Njoo tufanye biashara ya kununua korosho

Njoo tufanye biashara ya kununua korosho

Anaweza akawepo tajiri ambaye hana knowledge ambayo wewe unayo sasa ingekuwa vema kama ungeweka kabisa unataka mtaji wa kiasi gani na huyo mwekezaji anaweza akapata kiasi gani kwa pesa yake (au hasara kiasi gani)
 
Shida vyama havilipi on time mkuuu

Naangalia itv kila siku wanaanza akushukuru afu wanalia tunaombaa mtulipe kwa wakati

Na wengi wanassma wanalipwa wakati mwingjne .mda aa kupanda ushaisha

Kuwekeza mil 6 bila kuzunguka hili napo liangalie
Kwa uzoefu wangu mimi ambae huwa nanunulia korosho wilaya ya newala milion 6 unaweza kuizingusha mpaka mara 3
 
Ni biashara mzuri sana hasa ufuta na korosho vuta picha mkuu kwa mtaji wa milion 6 upate faida ya shiling 200 kwa kila kilo
Nnzuri mkuu na ykipata mkawa waaminifu mnatengeneza hela nzuri tu mnabakia kuulizia wapi wameshavuna
 
Nnzuri mkuu na ykipata mkawa waaminifu mnatengeneza hela nzuri tu mnabakia kuulizia wapi wameshavuna
Nikweli kabisa mkuu hii biashara inachangamoto zake ikiwemo ya vijana wanaosaidia kukusanya mzigo kutokuwa waaminifu
 
Kwanini usisafirishe kontena 1 upeleke China,India au Vietnam. Upate pesa maradufu
 
Kiukweli mkuu bado korosho zinalipa tu kwa mfumo wa kangomba ila inahitaji uwe na msuli wa pesa fikiria mfano umenunua korosho kilo 5000 kwa mchanganuo wa shiling 1300 kwa kangomba ambapo hapo inajumuisha na kijana anaekununulia ambapo yeye anachukua shiling 100 kwa kila kilo ndipo inakalia hiyo 1300... kwa hiyo ukiwa na mtaji wa kununua kilo 5000 kwa thamani ya shiling 6,500,000/= ambapo hapo imejumuisha kila kitu na ukipeleka ghalani hata ukipata faida ya kila kilo shiling 250 sio mbaya kwasababu itakuwa kilo 5000×250=1,250,000 faida....sasa tuwe tu wakweli kwa mtaji wa 6500000 uzalishe faida ya 1250000 tena ndani ya wiki 2 tu unaona ni kitu kidogo?
Nimeipenda hiii
 
Shida vyama havilipi on time mkuuu

Naangalia itv kila siku wanaanza akushukuru afu wanalia tunaombaa mtulipe kwa wakati

Na wengi wanassma wanalipwa wakati mwingjne .mda aa kupanda ushaisha

Kuwekeza mil 6 bila kuzunguka hili napo liangalie
Noma
 
Biashara Hiyo Wakati Wa Jiwe Watu Walisomeshwa Number
Mpaka Magari Ya Wale Jamaa Yakawa Yanaanguka Tu
 
Ni kweli inalipa lakini sio kama miaka 5 iliyopita ambapo Faida ilikuwa almost pasu pasu

Mfano kama umenunua Kangomba ya milioni 6.5 ilikuwa unapata Faida ya 7M ama 6M
Mbona hamkutuambia sasa dah
 
Kwanini usisafirishe kontena 1 upeleke China,India au Vietnam. Upate pesa maradufu
Hii ni biashara ya ulanguzi,ukitaka uifanye kuwa rasmi unahitaji kuwa 'na vibali 'na uifanye kwa njia inayokubalika na serikali ikiwemo kununua korosho zako kwenye minada kitu ambacho unatakiwa uwe 'na mtaji wa kutosha.
 
Wanajamvi, habari za muda huu na poleni na mihangaiko ya kutwa nzima.
Korosho ni zao linalolimwa zaidi mikoa ya Lindi na Mtwara na sasa ni kipindi rasmi cha msimu wa korosho.

Nahitaji Tajiri ambaye yupo tayari kununua korosho , kwa rejareja (kangomba ) kwa sababu nina uzoefu wa biashara hii na usimamizi wa zao la korosho. Kwa aliye tayari karibu sana, tuwasiliane Inbox.
Fanya hivi edit uzi wako kwakuweka mambo yafuatayo..

Uko wapi?
Unaweza ku supply kiasi gani?
Sample au sampuli unatoa?
Mawasiliano yako....

Sio mnunuzi lakini nmeona uweke hivi vitu ili wateja wajue uko seriousl. Asante
 
Mbona hamkutuambia sasa dah
Sio rahisi kumwambia Kila mtu, jambo la muhimu ni kuwa msomaji wa mara Kwa mara wa jukwaa la Uchumi na biashara.

Mara nyingi baadhi ya members huwa wanaposti fursa zinazopatikana kwenye maeneo yao
 
Back
Top Bottom