Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
1. Anza na panga siku yako vyema
Usikimbilie kuanza majuku yako ya siku bila kukaa chini na kutumia dakika chache za kutafakari mambo kadhaa.
Tafakari ni jambo gani muhimu zaidi ili uweze kulipa kipaumbele katika siku yako.
Jifunze kujiwekea malengo, haya yatakuwezesha kujua nini unachotakiwa kukitimiza ndani ya siku yako. Kwa njia hii utaweza kukamilisha vitu kulingana na muda uliojiwekea.
2. Gawanya kazi katika sehemu
Je uliwahi kusikia kanuni ya utawala wa wakoloni inayosema “gawanya na utawale”?
Hili pia lipo kwenye majukumu yako ya siku; unapogawanya kazi katika vipande vidogo vidogo ni rahisi kuzitawala na kuzifanya kwa wakati.
Kumbuka pia hata kazi ngumu huwa nyepesi kama itagawanywa katika sehemu ndogo ndogo kwani utaifanya kwa urahisi ndani ya muda uliopangwa vyema.
3. Weka vipaumbele
Jifunze kupanga kazi kulingana na vipaumbele vyake, usifanye kila kitu kwa sababu ni kazi bali fanya kwa kuongozwa na vipaumbele.
Jizoeze kusema “Hapana” kwa mambo, watu au kazi zisizokuwa na umuhimu. Ukifanya hivi utatumia muda wako vyema kwenye mambo ya muhimu kwanza.
Usikimbilie kuanza majuku yako ya siku bila kukaa chini na kutumia dakika chache za kutafakari mambo kadhaa.
Tafakari ni jambo gani muhimu zaidi ili uweze kulipa kipaumbele katika siku yako.
Jifunze kujiwekea malengo, haya yatakuwezesha kujua nini unachotakiwa kukitimiza ndani ya siku yako. Kwa njia hii utaweza kukamilisha vitu kulingana na muda uliojiwekea.
2. Gawanya kazi katika sehemu
Je uliwahi kusikia kanuni ya utawala wa wakoloni inayosema “gawanya na utawale”?
Hili pia lipo kwenye majukumu yako ya siku; unapogawanya kazi katika vipande vidogo vidogo ni rahisi kuzitawala na kuzifanya kwa wakati.
Kumbuka pia hata kazi ngumu huwa nyepesi kama itagawanywa katika sehemu ndogo ndogo kwani utaifanya kwa urahisi ndani ya muda uliopangwa vyema.
3. Weka vipaumbele
Jifunze kupanga kazi kulingana na vipaumbele vyake, usifanye kila kitu kwa sababu ni kazi bali fanya kwa kuongozwa na vipaumbele.
Jizoeze kusema “Hapana” kwa mambo, watu au kazi zisizokuwa na umuhimu. Ukifanya hivi utatumia muda wako vyema kwenye mambo ya muhimu kwanza.