Njoo uwekeze kwenye biashara ya mafuta (Fuel) kwa laki 1 tu kama kima cha chini

Njoo uwekeze kwenye biashara ya mafuta (Fuel) kwa laki 1 tu kama kima cha chini

Nikiwa kama mfanyabiashara Uliposema tu muwekezaji hatahusishwa na hasara ndo uliponipeperusha........hio deal wazungu wanasema ni "too good to be true"
kumbe umemwelewa huu ni high level utapeli
 
Mkuu kampuni ina properties inazomiliki so haiwezi kufa hadi kushindwa kuwalipa wawekezaji stahiki zao. Kwa wanaofanya biashara za mafuta hili wanalielewa vyema. Kumbuka kila kitu kinafanyika kisheria hivyo kufanya usalama wa pesa yako kuwa mkubwa. Nakukaribisha sana uwekeze Mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah..bosi kampuni yenu ni DINI gani? Nimevutika mno..[emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 
Kuna watu wanaenda pigwa hapa
Mafuta faida yake ni 200 hadi 500 kwa lita
Kwa mtaji wenu nyie mtanunua kwa hawa wakubwa maana yake faida imepungua tena sio 500
Hao watu 100 wakijichanga kwa 2mil kila mmoja ni 200mil ambayo mtafanikiwa nunua tanker 2 kwa mkupuo
Faida huwez pata ya kuwagawia wote 10pc ya uwekezaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah...Bosi huwezi jua lengo la kampuni....labda ni kusaidia watu..au kufua pesa....
Wanachukua mkopo kwa watu na kuulipa riba ya 120% kwa mwaka...wakati benki Sasa hivi Hadi 16% kwa mwaka unapata .....
Kama si wapigaji nitajiunga nao...ila siyo kwenye biashara yao..bali kwenye dini yao......[emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 
Hatari hii. Kuna sheria inavunjwa hapa. Kampuni private (LTD), hairuhusiwi kukusanya mtaji kutoka kwa public (uma) namna hii. Public company (PLC) mahali pake ni DSE.

Else aseme yeye ni benki anakusanya deposits....but ikiwa hivyo biashara ya mafuta haipo.

Lakini pia return (ROI) ya 10% kwa mwezi haipo mahali popote duniani....I can bet hata wanachimba mafuta hawapati hiyo ROI.

Nipo tayari kufundishwa/kuelimishwa hapa kuhusu hili....nimesoma zamani, huenda mambo yamebadilika sasa.

Mwanzo nilidhani ni issue ya April Fools, but naona ni thread ya 31/03/2019.
 
Hatari hii. Kuna sheria inavunjwa hapa. Kampuni private (LTD), hairuhusiwi kukusanya mtaji kutoka kwa public (uma) namna hii. Public company (PLC) mahali pake ni DSE.

Else aseme yeye ni benki anakusanya deposits....but ikiwa hivyo biashara ya mafuta haipo.

Lakini pia return (ROI) ya 10% kwa mwezi haipo mahali popote duniani....I can bet hata wanachimba mafuta hawapati hiyo ROI.

Nipo tayari kufundishwa/kuelimishwa hapa kuhusu hili....nimesoma zamani, huenda mambo yamebadilika sasa.

Mwanzo nilidhani ni issue ya April Fools, but naona ni thread ya 31/03/2019.
Mkuu nimetoa ufafanuzi wa kutosha tu hapo juu namna ya ufanyaji wetu kazi na kila kitu kinafanyika kisheria hakuna longo longo. Kwa maelezo zaidi karibu ofisini kwetu Chanika Dar Es Salaam ujionee mkuu na upate ufafanuzi zaidi. Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kumbe umemwelewa huu ni high level utapeli

Mfanyabiashara yeyote/tafsiri sahihi ya mjasiriamali ni lazima uingie risk ya pata potea ndo njia pekee ya kuongeza thamani ya pesa yako.

Hiki anachokielezea ni kama njozi. Yani wao wabebe gharama za uendeshaji na wabebe hasara halafu wewe wakupe tu faida? Charity work??? Maybe

Basi kila mtu angekua tajiri kama kuna mfumo huo wa biashara
 
Kwani mkuu ukiweka bank fixed deposit then kwa bahati mbaya bank ikapata hasara pesa yako itapotea ama utaipata? So huo ni mfano tu mkuu, ungekua shareholder ndio ungehusika kwenye hasara haya mbona yanafanyika sehemu nyingi tu Duniani mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app

Mfumo wa benki una taratibu zake. Hizo fixed deposit accounts hazijakuwepo tu. Kuna biashara ambako hio hela inapelekwa "low risks" kama government bonds au treasury bonds na vitu km hivyo. Na bado kuna usimamizi mkubwa wa BOT ili kumantain liquidity ya taasis husika

Pia biashara nyingine ambayo unawekeza na hela yako inaongezeka tu(haiwezi kula kwako) na haina gharama za uendesheji ni mifuko ya pensheni. Ina taratibu mahususi zake

Ila hii yalwako nashangaa. Hakuna gharama za uendeshaji na hakuna hasara ni faida tu. Nyie mnachapisha noti au?

Halafu kusema sehemu nyingi duniani wanafanya hivo hata telegram/deci kila aina ya ponzi schemes ziko dunia nzima hio sio sababu.

Kinachoniogopesha ni kuwa mfumo wenu wa biashara unavunja miiko yote ya biashara toka dunia iumbwe.

Unaposema ukiweka hio hela unakua sio shareholder sasa shareholder ni nani kama anayewekeza sio shareholder. Kitendo cha kuongeza mtaji kwa nia ya kupata faida automatically unakua shareholder.

Labda unipe maelezo zaidi. Unaweza kunishawishi mimi nifunge biashara zangu zoote niwaletee hata milion 200 halaf nikae likizo nasubiria miez mi3 nipate gawio la 10% bila kufanya kazi yoyote bila risk yoyote
 
Chanika mkuu, Karibu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Nina Uzoefu mkubwa na mambo ya mafuta,
Ukisema Chanika napata wasiwasi pengine ni kituo kidogo tu cha mafuta unazungumzia. Labda unataka mjichangishe mnunue Kurasini au Kigamboni na kuuza rejareja au kwenye Petrol Station yenu kisha mgawane faida. Ukitumia bei za "Platt" basi faida ya mafuta haizidi hata 100/=. Watu wako tayari kwa uwekezaji, lakini unahitajika kua muwazi zaidi. Unless kama unaogopa kuibiwa idea yako.
 
UWEKEZAJI KATIKA BIASHARA YA MAFUTA

Nimeona niwaletee fursa niliyonayo ambayo inahusiana na uwekezaji kwenye biashara na kuweza kujiongezea kipato nje ya mshahara au kazi yako unayofanya, fursa hii inawahusu watu wote ila nimeona ni vyema nanyi niwashirikishe kuliko kuwafaidisha wengine tu nikawasahau ndugu zangu, sasa twende pamoja kuijua fursa hii!

Tuna kampuni inayojihusisha na biashara ya mafuta na gas ambapo tumeona ni vyema kuwashirikisha wadau katika uwekezaji wa biashara hii ya mafuta.

Tunakaribisha watu mbalimbali kuwekeza kwenye mradi wetu wa mafuta kiasi ambapo mwekezaji atakua anapata Gawio la 10% kila mwezi kutokana na uwekezaji wake na baada ya muda wa mkataba tuliokubaliana kumalizika mhusika anaweza kuamua kuhuisha mkataba wake ama akachukua hela yake aliyowekeza. Namna ya kuwekeza ni kama ifuatavyo ;

1. uwekezaji huu unafanyika kisheria kwa kufuata taratibu zote za uwekezaji katika miradi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya usimamizi wa mwanasheria wa kampuni!

2. Mwekezaji atalipwa gawio la 10% ya Gharama ya uwekezaji wake kila mwezi bila kuathiri pesa yake aliyowekeza.

3. Mwekezaji hatahusishwa na hasara yoyote itakayojitokeza ktk uendeshaji.

4. Mwekezaji hatohusishwa na Gharama yoyote ya uendeshaji.

5. Kiwango cha chini cha uwekezaji ni 100,000 na Kiwango cha juu ni 2,000,000 kwa mtu binafsi. Kwa taasisi au kampuni kima cha chini cha uwekezaji ni 500,000 na kima cha juu ni 10,000,000 kwa taasisi au kampuni moja.

6. Mkataba wa uwekezaji kwa mtu binafsi utahuishwa kila baada ya miezi 3 ( hivyo kila baada ya miezi 3 utaamua kuendelea kuwekeza au kuondoa pesa yako kwenye uwekezaji). Kwa taasisi au kampuni muda wa kuhuisha mkataba ni kila baada ya miezi 6.

7. Gawio litatolewa tar 1 ya kila mwezi kupitia account ya kampuni ( hapa pesa hutumwa kwa mhusika automatically kwa kutumia system ya bank inayotumiwa na kampuni yetu).

8. Mwekezaji anaruhusiwa kukagua mradi wetu wa mafuta na documents zote za usajiri kisheria ili kujiridhisha kabla hajaamua kuniunga na mradi.

9. Mwekezaji anaruhusiwa kuwa na mwanasheria wake au shahidi wakati wa kufanya makubaliano ya mkataba.

Sifa za Mwekezaji ni kama ifuatavyo ;
1. Anatakiwa kuwa mtanzania wa kuzaliwa au kuandikisha (akiwa sio mtanzania anapaswa kuwa na kibali cha kuishi nchini na kibali cha kufanya kazi nchini)

2. Anatakiwa kuwa na umri usiopungua miaka 18.

3. Awe na akili timamu.

4. Jinsi zote.

5. Awe na kitambulisho cha Taifa, cha mpiga kura au leseni ya udereva. Picha moja passport size.

6. Shilingi elfu 2 ya kulipia form.

7. Pesa ya uwekezaji isiyopungua 100,000 kwa mtu binafsi na 500,000 kwa taasisi.

NB : Kwa aliyekidhi vigezo tajwa hapo anazo sifa za kuwa mwekezaji wetu, tunahitaji wawekezaji 100 kwa awamu ya kwanza.
Dirisha la usajiri kwa awamu ya kwanza litafungwa tarehe 30 April 2019.

Tunapenda kuwakaribisha nyote katika uwekezaji huu wa kibiashara, kwa watakaowiwa kuwekeza wawasiliane nami kwa maelezo zaidi kupitia ;
0764 143 900
0715 143 900
hemedrenatus@yahoo.com
hgecompany@gmail.com

Ahsante

Sent using Jamii Forums mobile app

Huwa kuna wakati nawashangaa watu kama nyie. 80% ya wana JF wamevurugwa kiamaisha (kwa mujibu wa tathmini yangu isiyo rasmi) halafu wewe unakuja na uzi usio na kichwa wala miguu.. Let me warn you si kila siku ni ijumaa acheni hizo mwisho wenu si mzuri sana.

Wana JF hii ni kama zileeeee...
 
Kuna watu wanaenda pigwa hapa
Mafuta faida yake ni 200 hadi 500 kwa lita
Kwa mtaji wenu nyie mtanunua kwa hawa wakubwa maana yake faida imepungua tena sio 500
Hao watu 100 wakijichanga kwa 2mil kila mmoja ni 200mil ambayo mtafanikiwa nunua tanker 2 kwa mkupuo
Faida huwez pata ya kuwagawia wote 10pc ya uwekezaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Huo ndo ukweli, ukiona unaitwa kwenye fursa jua ww ndo fursa

Sent using My phone
 
Ndugu naomba nikujulishe tuu hiki unachokifanya ni kinyume na sheria za nchi kwahiyo hakuna mkataba ambao utasimama kwa sababu mkataba ni batili toka mwanzo ( void ab initio). Kama ungekuwa unauza share za kampuni tungekubaliana ni sawa ila hii kitu unafanya hakuna huwezi kuchukua hela kutoka kwenye public halafu ukaahidi kutoa riba wakati ujasajiliwa kama taasisi ya fedha Soma Kifungu cha sita 6(1mpaka 4 cha Bank and finance act see a link https://www.bot.go.tz/BankingSupervision/BAFIA2006.pdf ) Ukipata muda wa ziada unaweza kusoma kesi namba 66/2007 kati ya ULF NILSON dhidi ya Dr Tito M Andrew imeambtanishwa hapo chini.
 

Attachments

Back
Top Bottom