Njia 10 za Uchumba Salama

Njia 10 za Uchumba Salama

kwa nini na wewe usiandike uzi wako alafu unyooshe icho kiswahili chako..... sisi tunaelewa acha maneno πŸ˜¬πŸ˜¬πŸ˜¬πŸ˜¬πŸ˜¬πŸ‘†
Tulia dawa ikuingie..πŸ˜‚πŸ˜œ
 
kwa nini na wewe usiandike uzi wako alafu unyooshe icho kiswahili chako..... sisi tunaelewa acha maneno [emoji51][emoji51][emoji51][emoji51][emoji51][emoji115]
Bora useme wewe mkuu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Halafu kiswahili chenyewe kimenyooka tu,yeye anataka kukipindisha
 
Hongera sana, mengi uliyoyaandika pia ni maagizo kutoka kwa Mungu muumba wetu

Ila kwakweli kwa kizazi hiki cha sasa utapingwa na si bure hata kutukanwa.

''Avumiliaye mpaka mwisho atapata taji''

''Lisilowezekana kwa Binadamu kwa Mungu linawezekana'' hata kuishi bila Uzinzi pia inawezekana ukiwa na Mungu.
 
Hongera sana, mengi uliyoyaandika pia ni maagizo kutoka kwa Mungu muumba wetu

Ila kwakweli kwa kizazi hiki cha sasa utapingwa na si bure hata kutukanwa.

''Avumiliaye mpaka mwisho atapata taji''

''Lisilowezekana kwa Binadamu kwa Mungu linawezekana'' hata kuishi bila Uzinzi pia inawezekana ukiwa na Mungu.
Amen[emoji4][emoji120][emoji120]
Akhsante kwa kunitia moyo

Ubarikiwe
 
Habari!

Natumaini wote ni wazima na namshukuru Mungu juu ya kila mmoja wetu. Natamani kushare nanyi mambo haya machache muhimu katika Uchumba:

1. Usiweke agano na mchumba.
Kuna Watu huwa wanajiapiza eti nisipokuoa/nisipoolewa na wewe bora nife kuliko kuoa/kuolewa.
Maagano ya namna hii yamewagharimu wengi.

Maandiko yanatambua agano la ndoa na si la uchumba.Acha mpango wa Mungu usimame kwenye uchumba wenu.

2. Usizae na mchumba ili akuoe.
Hii huwakumba Sana wadada.Wengi huingia kwenye huu mtego kwa kudanganywa na kuambiwa nizalie kwanza mtoto ndipo nikuoe.

Pia, kuna wadada hujitegesha. Kuna wadada hujitegesha wenyewe wapate mimba wakidhani watapendwa zaidi.
Wengi wamezalishwa na kutelekezwa.

3.Usioe/kuolewa na mtu asiyemcha Mungu.
Moyo wa mtu asiyemcha Mungu hauna hofu ya kitu chochote ndani yake.kufanya Jambo lolote kwako siyo tatizo kwake maana moyoni mwake hakuna hukumu.

4. Usikubali kuoa/kuolewa na mtu aliyekuwa kwenye ndoa tayari na ndoa ile ikavunjika na wewe ukataka kuingia naye kwenye ndoa bila kujua sababu za ndoa yake ya mwanzo kuvunjika.

Ni vema ukajua sababu kupitia kutafuta taarifa kwa watu wengine na si kwake maana atakudanganya.

5. Uchumba usiwe Siri.
Unaweza kujikuta unaoa/unaolewa na mume au mke wa mtu bila kujua.

6. Usioe au kuolewa na mtu kwa sababu unamhurumia.
Ni kweli kaonyesha upendo,Ni kweli anakujali lakini je!huyo mtu yumo moyoni mwako?unampenda? Au unajilazimisha kwa sababu ya zawadi anazokupa.

Ndoa nzuri ni ile ya watu wawili wanapendana na si ya upande mmoja.

7. Msichukuane kienyeji.
Ndoa Ina taratibu zake na taratibu hizo Zina baraka zake. Usijiweke kwenye mazingira ya kuibiwa usiku.

8. Acha kujiaminisha Sana kwamba utamuoa au utaolewa naye.
Kumbuka uchumba siyo ndoa.Lolote linaweza kutokea Kama siyo upande wako basi upande wake. Ruhusu mpango wa Mungu utimie na si utashi wako.

9. Epuka kumhonga mchumba vitu vya thamani kubwa, kumsomesha nk.
Usiwekeze Sana kwa mchumba. Lakini Kama unadhani uchumba ujivunjika hutaumia mpe,ila Kama unaona uchumba ukivunjika utaumia usimpe.

Simaanishi wachumba wasisaidiane,Kuna viwango vya kusaidiana wachumba. Mengine hayo ukitaka kuyafanya weka ndani.

10. Usizini.
Tendo la ndoa ni kwa wanandoa na ndiyo maana linaitwa tendo la ndoa na si tendo la uchumba. Ukiona mchumba anataka tendo Hili kwa Kasi kubwa huku akikwambia siwezi kuuziwa mbuzi kwenye gunia jua huyo hana mpango wa ndoa.

Niwatakie siku njema
Hapo namba 10 mkuu, umekosea sana!
 
Back
Top Bottom