Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe linamshikilia mtoto wa umri wa miaka (12) kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wa darasa la nne (10) katika shule moja iliyopo Makambako mkoani Njombe.
Hayo yamebainishwa leo Aprili 13, 2024 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Mahamoud Banga zungumza na waandishi wa habari mkoani hapa.
Amesema tukio hilo lilitokea Aprili 4, 2024 Mtaa wa Jeshini mjini Makambako.
Amesema mwanafunzi huyo alikuwa akilawitiwa kwa ahadi ya kupewa fedha na mtuhumiwa huyo ambaye aliacha shule akiwa darasa la sita.
"Mtuhumiwa huyu anaonekana aliacha shule akiwa darasa la sita lakini amekuwa akimfanyia hivi vitendo kwa muda mrefu kwa ahadi ya kumpatia fedha," amesema Banga.
Amesema kwa muda wote huo mwanafunzi huyo hakusema kwa wazazi lakini tabia yake ilianza kubadilika baada ya kuwa anatokwa na haja kubwa na baada ya mama yake kumwadhibu, ndipo alisema kuwa anafanyiwa vitendo hivyo.
Ongezeko la matukio ya ulawiti hapa nchini Tanzania ni tatizo linalozidi kuongezeka, hususan kutokana na kuibuka kwa matikio yanayohusisha watoto, hali hii inaleta wasiwasi kwa jamii na kuathiri maendeleo ya kijamii na ustawi wa watoto.
Hii ni aina ya unyanyasaji wa kijinsia ambao unahusisha kutumia nguvu au ulaghai, na ni matukio yanayokandamiza haki za binadamu na kusababisha madhara makubwa kisaikolojia, kimwili na kijamii kwa wahusika, hususan watoto.
Mwananchi
Hayo yamebainishwa leo Aprili 13, 2024 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Mahamoud Banga zungumza na waandishi wa habari mkoani hapa.
Amesema tukio hilo lilitokea Aprili 4, 2024 Mtaa wa Jeshini mjini Makambako.
Amesema mwanafunzi huyo alikuwa akilawitiwa kwa ahadi ya kupewa fedha na mtuhumiwa huyo ambaye aliacha shule akiwa darasa la sita.
"Mtuhumiwa huyu anaonekana aliacha shule akiwa darasa la sita lakini amekuwa akimfanyia hivi vitendo kwa muda mrefu kwa ahadi ya kumpatia fedha," amesema Banga.
Amesema kwa muda wote huo mwanafunzi huyo hakusema kwa wazazi lakini tabia yake ilianza kubadilika baada ya kuwa anatokwa na haja kubwa na baada ya mama yake kumwadhibu, ndipo alisema kuwa anafanyiwa vitendo hivyo.
Ongezeko la matukio ya ulawiti hapa nchini Tanzania ni tatizo linalozidi kuongezeka, hususan kutokana na kuibuka kwa matikio yanayohusisha watoto, hali hii inaleta wasiwasi kwa jamii na kuathiri maendeleo ya kijamii na ustawi wa watoto.
Hii ni aina ya unyanyasaji wa kijinsia ambao unahusisha kutumia nguvu au ulaghai, na ni matukio yanayokandamiza haki za binadamu na kusababisha madhara makubwa kisaikolojia, kimwili na kijamii kwa wahusika, hususan watoto.
Mwananchi