Njoo tujuzane kuhusu Hisa

Njoo tujuzane kuhusu Hisa

Je kama ntamiliki hisa za kampuni X, na nikapewa cheti cha umiliki hisa, ikatokea hiyo kampuni kufanya vibaya kiasi CHA kushusha thamani ya mtaji, vipi status ya kile cheti nkienda kuombea mkopo!

Tusisahau kuwa cheti kile kinabeba thamani ya hisa kwa hyo hupungua na kupanda thamani kulingana na hisa zako sokoni
 
umeleta cha mana sana lkn ebu niulize kaswali his a isipoongezaka haupati chochote??????

Utaweza kubakia faida 2 kama hisa isipoongezeka;1)utaendelea kupata dividends(gawio la faida kwa kila mwanahisa) 2; kuwa na asset ambayo ni cheti cha umiliki wa hisa...
NB; mara nyingi sana hisa hubadilika hivyo ngumu sana kubakia bei ile ile
 
Mimi nahitji sana elimu juu ya huu uwekezaji,OK huyo broker nani mlipa mwisho wasiku??
 
elimu nzuri sana hii ngoja nipitie dse.
 
umeleta cha mana sana lkn ebu niulize kaswali his a isipoongezaka haupati chochote??????
Sio tu kwamba haupati chochote, thamani ya hisa ikishuka unaweza ukapoteza kila kitu, na pia hakuna guarantee ya dividends kwa vile una hisa, kampuni ina uhuru wa kuamua kama itatoa dividends kila mwaka.

Kuinvest katika hisa individually ni kama bahati na sibu fulani, na DSE bado iko shallow sana makampuni ni machache sio rahisi kufanya diversification ya maana, ni vizuri zaidi kuinvest kwenye funds, funds zina mchanganyiko wa hisa za makampuni mbalimbali, bonds etc.

Pia kwa TZ protection ya shareholders sio nzuri katika hisa angalia suala la NICOL yaani hawa DSE kama vile wamenawa mikono na ilemissue hakuna taarifa yoyote inayoeleweka.

Na niseme kuwa nina suspicion kubwa kuwa kuna insider trading inaendelea na hisa za kampuni nyingi hapa bongo, insider trading ni pale watu wa ndani ya kampuni wanapotumia taarifa ambazo sio public kuuza na kununua hisa so wao wanafaidika sisi wawekezaji wa kawaida inakula kwetu.
 
Sio tu kwamba haupati chochote, thamani ya hisa ikishuka unaweza ukapoteza kila kitu, na pia hakuna guarantee ya dividends kwa vile una hisa, kampuni ina uhuru wa kuamua kama itatoa dividends kila mwaka.

Kuinvest katika hisa individually ni kama bahati na sibu fulani, na DSE bado iko shallow sana makampuni ni machache sio rahisi kufanya diversification ya maana, ni vizuri zaidi kuinvest kwenye funds, funds zina mchanganyiko wa hisa za makampuni mbalimbali, bonds etc.

Pia kwa TZ protection ya shareholders sio nzuri katika hisa angalia suala la NICOL yaani hawa DSE kama vile wamenawa mikono na ilemissue hakuna taarifa yoyote inayoeleweka.

Na niseme kuwa nina suspicion kubwa kuwa kuna insider trading inaendelea na hisa za kampuni nyingi hapa bongo, insider trading ni pale watu wa ndani ya kampuni wanapotumia taarifa ambazo sio public kuuza na kununua hisa so wao wanafaidika sisi wawekezaji wa kawaida inakula kwetu.

DSE kuwa shallow inachangiwa na uvivu na uzembe wa serikali.
Serikali ilitakiwa itunge sheria ya kuyafanya makampuni ambayo yamefikia mtaji au thamani kiasi fulani yaingie DSE.
Kuna makampuni mengi yanatakiwa kuingia DSE. Angalia sekta ya mawasiliano, uchukuzi, viwanda vikubwa na vya kati, utalii.
 
Bei husika ni hyo closing price
 

Attachments

  • 1439281408560.jpg
    1439281408560.jpg
    22.5 KB · Views: 206
**INAENDELEA***


#Wapi ninaweza kununua au kuuza hisa??

Hisa zinanunuliwa na kuuzwa kupitia madalali(shares brokers) maalum ambao wamehalalishwa na serikali na wana leseni za biashara hiyo.

#Kwa wakati gani na kwa namna gani ninaweza kununua hisa??

Kwanza kabisa inabidi kuhakikisha kampuni unayotaka kununua hisa imeorodheshwa(is listed company) na soko kuu la hisa la Dar es salaam. Mpaka sasa soko limeorodhesha kampuni zipatazo 21, kampuni 14 zikiwa za ndani ya nchi na 7 zikiwa zakutokea nje.Pia unahitajika kujua bei kwa kila hisa ambazo unahitaji kununua.
Ukishajua hayo, unatakiwa uende kwa dalali wa hisa kwa ajili ya usajili na ununuaji wa hizo hisa.kumbuka bei za hisa unaweza ukazipata kutoka kwenye tovuti ya dse.go.tz alafu nenda kwenye market reports uchague daily market report hapo utaona bei za hisa za kampuni zote kwa siku husika.

#NB ;bei husika ni hyo closing price na sio opening price. Na pia kama huna uhakika na hisa unazotaka kununua ni vyema ukapata ushauri kutoka kwa dalali(share broker).

#Mahitaji yapi natakiwa niwe nayo wakati wa kununua hisa??
Ili uweza kusajiliwa na dalali wa hisa unaweza kuhitajika kutoa taarifa fupi zinazokuusu wewe kama vile; jina kamili,mawasiliano yako,namba ya akaunti yako,kitambulisho chochote na muhimu mtaji wako ulionao uanotaka kuwekeza.

#Gharama zipi hutozwa pindi ununuapo hisa ??

Dalali analipwa ada ya asilimia 2 ya mtaji wekezwa( 2% of capital).N gharama ya Tsh.1000/= kwa ajili ya kuingiza fedha kwenye akaunti ya dalali.

#Mfano ; tuseme kwamba unataka kununua hisa 200 za CRDB ambazo gharama yake ni Tsh.400/= kwa kila moja, inamaana unahitajika uwe na mtaji wa Tsh.80000/=(200x400=80000).ada ya dalali unamlipa Tsh.1600 yaani 2%x 80000=1600/=.

#NB ;kiasi cha chini cha hisa unachotakiwa kupanga kununua kwa Tanzania hakitakiwi kipungue hisa kumi(10).


#ZIADA ;
Orodha ya madalali na mawasiliano yao;

**Orbit Securities Company Limited
P.O. Box 70254, DAR ES SALAAM
Offices: 4th Floor, Golden Jubilee Towers, Ohio Street,
Tel: 255 22 2111758, Fax: 255 22 2113067
E-mail: orbit@orbit.co.tz
-
**Core Securities Ltd
P.O. Box 76800, DAR ES SALAAM.
Offices: Fourth Floor – Elite City Building, Samora Avenue,
Tel: +255 22 2123103, Fax: +255 22 2122562
E-mail: info@coresecurities.co.tz
Website: www.coresecurities.co.tz
-
**SOLOMON Stockbrokers Limited
P.O. Box 77049, DAR ES SALAAM
Offices: Ground Floor – PPF House, Samora Avenue/Morogoro Road.
Tel: 255 22 2124495/2112874, Fax: 255 22 2131969
Mob: +255 714 269090 +255 764 269090
E-mail: solomon@simbanet.net, info@solomon.co.tz
Website: www.solomon.co.tz
-


**Zan Securities Limited P.O. Box 5366,
Dar es salaam P.O. Box 2138, Zanzibar
Offices: Mezzanine Floor, Haidary Plaza, Dar es salaam 1st Floor, Muzammil Centre, Malawi Road, Zanzibar
Tel: +255 22 2126415, Fax: 255 22 2126414 Mob: +255 786 344767, +255 755 898425
E-mail: info@zansec.com
-
**Rasilimali Limited P.O. Box 9373, DAR ES SALAAM
Offices: 3rd Floor, CHC Building, Samora Avenue,
Tel: 255 22 2111711 Fax: 255 22 2122883
Mob: +255 713 777818 / 784 777818 / +255 754 283185
E-mail: rasilimali@africaonline.co.tz
-
**Tanzania Securities Limited
P.O. Box 9821, DAR ES SALAAM O
ffices: 7th Floor, IPS Building Samora Avenue/Azikiwe Street
Tel: 255 (22) 2112807, Fax: 255 (22) 2112809
Mob: +255 718 799997 / +255 713 244758
E-mail: info@tanzaniasecurities.co.tz
Website: www.tanzaniasecurities.co.tz
-
**Vertex International Securities Ltd
P.O. Box 13412, DAR ES SALAAM.
Offices: Annex Building – Zambia High Commission, Sokoine Drive/Ohio Street,
Tel: 255 22 2116382 Fax: 255 22 2110387
E-mail: vertex@vertex.co.tz,
 
naomba kuuliza swali mtoa mada cheti ya hisa nachopewa mimi! kina dhamani si ndiyo? je unaweza tumia kama bond ya kukopea mkopo bank? Kama ndio mkopo unabase kwenye dhamani ya hisa au dhamani baada ya kawio?
 
kwa mfano kama gawio linagawiwa mara moja... Nitaendelea kupewa gawio kwa miaka mingap?kwa ufafanuzi zaidi mwisho wa kulipwa kutokana na hisa nilizoweka ni miaka mingap?
 
Tangu niangalie sinema ya "Wolves Of Wall Street" naogopa hili neno soko la hisa,.....
 
unatoa fedha zako(kununua hisa).... zinatumiwa na hao wauza hisa kuendeshea shughuli zao halafu wakipata faida mnagawana kwa mujibu wa mkataba wenu na kiasi cha faida kilichopatikana.
 
CEOgwamzy nimependa sana maelezo yako!!! lakini hili sakata la benki ya walimu limeishia wapi???
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom