Njia ni Nyembamba na Mlango ni Mwembamba, Waingiao ni wachache (Spirit Science)

Njia ni Nyembamba na Mlango ni Mwembamba, Waingiao ni wachache (Spirit Science)

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,887
Nawasalimia wana JF wote. Huu nimwendelezo wa kujifunza Science ya kiroho na namna ya kujitambua.

Leo nitaongelea jinsi gani ilivyo vigumu kujitambua na kujua wewe asili yako ni nini. Jambo gumu kuliko mambo yote ni namna ya kujitambua. Inahitaji bidii na nia ya dhati ndipo utakapoanza kusonga mbele na kujua wewe umetoka wapi.

Nitaanza kueleza kwa ushuhuda wangu binafsi. Kwamba nilikuwa na nia sana ya kutambua hivi sisi binadamu ni kitu gani? Asili yetu ni nini? na tumetoka wapi? Na lengo letu hapa duniani ni nini?
Nilikuwa na maswali mengi sana pasipo na majibu. Nimekuwa sasa nikijifunza na kutafuta ukweli pasipokuwa na akili iliyofungwa. Nilianza kupata masomo ya kujitambua kupitia meditation. Kwa kweli inahitaji bidii ya hali ya juu ili kuweza kusonga mbele.

Siku moja nilikuwa nimejilaza kwenye kitanda (Baada ya kuanza kujifunza Out of Body Experience). Ghafla nikawa naisi mwili wangu unakufa ganzi (Nilikuwa na hofu sana, lakini nikajipa moyo ngoja nione kitu gani kitatokea). Baada ya muda, wakati nimetulia nikaanza kuhisi nwili wangu kama unabebwa. Nikawa na uwezo wa kupaa, nilitoka nje na kuangalia huku na huku. Mara nikarudi ndani. Nilipo rudi nikakuta kunamtu anafanana na mimi kajilaza kitandani. Ha niakaanza kuuliza wewe nani? Mtu huyo alikuwa kimya tu. Kwa kukata stori hiyo baada ya muda nikarudi katika hali ya kawaida. Nilikuwa nimelala hapo hapo.

Baada ya kupata somo kuwa huo mwili ilikuwa ni mwili wangu na mimi nilikuwa katika ulimwengu wa kiroho. Nilifurahi sana kuona kwamba ninaweza kufanya jambo hilo.

Siku nyingine tena nikiwa najifunza. Nilikuwa nimelala na gafla usingizi ukawa umepotea. Nikasema ngoja nifanye OBE. Nikawa nimejilaza kitandani mda kama dakika 40. Nikaanza kuhizi mwili wangu unakufa gazi. Kuanzia kwenye miguu hadi kwenye kichwa. Nilikaa katika hali hiyo kama baada ya saa moja hivi. Baadaye nikaamua nibadilishe namna ya kulala. Nili lala kifudi fudi(Yaani tumbo chini ya kitanda). Nilitulia tena baada ya muda mwili ukaanza kufa ganzi. Nikaendelea kujituliza. Baadaye nikahisi mwili wangu unatetemeka. Nikaangalia pembeni nikajiona. Kisha nikaamua kwenda ninakotaka. Hakika niliondoka nilikuwa na uwezo wa hali ya juu. Kila ninakotaka kwenda niliweza. Nilikutana na viumbe tofauti tofauti na watu wa aina tofauti.

Ninapenda kueleza kwamba jambo hili si rahisi linahitaji uthubutu na kuondoa woga maana unawasiliana na nafsi yako mwenyewe. Watu wengine wanataka kufanya siku moja na kuona matokeo. Inahitaji bidii. Ukishaanza kuendelea utaanza kugundua vitu vingi sana. Utajitambua kuwa wewe ni nani hasa. Utaelewa na utakuwa huru. Utumwa wa fikra utaanza kupotea na utaanza kuwa na maamuzi sahihi.

Ni wachachetu wala si wengi watakao elewa na kufuatilia ninachoongelea. Kukata tamaa na uvivu, umewakumba watu walio wengi. Lakini wale wenye kuthubutu hakika wataelewa. Ni faida ya mtu binafsi si kwaajili ya kikundi au ukoo. Ni jitihada ya mtu mwenyewe. Kuangaziwa nuru na kuondoka kwenye ufungwa ni hatua muhimu sana kwa kipindi hiki.

Chukua hatua ya kuanza kujitambua. Ukiwa na nia na matamanio, mwalimu atakuja kukutafuta na hakika utajifunza. Mwalimu yupo kila wakati anahitaji mwanafunzi.

By Annael.
The Spirit Science Teaching And Self Reality.
 
Hicho kitu ni hatari, nijuavyo mie na kupitia movies mtu akishanyanyua nafsi vile ule mwili hautakiwi kugeuzwa, ukijigeuza tu unarudisha jezi kwa muumba, sasa we uliwezaje kugeuka na kurudisha nafsi?
si ndo hivo wataalamu? mshana jr Rakims
 
Last edited by a moderator:
Hicho kitu ni hatari, nijuavyo mie na kupitia movies mtu akishanyanyua nafsi vile ule mwili hautakiwi kugeuzwa, ukijigeuza tu unarudisha jezi kwa muumba, sasa we uliwezaje kugeuka na kurudisha nafsi?
si ndo hivo wataalamu? mshana jr Rakims
Ndugu yangu ni kuogopesana tu. Hakuna cha kufa wala nini. Mimi uwa ninafanya mara kwa mara mbona nipo tu hai!!. Woga ndio unaowafanya watu wasindwe. Inatakiwa uanze hatua kwa hatua na kitu kikubwa ni kujifunza taratibu na kuelewa.

Kitu kinacho wachanganya watu baada ya kuona kuna mtu mwingine. Lakini kama umeshaelezwa hakika hautaogopa. Utakapokuwa kwenye ulimwengu wa roho kitu kikubwa ni kujiamini basi. Hakuna kitu chochote kitakacho kuathili.
 
Which spiritual side are You?Jesus Christ or Satanic?

This is what the world of today hates. You are told about you "I" halafu unakuja na story za Yesu na shetani. By the way Jesus is not the reverse of Satan, neither satan is.

If you want you can be a saint. If you want you can google what is a saint? Someni kila wakati.
 
Wewe ni mchawi tu kama wengine duniani. Hayo ni mafundisho ya ulimwengu wa kichawi yaliyozagaa hata mitandaoni.
 
Twend Pole Pol Annael Somo Zur Umesema Ukiwa Tayar Mwalim Atakutafuta Hap Umemaanish Nin Mfan Mim Niko Bush Mwalm Atatokeaj Na Utafahamuj Kuw Huy Ananifundsh Kit Sahh Coz Hat Wachawa Wanatoka Nje Ya Mwli, Na Unaonaj Kama Mtu Akianza Na Hatua Za Awal Za Meditation Ambaz Hujazizungumzia Ili Tunaanza Tusianze Kuogpa Kufa Ganz Usingizin Wakat Hat Ku Concetrate T Katka Medtation Tnaogap ,
 
Ndugu yangu ni kuogopesana tu. Hakuna cha kufa wala nini. Mimi uwa ninafanya mara kwa mara mbona nipo tu hai!!. Woga ndio unaowafanya watu wasindwe. Inatakiwa uanze hatua kwa hatua na kitu kikubwa ni kujifunza taratibu na kuelewa.

Kitu kinacho wachanganya watu baada ya kuona kuna mtu mwingine. Lakini kama umeshaelezwa hakika hautaogopa. Utakapokuwa kwenye ulimwengu wa roho kitu kikubwa ni kujiamini basi. Hakuna kitu chochote kitakacho kuathili.
Hiyo hali ya kuupoozesha mwili inahusisha ubongo si ndio? Sasa ukishtuka na kugeuza mwili kwani unabaki umepooza vile vile?
 
Nafikiri somo linauhusu meditation na sio kujitambua.

Halafu heading na contents kuna walakini.
 
Hiyo hali ya kuupoozesha mwili inahusisha ubongo si ndio? Sasa ukishtuka na kugeuza mwili kwani unabaki umepooza vile vile?
Kuna connection kati ya mwili na ulimwengu wa roho. Kwa hiyo hali hiyo ikiwa inatokea ubongo utakuwa umeuandaa mwili katika hali ya kutulia. Huwezi ukapooza kamwe na kitu hiki ni kizuri sana itakapogundua kuwa kumbe inawezekana hata kwenda sehemu tofauti tofauti ulimwenguni katika ulimwengu wa roho.

Hii elimu imefichwa na wengi hawataki wengine waijue. Usiogope, chukua hutua, haukuna kitu kibaya chochote, mtu awe yeyote asikutishe maana unawasiliana na nafsi/roho yako (God is within you)
 
Nafikiri somo linauhusu meditation na sio kujitambua.

Halafu heading na contents kuna walakini.
Ila kitu kimoja ningependa uelewe. Meditation lengo lake ni kuelekea kujitambua. Halafu kichwa cha habari kinaongelea ni nanmna gani ilivyo vigumu kuweza kufikia level ya kujua wewe ni nani. Na niwachache tu wenye nia thabiti wanapita katika mlango wa Spiritual Reality.
 
Ila kitu kimoja ningependa uelewe. Meditation lengo lake ni kuelekea kujitambua. Halafu kichwa cha habari kinaongelea ni nanmna gani ilivyo vigumu kuweza kufikia level ya kujua wewe ni nani. Na niwachache tu wenye nia thabiti wanapita katika mlango wa Spiritual Reality.

Labda Mimi sijjtambui ndo maana.sijaelewa mpaka sasa hahahah.
 
Which spiritual side are You?Jesus Christ or Satanic?

Nice question...kwa sababu anachokisema hakihusiani kabisa na meditation, isipokuwa ni ndoto tu ya kuota unapaa ambapo ni ishara ya kufuatwa na washirikina au mapepo...
 
Nawasalimia wana JF wote. Huu nimwendelezo wa kujifunza Science ya kiroho na namna ya kujitambua.

Leo nitaongelea jinsi gani ilivyo vigumu kujitambua na kujua wewe asili yako ni nini. Jambo gumu kuliko mambo yote ni namna ya kujitambua. Inahitaji bidii na nia ya dhati ndipo utakapoanza kusonga mbele na kujua wewe umetoka wapi.

Nitaanza kueleza kwa ushuhuda wangu binafsi. Kwamba nilikuwa na nia sana ya kutambua hivi sisi binadamu ni kitu gani? Asili yetu ni nini? na tumetoka wapi? Na lengo letu hapa duniani ni nini?
Nilikuwa na maswali mengi sana pasipo na majibu. Nimekuwa sasa nikijifunza na kutafuta ukweli pasipokuwa na akili iliyofungwa. Nilianza kupata masomo ya kujitambua kupitia meditation. Kwa kweli inahitaji bidii ya hali ya juu ili kuweza kusonga mbele.

Siku moja nilikuwa nimejilaza kwenye kitanda (Baada ya kuanza kujifunza Out of Body Experience). Ghafla nikawa naisi mwili wangu unakufa ganzi (Nilikuwa na hofu sana, lakini nikajipa moyo ngoja nione kitu gani kitatokea). Baada ya muda, wakati nimetulia nikaanza kuhisi nwili wangu kama unabebwa. Nikawa na uwezo wa kupaa, nilitoka nje na kuangalia huku na huku. Mara nikarudi ndani. Nilipo rudi nikakuta kunamtu anafanana na mimi kajilaza kitandani. Ha niakaanza kuuliza wewe nani? Mtu huyo alikuwa kimya tu. Kwa kukata stori hiyo baada ya muda nikarudi katika hali ya kawaida. Nilikuwa nimelala hapo hapo.

Baada ya kupata somo kuwa huo mwili ilikuwa ni mwili wangu na mimi nilikuwa katika ulimwengu wa kiroho. Nilifurahi sana kuona kwamba ninaweza kufanya jambo hilo.

Siku nyingine tena nikiwa najifunza. Nilikuwa nimelala na gafla usingizi ukawa umepotea. Nikasema ngoja nifanye OBE. Nikawa nimejilaza kitandani mda kama dakika 40. Nikaanza kuhizi mwili wangu unakufa gazi. Kuanzia kwenye miguu hadi kwenye kichwa. Nilikaa katika hali hiyo kama baada ya saa moja hivi. Baadaye nikaamua nibadilishe namna ya kulala. Nili lala kifudi fudi(Yaani tumbo chini ya kitanda). Nilitulia tena baada ya muda mwili ukaanza kufa ganzi. Nikaendelea kujituliza. Baadaye nikahisi mwili wangu unatetemeka. Nikaangalia pembeni nikajiona. Kisha nikaamua kwenda ninakotaka. Hakika niliondoka nilikuwa na uwezo wa hali ya juu. Kila ninakotaka kwenda niliweza. Nilikutana na viumbe tofauti tofauti na watu wa aina tofauti.

Ninapenda kueleza kwamba jambo hili si rahisi linahitaji uthubutu na kuondoa woga maana unawasiliana na nafsi yako mwenyewe. Watu wengine wanataka kufanya siku moja na kuona matokeo. Inahitaji bidii. Ukishaanza kuendelea utaanza kugundua vitu vingi sana. Utajitambua kuwa wewe ni nani hasa. Utaelewa na utakuwa huru. Utumwa wa fikra utaanza kupotea na utaanza kuwa na maamuzi sahihi.

Ni wachachetu wala si wengi watakao elewa na kufuatilia ninachoongelea. Kukata tamaa na uvivu, umewakumba watu walio wengi. Lakini wale wenye kuthubutu hakika wataelewa. Ni faida ya mtu binafsi si kwaajili ya kikundi au ukoo. Ni jitihada ya mtu mwenyewe. Kuangaziwa nuru na kuondoka kwenye ufungwa ni hatua muhimu sana kwa kipindi hiki.

Chukua hatua ya kuanza kujitambua. Ukiwa na nia na matamanio, mwalimu atakuja kukutafuta na hakika utajifunza. Mwalimu yupo kila wakati anahitaji mwanafunzi.

By Annael.
The Spirit Science Teaching And Self Reality.

I have advanced degree in Metaphysics and study of meditation and human chakral points. Unachoeleza hapa ni ndoto ya kawaida kabisa ambayo inahusiana na kunyemelewa na washirikina na au mapepo unapokuwa usingizini hasa usiku.....it has totally no relation to what you are trying to lie.

Na hata katika kuexperience out of body hata kama you are used to it si rahisi kiasi hicho. It takes a lot of time inclusing conditioning your body sometimes through fasting......and when you start the process si kitu cha kuingia kirahisirahisi kama unavyodanganya hapa.
 
I have advanced degree in Metaphysics and study of meditation and human chakral points. Unachoeleza hapa ni ndoto ya kawaida kabisa ambayo inahusiana na kunyemelewa na washirikina na au mapepo unapokuwa usingizini hasa usiku.....it has totally no relation to what you are trying to lie.

Na hata katika kuexperience out of body hata kama you are used to it si rahisi kiasi hicho. It takes a lot of time inclusing conditioning your body sometimes through fasting......and when you start the process si kitu cha kuingia kirahisirahisi kama unavyodanganya hapa.
Tatizo lako umesoma na hujawahi kufanyia kazi. Na ndio maana nimesema kuwa si rahisi na inahitaji bidii. Halafu unaposema una degree ya Metaphysics na Meditation una maanisha nini? Meditation is not all about learning its about practice.

Ungekuwa unajua Relationship btw Lucid dreaming na OBE hapa tungekuwa tunaongea. Ona sasa umeanza kuleta imani za kichawi hapa.

Na pia usitishe watu, kama wewe ulishindwa waache wengine wajaribu, sio kuwakatisha tamaa kwa kusema umesomea hayo mambo.
 
Mara unakuwa unawasiliana na nafsi yako katika ulimwengu wa roho, hapo hapo unakuwa "god within you". Ulimwengu wa roho ni nini Annael, labda tuanzie hapo. Maana hayo ma NWO agenda yanakupoteza.
 
Last edited by a moderator:
Mara unakuwa unawasiliana na nafsi yako katika ulimwengu wa roho, hapo hapo unakuwa "god within you". Ulimwengu wa roho ni nini Annael, labda tuanzie hapo. Maana hayo ma NWO agenda yanakupoteza.
God is state consciousness level. Kama utakuja kufahamu kuwa God is within you and God is you. Ndipo utakaponielewa nina maanisha nini.

Uungu ni hali, sio kitu. Unaweza ukatumia nguvu yako ya uungu iliyomo ndani yako. Utakapo anza kuangaziwa na kuipata nuru ndipo utakapojua Mungu maana yake ni nini.
 
Back
Top Bottom