Wafanyakazi wengi wamelazimika kuweka Pesa huko kingine ni affordable makato nafuu, ungejibu hivyoUwongo pro max, serikali inalipa popote hata ukiwa na akaunt bank ya Amana
We zwazwa njoo kijijini uone, watu wa bank wanaongea na hizo taasisi(hasa wahasibu) wanakwambia malipo yako lazima yapitie NMB au kama unatumia CRDB cheque ni ya NMB(wanakwambia taasisi ina account NMB pekee) gharama za kuhamishia CRDB ni za kwako, hapo sasa unadai 2M gharama za transfer ni zaidi ya elf 10(mind you na transfer ni 72Hrs within working days).Uwongo pro max, serikali inalipa popote hata ukiwa na akaunt bank ya Amana
Wewe unaongelea malipo yanayolipwa kwa TISS(BoT direct) na siyo cheque na hizi taasisi ndogo ndogo ambapo cheque lazima isainiwe na DT/DMO/DEO na Mwenyekiti wa kamati.Uwongo pro max, serikali inalipa popote hata ukiwa na akaunt bank ya Amana
Kwani CHADEMA hawalipi kodi?Kumbe CHADEMA mnapewa kazi kwenye Serikali ya CCM?
Yes hili la MAKATO nafuu nakubaliana na wewe kabisa kule CRDB niliweka 150,000 baada ya muda nikakuta sifuri kuomba statement ni makato duuWafanyakazi wengi wamelazimika kuweka Pesa huko kingine ni affordable makato nafuu, ungejibu hivyo
Huyu kama atakubali Rais amteue na akapewe kitengo kule Mwigulu kashindwa,View attachment 2805767
MS Ruth Zaipuna Mkurugenzi Mkuu NMB.
======
Wasalaam Jf team,
Waswahili tunasema " Mnyonge Mnyongeni lakini haki yake Mpeni "
Sote tunakumbuka baada ya NBC Bank kuvunjwa Mwaka 1997 na baadae kuanzishwa kwa Benki mpya ya Makabwera ya NMB na baadae Benki hiyo kubinafsishwa kwa Rabobank ya Uholanzi iliyomiliki hisa asilimia 49 na Rabo baadae kumuuzia baadhi ya Shea Arise,
Wakati wote NMB PLC imekuwa ikiongozwa na watu kutoka nje ya nchi tu isipokuwa huyu Mkurugenzi wa Sasa Bi Ruth Zaipuna aliyekabidhiwa nafasi hiyo ya Ukurugenzi Mkuu rasmi mwaka 2020.
Kumbukumbu zinaonesha wakati mama huyu anaingia madarakani NMB bank ilikuwa na matawi yapatayo 100 tu nchi nzima na ATMs zipatazo 500 nchi nzima.
Leo NMB bank imefikisha matawi zaidi ya 230 na ATMs zaidi ya ATMs 1,000 na mawakala zaidi 12,000 nchi nzima hii ni sawa na kusema mama huyu ameikuza bank hii ya Makabwera kwa zaidi ya marambili, yaani ukuaji wa 100% au kwa lugha rahisi ni sawa na kusema NMB bank PLC imefika katika Kila Jimbo la Uchaguzi la kiserikali haba bara.
Kutoka katika tovuti ya NMB taarifa zinaonesha NMB bank ilikuwa na wateja wasiozidi 600,000 miaka kumi iliyopita na wakati huu wa Ruth Zaipuna banki hii imefikia wateja zaidi ya 6M nchi nzima,karibu mara kumi zaidi.
Kuhusu Uzalendo & Uzawa Kunajambo la kujifunza kwa hawa wanawake watatu yaani Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, Spika wa bunge la JMT na IPU Mhe Dkt Tulia Aksoni na Mkurugenzi Ruth Zaipuna kwa namna wanavyoleta mabadiliko ya kasi kwenye taasisi wanazoziongoza,
Hebu tazama orodha hii ya faida kwa mabenki kumi ya Tanzania yaliyofanya vizuri katika robo ya tatu tu ya mwaka huu wa 2023 ndio utaelewa vizuri nachosema kuhusu huyu Mkurugenzi.
1. NMB Bank: TZS 398 billion
2. CRDB Bank: TZS 280 billion
3. Stanbic Bank: TZS 95 billion
4. StanChart: TZS 64 billion
5. NBC Bank: TZS 62 billion
6. Citibank TZS 44 billion
7. PBZ TZS 41 billion
8. Exim Bank TZS 40 billion
9. Absa Bank TZS 37 billion
10. KCB Bank TZS 35 billion
Taarifa zinaonesha faida ya Jumla kwa mabenki yote Tanzania ni shilingi trilioni moja katika robo hii ya tatu, Hii ni sawa na kusema NMB PLC pekee anamiliki 40% ya faida yote huku ikimpiku kwa mbali mshindani wake wa karibu CRDB bank kwa zaidi ya TZS 118 BL sawa na 70% ya faida yake.
Wakati Ruth Zaipuna anakuwa Mkurugenzi Mkuu Benki hii ilikuwa na wastani wa faida ya TZS 200BL baada ya kodi wakati Leo faida imekuwa na kufikia wastani wa karibu TZS 400BL kwa mwaka yaani sawa na marambili zaidi.
Pia, taarifa zinaonesha Benki ya NMB inashika nafasi ya sita kwa Ukubwa katika nchi zote Kusini mwa jangwa la Sahara na ndio Benki pekee toka Tanzania inayoshindana kimataifa katika ukubwa wa Biashara.
Watanzania tuna la kujivunia toka kwa Mkurugenzi huyu mzawa akisaidiwa na management nzima ya NMB PLC pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wa NMB PLC chini ya Dkt Edwin Mhede, Hakika Mmestahili Heshima.
Kwa msiofahamu Mwaka 2021, Benki ya NMB chini ya Ruth Zaipuna ilitambuliwa na kutunukiwa tuzo saba za kimataifa
ikiwemo tuzo ya Euromoney ya Ubora, ikiitambua benki ya NMB kama Benki
bora Tanzania (kwa miaka tisa mfululizo) na tuzo kutoka Jarida la Global
Finance ikiitambua benki ya NMB kama benki salama zaidi Tanzania.
Pia mwaka 2021, benki ya NMB ilitambuliwa na kupewa tuzo na Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) ikiitambua kama mlipa kodi mkubwa zaidi kwenye
sekta ya fedha na pia mlipa kodi mkubwa namba tatu kwa ujumla nchini hii ni chini ya Ruth Zaipuna.
Kwa matokeo haya, Huenda Ukimwacha Rais Dkt Samia na Spika Dkt Tulia mwingine ni huyu Ruth Zaipuna wa NMB PLC deserves better.
BangiMwigulu na bagia unachagua nini
Ahaa unacagua bangi sioBangi
Asishauriwe kuingia kwenye sihasa yaani atachafuka fastaaaa
Huyu apewe uwaziri tu itapendezaHuyu Mama namkubali sana, Hana mchezo na kazi
Kaolewa na watoto kibaoNa hajaolewa eti!
Ni kweli kabisa Kimei kule bungeni na jimboni kapotezwa mazima...Ingekuwa analysis nzuri kama ungesema as compared to what? Maana banking industry yote ya Tanzania miamala ya ATM, mobile banking, branches zimekua zaidi ya mara mbili!! Yaani hata Maendeleo bank imekua zaidi ya Mara mbili ilihali ina assets ndogo zaidi.
Yes ilikuwa na assets nyingi miaka na miaka wala sio sababu ya
Analysis ya faida za kibenki hatupimi kwa billion hizi na hizi, maana obvious mtaji ukikua lazima faida ikue. So huwa wanapima kwa return on assets, au return on equity, sasa tukienda huko ndio ungetupa picha kamili kwamba kwa kila ongezeko la mtaji je kazalisha shingapi. ROA, ROE, au NIM.
Yeah apewe pongezi kwa kumaintain ukubwa wa NMB lakini kama mnamfanyia branding ili ateuliwe na Mama samia kwenye siasa mtampoteza. She might be good sababu ya ukubwa wa taasisi ila mkimpeleka sijui wizara ya uchumi, au sijui biashara na viwanda she'll be exposed of her weaknesses na atapoteza status yake.
Waacheni wabaki kwenye corporate world wana mchango mkubwa huko ila kwenye siasa atakua kama Kimei au Muhongo
Jibu hoja kwa facts...Naona umetumwa na CRDB hahaha
Ongezea na NMB MPANDA, KATAVI ni shidaa...Hongera lakini hili linamchafua...
Kuhusu suala la foleni kwenye matawi Yao unakuta madirisha matatu lakini moja tu linamhudumu. Kitendo hiki kinapelekea foleni ya saa 1-2 kusubiri huduma.
Reference Nmb Msamvu, Nmb Masika, Nmb Wami Morogoro. Hii inafikia mahala mtu ukiwa na suala lako la kibenki (lisilowezekana online) ujiandae kukumbana iyo foleni.
Pengine imechangiwa na kuongeza matawi pasi na kuongeza wafanyakazi. Bank za Mjini katu hazifai kuwa mhudumu mmoja (Teller).
Barua tuu 59,000/=???CRDB wana nyodo sana, hata ukitaka huduma mfano nilitaka kuandikiwa barua ya kupeleka kwa mwajiri wangu mpya. Barua ilikuwa inahusu mwenendo wa account yangu, walinitoza 59,000/= eti service fee wakati Mimi ni mteja wao miaka nenda rudi. Ninatabili CRDB itakimbiwa na wateja wengi.
Cc Mpwayungu VillageBila Walimu hakuna Bank hapo...
Nasisitiza bila Walimu hakuna bank hapo....
Pongezi kwa Walimu.