Njia za kukusaidia kuweza kutumia muda vizuri

Njia za kukusaidia kuweza kutumia muda vizuri

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1. Anza na panga siku yako vyema
Usikimbilie kuanza majuku yako ya siku bila kukaa chini na kutumia dakika chache za kutafakari mambo kadhaa.

Tafakari ni jambo gani muhimu zaidi ili uweze kulipa kipaumbele katika siku yako.

Jifunze kujiwekea malengo, haya yatakuwezesha kujua nini unachotakiwa kukitimiza ndani ya siku yako. Kwa njia hii utaweza kukamilisha vitu kulingana na muda uliojiwekea.

2. Gawanya kazi katika sehemu
Je uliwahi kusikia kanuni ya utawala wa wakoloni inayosema “gawanya na utawale”?

Hili pia lipo kwenye majukumu yako ya siku; unapogawanya kazi katika vipande vidogo vidogo ni rahisi kuzitawala na kuzifanya kwa wakati.

Kumbuka pia hata kazi ngumu huwa nyepesi kama itagawanywa katika sehemu ndogo ndogo kwani utaifanya kwa urahisi ndani ya muda uliopangwa vyema.

3. Weka vipaumbele
Jifunze kupanga kazi kulingana na vipaumbele vyake, usifanye kila kitu kwa sababu ni kazi bali fanya kwa kuongozwa na vipaumbele.

Jizoeze kusema “Hapana” kwa mambo, watu au kazi zisizokuwa na umuhimu. Ukifanya hivi utatumia muda wako vyema kwenye mambo ya muhimu kwanza.
 
Unaamka asubuhi mara mtoto anaumwa, unaenda hospitali ya serikali huduma masaa 6..

No hurry in africa.
16316961954385397743496650409167.jpg
 
Pole chief.Katika harakat za kutafuta clients wa biashara yangu niko haoa namngoja manager masaa mawil sasa na nilipewa appointment toka last week na jana nikakumbushia .
No hurry in africa
Ukiwa smart sana katika kufuata muda barani la africa utagombana na watu wote. Kuanzia wazazi wako na jamii inayokuzunguka.
 
Na sisi ambao tupotupo tu hii thread inatuhusu?

Maana tuna muda wa kutosha hata tukiona watu wamejazana sehemu na sisi hujazana hapohapo tushuhudie kuna nini!!
 
Na sisi ambao tupotupo tu hii thread inatuhusu?

Maana tuna muda wa kutosha hata tukiona watu wamejazana sehemu na sisi hujazana hapohapo tushuhudie kuna nini!!
Nyie mshatoboa kimaisha tayar so tupen tu uzoefu
 
Ukiwa smart sana katika kufuata muda barani la africa utagombana na watu wote. Kuanzia wazazi wako na jamii inayokuzunguka.
Kwakifup sio rahis.Inabid ukubali tu matokea ila jitahid wasiku transform kuwa kama wao.How?? Plan less in ur day but strive to achieve more.
 
Kwakifup sio rahis.Inabid ukubali tu matokea ila jitahid wasiku transform kuwa kama wao.How?? Plan less in ur day but strive to achieve more.
Mwafrika ni mtu mwepesi sana kuvunja appointment tena haombi msamaha

mwafrika ni mwepesi sana kupotezea mtu mwingine muda tena haombi msamaha

anaweza kukuita mahali mkutane ukafika halafu yeye asifike na simu asipokee na akakutafuta kesho yake bila aibu
 
Back
Top Bottom