Njooni tuambizane ukweli, Hivi wanawake wa kaskazini ni wife material kweli wa kuweka ndani kama mke au nataka kuingia choo cha kike?


Ukitaka ufanywe dili, wee jichomeke
 
Hawafai na ni hatari, nipe namba yake nimuhoji.
 
Angalia tabia usiangalie kabila,
 
Kiufupi kipindi Bro yupo hai mwanamke alikua anatoroka anaenda kufanya umaid kwenye Bar anakaa mpaka muda ataojisikia yeye kurudi Nyumbani. Alivofariki mke aliuza kila kitu alichoachiwa na bro akaondoka na watoto kwenda kuolewa na mwanaume mwingine.
Hio wapi Kilimanjaro moja? Chagga & Pare originality
 
Mi naona haya ya kabila hili wapo vipi na wale wapo vipi ni masuala ya kizamani, nyie weusi mnabaguana nyie kwa nyie kwanini waarabu ,wazungu nawahindi wasiwabague mwishowe mnaanza kulia mnabaguliwa....

Haa mambo ya makabila na tabia ni zilipendwa kipindi hicho wazee wetu wanakulia vijijini wanakuja mjini kutafuta maisha, katika ile kujichanganya wanakutana na watu wenye tabia tofauti tofauti wametoka nazo vijijini...

Hivi sasa vijana hawa wa mjini anakuambia mchaga au mkurya lakini hana tabia hizo...

We kama umempenda oa tu.. jamii hivi sasa imeelimika na jamii nyingi zinaishi kwa pamoja...
 
Mzee wangu lazima ulisome kabila kabla haujaingia kwenye mila na desturi za watu sio baadae ukoo mzima unahamia kwako uwalishe unaanza kukaza macho, wao kwao kuhamia kwa mtu aliemuoa ndugu yao ni kitu cha kawaida kumbe wewe kwenye desturi zenu haipo hio hapo lazima upasuke
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…