Njooni tusemezane. Sheria gani inakataza watu kuchangishana? Waziri Mkuu yupo sahihi kumkamata Niffer?

PM yupo sahihi kila mtu akisema anachangisha .. ni mwanya wa utapeli "tuma kwenye namba hii" kitengo cha maafa kipo chini ya ofisi ya waziri mkuu na yanapotokea maafa yoyote utaratibu wa kusaidia utatoka chini ya ofisi yake kupitia katibu mkuu... Ni kiasi cha kufuata utaratibu tu ... Bila utaratibu ni machafuko
 
Tangu huyu PM adanganye kuwa rais aliyepita yupo ofisini anachapa kazi wakati ameshakata moto sina imani nae tena
 
Mnamlaumu PM bure. Mmesahau kuwa ametumwa na hili nalo akaliangalie
 
Msilete ushabiki kwenye mambo ya kisheria! Huyo Nifer hajaenda kuuawa bali anahojiwa na mamlaka zitaona nia yake ilikuwa nini. Mamlaka hazina bifu na huyo dada naamini ni ishu ya yeye kutoa ushirikiano tu ishu yake inaisha.

Sema kwa akili zake za mitandaoni ndo utaskia anapost kuwa ana strong arm hayo ndo yanaweza kumkost. Nadhan hajui serikali inavyofanya kazi yeye anajua kuuza bidhaa kutoka China basi. Anafikiri serikali ni kama konteina la bidhaa
 
Mi naona Tatizo sio kuchangisha, tatizo lipo katika kuwajibika Kwa waliokusanya hiyo michango kutoa maelezo ya Matumizi Ya hizo Fedha na wawe tayari , kukaguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Sirikali au atakaye teuliwa au kuchaguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Sirikali na ripoti iwe wazi kwa umma.
 
Issue ni kuwatoa kwenye jambo muhimu muishie kujadili yasiyo na tija kwa Taifa
Hao wote ni dugu moja
Mpo hapa kumhurumia sijui nifa
 
Sheria irekebishwe. Inaua moyo wa kujitolea. Iangalie namna ya kujumuisha wenye ushawishi na ambao kwa kweli hufanya harambee za namna hiyo kwa matukio ndani ya jamii, kama malisa, nifa na mwl yusuf. Wapo wengi ambao huwiwa kufanya mchango wao kupitia ushawishi wao. Ofisi ya waziri mkuu sidhani kama ina ushawishi wa kuwafikia wafuasi wa mitandao ya kijamii wa watu kama nisha, sasa unatap vipi michango yao hao ambao ni "jeshi kubwa" ili nao wajisikie wamefanya kitu kwenye maafa yoyote. Ni kwa kuwatumia influensa, watu wanaowafutilia mitandaoni kama nifa.
 
Naunga mkono hoja. Wapewe akaunti maalum za majina yao hawa mainfluensa ambazo mwisho wa siku zitaenda benki kuu kwenye akaunti mama ya maafa ya serikali
 
Mkuu kuna maafa ya kitaifa na matatizo binafsi.... Hapa tunazungumzia maafa ya kitaifa na jukumu la haya maafa liko chini ya ofisi ya Waziri mkuu

Ukisoma hiyo sheria maafa yote yameelezewa vizuri kabisa na ndio maana hukuona serikali ikimwandama kipindi kile anachangisha pesa za matibabu ya mtu binafsi.
 
Weka sheria na kifungu kilichokoukwa ili usiwe shabiki kama mimi
 
You belong to the past. Mwaka 2024 unaweza toa hoja kama hii? Dawa hapo weka mechanism ya kuwatumia hao influensa kupata michango ya raia wwa kawaida. Unadhani nifa atapata mchango gani toka kwenye taasisi ama mashirika, yale mashirika yanataka pr ni wazi yataenda serikalini na kwenye vyombo vya habari wakati wanatoa mchango wao. Sasa nifa anakusaidia kuipata pesa ya wadangaji, masista duu na mabrazameni wa buku 2000 na kada kama hizo. Ambazo kiuhalisia hazina interaction na formalities.
 
Kiswaswadu ni mkurupukaji sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…