Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Katika kile kinachoonekana mwendelezo wa wiki ya vituko, kiki na ukiukwaji wa misingi ya utawala wa sheria, Mkuu wa Wilaya ya Nkasi bw. Said Mtanda jana 12.08.2017 aliamuru wanajeshi wa JKT kikosi cha Milundikwa kuwapa adhabu za kijeshi wananchi wa kijiji cha Ntuchi wilayani humo.
Habari zilizopatikana toka chanzo cha habari kilichokuwa eneo la tukio kwenye mnada uliopo kijijini hapo kinasema Chanzo cha tukio hilo ni kwamba, kulikuwa na Kazi ya ujenzi Wa darasa kwa njia ya kujitolea katika shule ya kijiji hicho lakini pia siku hiyo ni siku ambayo kijijini hapo kunakuwa na mnada (gulio) kila mwezi hivyo wananchi hupata fursa ya kufanya manunuzi ya mahtaji mbalimbali kwa ukaribu Mara moja kila mwezi maana vinginevyo wanalazimika kwenda mjini Namanyere umbali wa kilomita zaidi ya 20 toka kijijini hapo.
Hivyo baadhi ya wananchi walikwenda mnadani kujipatia mahtaji hasa baada ya pendekezo lao kwa uongozi wa kijiji kupanga siku nyingine nyuma au mbele ya siku hiyo kukataliwa kwa madai kuwa siku hiyo ndo Mkuu wa wilaya ana nafasi ya kuja kushiriki nao.
Mkuu wa wilaya alipowasili na kukuta watu wachache aliamuru Gari la Jeshi la wananchi kuwaleta askari Wa JKT ambao walitinga mnadani na kusimamisha shughuli za biashara na kuanza kutenga wananchi kutokana na vijiji wanavyotokea na aliyeonekana anatokea kijiji cha Ntuchi aliamuriwa kuruka kichura au kujiviringisha toka hapo mnadani hadi eneo la ujenzi umbali Wa zaidi ya mita 200. Walioonekana kushindwa adhabu hizo au kudanganya makazi walipigwa na kuburutwa.
Mtoa taarifa mwingine niliyeongea naye anasema wakazi wa kijiji hicho hasa wazee ambao wengine wameshapita umri Wa kushiriki shughuli za maendeleo wamepanga kulifikisha suala hili kwa Mkuu wa mkoa wa Rukwa Bw. Zelothe Stevine.
Kama mwandishi wa habari niko safarini Mbeya, nikifika Rukwa kesho kutwa nitakuwa na mwendelezo wa sakata hili.
-----------
Taarifa hii imekanushwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Zaidi soma => News Alert: - Usahihi wa taarifa toka Nkasi
Habari zilizopatikana toka chanzo cha habari kilichokuwa eneo la tukio kwenye mnada uliopo kijijini hapo kinasema Chanzo cha tukio hilo ni kwamba, kulikuwa na Kazi ya ujenzi Wa darasa kwa njia ya kujitolea katika shule ya kijiji hicho lakini pia siku hiyo ni siku ambayo kijijini hapo kunakuwa na mnada (gulio) kila mwezi hivyo wananchi hupata fursa ya kufanya manunuzi ya mahtaji mbalimbali kwa ukaribu Mara moja kila mwezi maana vinginevyo wanalazimika kwenda mjini Namanyere umbali wa kilomita zaidi ya 20 toka kijijini hapo.
Hivyo baadhi ya wananchi walikwenda mnadani kujipatia mahtaji hasa baada ya pendekezo lao kwa uongozi wa kijiji kupanga siku nyingine nyuma au mbele ya siku hiyo kukataliwa kwa madai kuwa siku hiyo ndo Mkuu wa wilaya ana nafasi ya kuja kushiriki nao.
Mkuu wa wilaya alipowasili na kukuta watu wachache aliamuru Gari la Jeshi la wananchi kuwaleta askari Wa JKT ambao walitinga mnadani na kusimamisha shughuli za biashara na kuanza kutenga wananchi kutokana na vijiji wanavyotokea na aliyeonekana anatokea kijiji cha Ntuchi aliamuriwa kuruka kichura au kujiviringisha toka hapo mnadani hadi eneo la ujenzi umbali Wa zaidi ya mita 200. Walioonekana kushindwa adhabu hizo au kudanganya makazi walipigwa na kuburutwa.
Mtoa taarifa mwingine niliyeongea naye anasema wakazi wa kijiji hicho hasa wazee ambao wengine wameshapita umri Wa kushiriki shughuli za maendeleo wamepanga kulifikisha suala hili kwa Mkuu wa mkoa wa Rukwa Bw. Zelothe Stevine.
Kama mwandishi wa habari niko safarini Mbeya, nikifika Rukwa kesho kutwa nitakuwa na mwendelezo wa sakata hili.
-----------
Taarifa hii imekanushwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Zaidi soma => News Alert: - Usahihi wa taarifa toka Nkasi