No referendum for ZNZ; Yes for Unity Government!


CCM wanajua lazima washinde urais siku zote, makamo akiwa CUF, rais anakuwa CUF ni kurudi kule kule...
 
Matatizo ya muungano yanajulikana. Na hata siku moja hayatakwisha kwa referendum (hata ziwe ngapi). Kinachotakiwa ni kuyatafutia utatuzi matatizo hayo kwa ukweli, uwazi na nia njema kabisa na haraka sana.

Siamini kuwa ZnZ ina nia ya kuuvunja muungano. Vile vile siamini kuwa Tanzania bara ingependa muungano uvunjike. Bali naamini kwa dhati kabisa kuwa, kama matatizo yaliyopo hayatapatiwa utatuzi wa kudumu, suluhu pekee litakuwa kuuvunja muungano, na ikiwezekana kuunda upya.

Muungano tulionao ukivunjika hakuna atakaefaidika, si bara wala visiwani. Ila matatizo yaliyopo yasipotatuliwa, hakuna atakaeweza kuuzuia muungano usivunjike. Uamuzi uko mikononi mwa watawala. Waamue kama wana nia thabiti ya kuulinda muungano au kuuachia ufe. Vyovyote iwavyo ni lazima maamuzi magumu yafanyike.
 
asante sana mkuu kwa kutu update,ila ujasema baadhi ya watu kama Shemhuna wakoje?na unaonaje upopo wa kisiasa upoje hapo?
 
Asante sana Pasco kwa kazi nzuri.

Nahisi mawaziri wanachangia sana hii hoja maana wanajua ikiwepo serikali ya mseto kabla ya uchaguzi, wao ndio watakaokosa ulaji kupisha mawaziri wapya!
 

Am interested with dondoo na 2.Mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa...nasubiri kwa hamu sana.
 
Kwa hiyo wanaombwa kuridhia maridhiano ambayo hata hawayajui?? Nafikiri ni muda muuafaka kuwaita Karume na Seif waje waeleze hayo maridhiano yao. nafikiri Karume na seif walitaka kuwatega wawakilishi ila janja inastukiwa. Can't wait for the CC on Sat and NEC on Mon.
 
Oh yeah...kule Canada walifanya referendum kuhusu Quebec....na baada ya hapo ndio ikawa vurugu mechi. Kila jimbo likaanza kudai referendum....British Columbia walitaka...Nova Scotia walitaka, Ontario walitaka....aaaah basi ikawa vurugu mechi kabisa! Sisi wabongo hatuwezi ku afford hizo vurugu mechi
 
asante sana mkuu kwa kutu update,ila ujasema baadhi ya watu kama Shemhuna wakoje?na unaonaje upopo wa kisiasa upoje hapo?
.
Shamhuna always anasmile, ameshaambia he is next, na siasa za ZnZ ni fitna sana, huku akifurahi na kujipa moyo kumbe kila mmoja kaambiwe ni yeye, Huku Khatib akisubiri, Dr. Mwinyi akiamini uraisi ni haki ya watoto wa maraisi kama alivyo Balozi Karume. Naye Nahodha ndiye wa pili wa Karume anajua ndiye yeye. Dr. Bilal baada ya kufanyiwa mtimanyongo mara mbili, hii kwake ndio last chance basi tuu huku mambo si mambo, ilimradi.
 
@Pasco
Thanks for the updates...couldnt live without your help on this one. 😀
 
Mseto ni sawa. Lakini sio kama huu ambao wanadai CUF wanaupendelea. Kama wapiga kura wamepiga kura kuchagua CCM kushikilia kiti cha Urais, na ukawa na Makamo mmoja (atakayetokea CUF), Mathalani Rais amefariki katika kipindi cha chini ya miezi sita baada ya kushika madaraka. Jee CUF (kwa maana ya Makamo wa Rais) apewe satuwa ya kushikilia Urais. Jee unawaaqmbia nini wapiga kura (walio wengi) ambao wamechagua CCM katika Urais kwa muhula huo wa miaka mitano? Wapi Demokrasia hapo?
 

Usilaumu wapinzani wakati wote, kwani mfumo uliopo hautowi haki sawa na walio madarakani wanataka uendelee hivyo kwa kutumia madaraka waliyonayo ili wandelee kuimiliki nchi na watanzania. Binafsi nawapongeza sana walio upinzani kwa effort wanazozifanya mpaka wakati huu japo hawajafanukiwa sana na wapambana challenge za wenye madaraka na fedha chafu lakini shughuli zao zinaonekana
 

Kweli kabisa, kuridhia mambo usiyoyajua ni sawa "kuuziana mbuzi kwenye gunia!"
 


shamkuma na Urais sijuwi ya mungu ni mengi.
 
"4. Baraza lifanye marekebisho ya vifungu vya 39, 42 na 62 ili kuweka utaratibu wa serikali ya Umoja wa kitaifa."

Kwa faida a yote hivi vifungu vina semaje haswa? Ili wote tujue ni nini haswa kina taka kufanyiwa marekebisho.

1. Ibara ya 39: Inahusu Ofisi ya Waziri Kiongozi wa Zanzibar na kazi zake.
2. Ibara ya 42: Inahusu Wizara za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
3. Ibara ya 62: Kazi za Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya.
Nimetumia Toleo la Katiba ya Zanzibar, 1984, linalojumuisha marekebisho yote ya Katiba ya Zanzibar tokea ilipoanza kutumika tarehe 12 Januari, 1985 hadi tarehe 17 Julai, 1995.
Kama kuna marekebisho yoyote yaliyofanyika tangu tarehe 18 Julai, 1995 hadi sasa kuhusu vifungu hivyo naomba yawekwe hapa ili tujadili kitu ambacho ni current! Naomba kutoa hoja!
 

Hawa CCM wajajanja hapo kwenye referundum ndiyo mchezo ulipo. Hivi sasa wanajaribu kutuliza mambo wewe subiri CUF wakubali kuwa serikali ya umoja wa kitaifa ije baada ya uchaguzi then baada ya uchaguzi utasikia kilio.
 
Hawa CCM wajajanja hapo kwenye referundum ndiyo mchezo ulipo. Hivi sasa wanajaribu kutuliza mambo wewe subiri CUF wakubali kuwa serikali ya umoja wa kitaifa ije baada ya uchaguzi then baada ya uchaguzi utasikia kilio.


Hapana mzee kama BLW likipitisha serikari ya mpito ikawa kwenye katiba hata kama baada ya uchaguzi CCM itacheza faulo kilio cha CUF kitakuwa na mshiko tofauti na wakati wa mwafaka wa kwanza walipodanganywa wasubiri kuingizwa serikalini
 
Am worried, Hivi hakutakuwa na mizengwe kwenye kura za maoni? serikali ikacheza rafu ili kuonyesha kwamba wazanzibari wengi hawaitaji mseto, nini kitatokea kwa upande wa CUF!!! Nahisi kuna ujanja wa kimafia hapa. tusubiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…