Njombe: Wawili wauawa na mganga wa kienyeji na kutupwa msituni

Njombe: Wawili wauawa na mganga wa kienyeji na kutupwa msituni

Watu wawili, Suzana mtitu(38) na Kassim Kitamkanga(35)wakazi wa Makambako Mkoani Njombe wamekutwa wamefariki katika msitu wa Tanwat uliopo Njombe huku uchunguzi ukibainisha kuwa wameuawa na mganga wa jadi baaya ya wateja hao kugundua kuwa dawa za kuwa matajiri walizopewa hazijafanya kazi.

RPC wa Njombe Hamis Issah amesema jeshi la Polis linamshikilia mganga huyo wa huyo Kienyeji, Joseph Mgunda(41)mkazi wa Sovi kata ya Mtwngo Wilayani Njombe kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.

"Watu wengi wafanyabiashara huyu mganga anawaambia ukipeleka hela anaziombea halafu baadaye zinaongezeka, sintofahamu iliyotokea kwa hawa watu wawili walipewa walipewa dawa tayari lakini wakaona matokeo hayaleti mafanikio wakaenda kumuuliza mganga mbona umetupa dawa ambayo haisaidii, mganga huyo alishikwa na hofu na kushauriwa na ndugu zake kutekeleza mauaji hayo"

"Ndugu zake wakamwambia ukitaka usipate shida wauwe hawa watu na kweli watu watatu na yeye mwenyewe mganga akiwa ni wanne wakatekeleza mauwaji. Mwanaume alikatwa mapanga sehemu za shavuni upande wa kulia na kushoto na kichwanina pia kapigwa rungu na kudondoka na mwanamke alipigwa rungu moja tu na kudondoka chini"

Kamanda Issah amesema watu wengine wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauwaji hayo ni Andrew Vahuruka, Gadi Mwanzalila9(36) na Kelvin Kilinge(29), Kamanda Issah ametoa wito kwa wananchi kutafuta pesa kwa juhudi za kufanya kazi na si kutafuta utajiri kwa waganga kwa kuwa utajiri unaoletwa na waganga.
kwasababu yeye ni tapeli, angesepa tu kuliko kutoa roho zao tena. too bad. lkn, mshahara wa dhambini mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele. hasara ninayoiona hapo ni watu wawili kufa bila Mungu na kuelekea motoni moja kwa moja, hiyo ndio hasara kubwa kuliko hata kifo chenyewe. tulio hai tujitafakari na kujifunza toka kwao, haya maisha unaishi mara moja tu, na baada ya kifo ni hukumu. hata watu wakikuombea huku duniani ukishakufa kama hukumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, utaelekea moja kwa moja motoni ukaungue pamoja na shetani. hii ni kwasababu bila kupitia imani (ya neema) kwa Yesu Kristo, Mungu hakutambui, ni Yesu tu alimwaga damu kama ukombozi na njia ya kufuta dhambi za wanadamu. alifanyika kafara la dhambi zetu na ukombozi wetu, alilipa deni letu lote, ni sisi tu kwenda kwake kwa kutubu tukimaanisha kuacha dhambi ili atusamehe na tuishi maisha ndani yake, hapo ukifa unaenda mbinguni.
 
Wajinga ndio waliwao
Utaendaje kutafuta utajiri kwa maskini maana waganga wooooote ni maskini eti akupe wewe utajiri how? Kwa nini asijajirishe mwenyewe

Huyo mganga kifungo cha maisha na wenzake
Fanya harambeeee Mkuu wa polisi Mkuu wa Mkoa waganga wooooteeee wajisalimishe
Walokole wachungaji uchwara wasoma nyota wasoma mwezi woooooote kusanya wajulikane walipishwe faini waache kurubuni watu vinginevyo jela inawahusu....

Safisha uchafu wa kipumbavu
Tufanye kazi hakuna short cut
 
Wangesogea kule Makete kwa Mwakipande au kwa Meseketwa kupata utajiri.. Wao wameishia Njombe tu .
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sasa mganga, mchawi, mshirikina jumlisha chifu unaweza kutofautisha hapo? Hao wote idara moja ni vitengo tu

Sent using Jamii Forums mobile app
'Chief' si kiongozi wa kabila tu?... Au kwa sababu kuna mila ndio kunamfanya yeye mganga?

Ina maana kina Mirambo,Mkwawa, Isike,Abushiri hawa wote walikuwa waganga?
 
'Chief' si kiongozi wa kabila tu?... Au kwa sababu kuna mila ndio kunamfanya yeye mganga?

Ina maana kina Mirambo,Mkwawa, Isike,Abushiri hawa wote walikuwa waganga?
Hiyo chief unayo isema hapa sio, hao machifu tunawajua na kila kabila wapo ndiyo utawakuta kina mtemi, mwene majina yao hayo, sasa wewe kama huamini nenda kwa chifu wa Urwira - Katavi kisha urudi hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
This country...
Au ndo maendeleo yenyewe.

Kuuwana kama kuchinja kuku ndo ishakuwa norm sasa.!!?
 
Wakipeleka hela zinaombewa alafu zinaongezeka.
Wajinga ndio waliwao
 
Back
Top Bottom