Njia za kufuata ili kuachana na unywaji wa Pombe na Ulevi uliopitiliza

kuacha pombe ni kitu kigumu sana ila kuna baadhi ya watu katika jamii wanafahamu namna ya kudhibiti tatizo hili mimi nilikuwa na mtu wangu wa karibu aliyesumbuliwa na tatizo hilo ila alivyopatiwa hiyo kitu aliacha kabisa siwezi kuuita dawa coz haipo katika mfumo wa dawa ila unaweza kuuita dawa coz inaweza kutibu hilo tatizo na muathirika wa ulevi akijaribu kurudia ata nusu glasi hutapika sana.
 
Unataka kuacha au kubadili POMBE ? Yaani unataka kuacha kali uwe unatumia nyepesi nyepesi. Ushauri wangu ni bora kuacha kabisa.
 
Heshima mbele wanajamvi..naomba msaada wa kimawazo kumsaidia mzee wetu ambaye amekuwa mtumwa wa pombe.Tatizo linalotukabili ni kuwa yeye hana utayari wa kuacha kiasi kwamba hataki kushirikiana na sisi in whatever ways za kumsaidia ikiwemo hizo dawa.Tumesha watumia wakubwa zake lakini he has been very furious akiambiwa.So naomba kujua kama kuna namna ya kumfanya aache bila yeye kujua.


Cc: Red Giant
 
Last edited by a moderator:
mkuu kuacha bila mwenyewe kuwa tayari ni ngumu sana. hata matumizi ya dawa inabidi nae awe tayari. na pia mtu akiwa mlevi sana inabidi kuacha chini ya uangalizi wa daktari vinginevyo anaweza kupata madhara. cha muhimu ni kujitahidi kumueleza kwamba hahitaji kuacha kabisa hata akipunguza itatosha.
 
Ni maamuzi tuu ya dhati kutoka moyoni pasipo kulazimishwa na mtu au na mazingira. Mi nilikua mlevi kupitiliza ila niliamka asubuhi moja hivi ambayo jana yake nililewa sana kiasi cha kugombana na mtu wangu wa karibu sana na kuanzia siku ile ckuthubutu kuonja pombe mpaka leo hii ni miaka mitatu sasa na hakuna aliyeamini nitaweza kuacha bz kwa kweli nilikua zaidi ya pampula, namshukuru Mungu.
 
Mitaa ya kko sokoni kwenye maduka ya vitu asilia kuna dawa ya kuchanganya na pombe unapewa unakunywa utatapika mpaka ukome siku nyingine ukiiona pombe ile harufu yake tu huwezi igusa unahisi kichefuchefu hapo ndo pombe kwako mwiko.
 
wengi nao wajua walioacha pombe wameacha kwa style zifuatazo moja, kuna jamaa yangu maeneo ya buguruni alikuwa analewa sana sasa siku moja akalewa mpaka akaangusha gari watoto wa buguruni wakamla tigo mpaka haja kubwa ikatoka kasha wakampiga picha jamaa aliacha pombe na kuhama mtaa pia kuna mwingine alikuwa mlevi sana siku moja akalewa ndugu zake wakamchukua wakampeleka mortuary wakaongea na yule mortuary attendant jamaa alilala mle ndani kuja kuzinduka jamaa akagundua amelala katikati ya maiti du jamaa akaacha pombe hadi hii leo ndio yuko jamii forums anajiita illegal migrant ndio anachangia hapa
 
Last edited by a moderator:
JE ULIKUWA UNATAMBUA KUWA ULEVI SUGU NI UGONJWA?

KWANZA KABISA ULEVI SUGU (ALCOHOLISM) NI NINI?

Shirika la Afya Duniani (W.H.O) lilithibitisha kuwa ulevi sugu kuwa ni ugonjwa sugu tangu mwaka 1949. Baada ya hapo ugonjwa huu umeendelea kusababisha vifo vya maelfu ya watu duniani. Hapa Tanzania pia watu wengi wameathirika na ugonjwa huu.
(Utafiti wa W.H.O umedhibitisha kuwa watu millioni 2 na nusu wanakufa kila mwaka kwa sababu ya unywaji wa pombe kupindukia)

MAGONJWA SUGU NI YAPI? Ni kama Ukimwi (HIV AIDS), DIABATES (KISUKALI), KANSA (CANCER), PRESSURE (MAGONJWA YA MOYO). Kumbuka magonjwa sugu ya hatua za (awali, kati na mwisho) kwa maana nyingine hauna TIBA.

HATUA YA KWANZA NI YEYE KUKUBALI KWAMBA ANA TATIZO NA YUKO TAYARI KUACHA YEYE MWENYEWE BILA SHINIKIZO LA MTU AU KITU CHOCHOTE.

Kwahiyo mi nakushauri mtafutie huyu jamaa yako umoja wa watu walioacha au wenye nia ya kuacha ULEVI SUGU uitwao:
Alcoholics Anonymous (A.A) ni ushirika wa wanaume na wanawake ambao wanashirikiana ujuzi, nguvu na matumaini kati yao ili waweze kutatua matatizo yao na kusaidia wengine kupona ulevi.

Sharti pekee la uanachama ni nia ya kuacha ulevi
. Hakuna ada ya kuwa mwanachama wa A.A, tunajitegemea wenyewe kwa michango yetu wenyewe. A.A haifungamani na madhehebu yoyote ya dini, siasa, shirika au taasisi na haitaki kujiingiza katika mabishano yoyote. Kadhalika A.A haiungi mkono wala kupinga chama chochote.
Nia yetu ya msingi ni kukaa bila kulewa na kuwasaidia walevi wengine kupona kutokana na ulevi.
A.A ni kwa ajili ya mlevi ambaye ana NIA YA KUACHA KUNYWA POMBE. Kama unadhani una tatizo la ulevi, unakaribishwa sana kuhudhuria vikao na mikutano.

Nakutakia mafanikio mema.

Usisite kuwasiliana nami ili nikupatie maelekezo zaidi: +255 789 780 529,
E-mail: rnelsontz@yahoo.com
 
ULEVI SUGU (ALCOHOLISM) NI NINI?

Shirika la Afya Duniani (W.H.O) lilithibitisha kuwa ulevi sugu kuwa ni ugonjwa sugu tangu mwaka 1949. Baada ya hapo ugonjwa huu umeendelea kusababisha vifo vya maelfu ya watu duniani. Hapa Tanzania pia watu wengi wameathirika na ugonjwa huu.
(Utafiti wa W.H.O umedhibitisha kuwa watu millioni 2 na nusu wanakufa kila mwaka kwa sababu ya unywaji wa pombe kupindukia)

MAGONJWA SUGU NI YAPI? Ni kama Ukimwi (HIV AIDS), DIABATES (KISUKALI), KANSA (CANCER), PRESSURE (MAGONJWA YA MOYO). Kumbuka magonjwa sugu ya hatua za (awali, kati na mwisho) kwa maana nyingine hauna TIBA.

HATUA YA KWANZA NI YEYE KUKUBALI KWAMBA ANA TATIZO NA YUKO TAYARI KUACHA YEYE MWENYEWE BILA SHINIKIZO LA MTU AU KITU CHOCHOTE.

Kwahiyo mi nakushauri mtafutie huyu jamaa yako umoja wa watu walioacha au wenye nia ya kuacha ULEVI SUGU uitwao:
Alcoholics Anonymous (A.A) ni ushirika wa wanaume na wanawake ambao wanashirikiana ujuzi, nguvu na matumaini kati yao ili waweze kutatua matatizo yao na kusaidia wengine kupona ulevi.

Sharti pekee la uanachama ni nia ya kuacha ulevi. Hakuna ada ya kuwa mwanachama wa A.A, tunajitegemea wenyewe kwa michango yetu wenyewe. A.A haifungamani na madhehebu yoyote ya dini, siasa, shirika au taasisi na haitaki kujiingiza katika mabishano yoyote. Kadhalika A.A haiungi mkono wala kupinga chama chochote.
Nia yetu ya msingi ni kukaa bila kulewa na kuwasaidia walevi wengine kupona kutokana na ulevi.
A.A ni kwa ajili ya mlevi ambaye ana NIA YA KUACHA KUNYWA POMBE.

Usisite kuwasiliana nami ili nikupatie maelekezo zaidi: +255 789 780 529,
E-mail: rnelsontz@yahoo.com

Nakutakia mafanikio mema.
 
WAZO ZURI,HII NI FURSA,LAKINI INABIDI TUWE KWANZA (beer) KWA SANA NA MAENEO YA KUKUTANA YAWE KI POMBE POMBE ZAIDI
 
ULEVI SUGU (ALCOHOLISM) NI NINI?

Shirika la Afya Duniani (W.H.O) lilithibitisha kuwa ulevi sugu kuwa ni ugonjwa sugu tangu mwaka 1949. Baada ya hapo ugonjwa huu umeendelea kusababisha vifo vya maelfu ya watu duniani. Hapa Tanzania pia watu wengi wameathirika na ugonjwa huu.
(Utafiti wa W.H.O umedhibitisha kuwa watu millioni 2 na nusu wanakufa kila mwaka kwa sababu ya unywaji wa pombe kupindukia)

MAGONJWA SUGU NI YAPI? Ni kama Ukimwi (HIV AIDS), DIABATES (KISUKALI), KANSA (CANCER), PRESSURE (MAGONJWA YA MOYO). Kumbuka magonjwa sugu ya hatua za (awali, kati na mwisho) kwa maana nyingine hauna TIBA.

HATUA YA KWANZA NI YEYE KUKUBALI KWAMBA ANA TATIZO NA YUKO TAYARI KUACHA YEYE MWENYEWE BILA SHINIKIZO LA MTU AU KITU CHOCHOTE.

Kwahiyo mi nakushauri utafute umoja wa watu walioacha au wenye nia ya kuacha ULEVI SUGU uitwao:

Alcoholics Anonymous (A.A) ni ushirika wa wanaume na wanawake ambao wanashirikiana ujuzi, nguvu na matumaini kati yao ili waweze kutatua matatizo yao na kusaidia wengine kupona ulevi.

Sharti pekee la uanachama ni nia ya kuacha ulevi. Hakuna ada ya kuwa mwanachama wa A.A, tunajitegemea wenyewe kwa michango yetu wenyewe. A.A haifungamani na madhehebu yoyote ya dini, siasa, shirika au taasisi na haitaki kujiingiza katika mabishano yoyote. Kadhalika A.A haiungi mkono wala kupinga chama chochote.
Nia yetu ya msingi ni kukaa bila kulewa na kuwasaidia walevi wengine kupona kutokana na ulevi.
A.A ni kwa ajili ya mlevi ambaye ana NIA YA KUACHA KUNYWA POMBE. Kama unadhani una tatizo la ulevi, unakaribishwa sana kuhudhuria mikutano.

Nakutakia mafanikio mema.

Usisite kuwasiliana nami ili nikupatie maelekezo zaidi: +255 789 780 529,
E-mail: rnelsontz@yahoo.com
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…