wachaga ..

Waarusha ni kabila la vizalia.... Ni mchanganyiko wa wachaga (wameru)+ wamasai... Hao ndio wachuga sasaa
 
Miaka ya nyuma wasafwa wao walikuwa wanakaa milimani tu
Walikuwa hawajichanganyi mijini
Ulikuwa ukienda na gari milimani
Huko wakiona gari wanakimbia wanajuwa mmekuja kuwadhuru
Ila walikuwa watu fulani wanyenyekevu sana

Ova
 
Back
Top Bottom