Nombeni Msaada: I think jamaa kaniroga

Nombeni Msaada: I think jamaa kaniroga

Msipende kupanda usafiri ambao sio public jaribuni kuwa wavilivu wanawake nyie hizo bajaji zinamatukio mengi. Mimi hua sipandi angalau boda

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
It's more likely un healed wound or dirty wound or chronic wound. Usi judge. Also it will disappear after a while. umelogwa nini?? Tembea in hospitals ujionee how things are.
 
Samahani msaada, tafsiri ya haya maneno
"Mida ya udubu"
"Abiria walikuwa weusi kishenzi"
 
Daah sipat picha muonekan wako mleta uz ukoj¿
maan unav andika mtu mwenye busara zake hawez kukuelewa kabisa.
 
Jana mida ya udubu nlikuwa naskilizia (dala)x2 nidandie kwenda Mwenge, Manyunyu yalkuwa yanakishi na dalili zlkuwa znaonesha soon kama sio hivi karibuni itakunya.

Ikaja bajaji chap jamaa anataka Buku atukimbize fasta, ila pale kituoni abiria walikuwa weusi kishenzi…wakakaza

Mi nkaona njitusu tu kwani jero shingapi hadi ulowe?
Nikaingia nkakaa ile siti ya nyuma peke yangu, tukawa tunaendelea kuskilizia abiria wa kuja kumalizia izo siti 2.

Akaja jamaa mmoja amevaa msuli akakaa pembeni yangu, tukawa mtu bee pale nyuma..


Tatizo likaanza sasa baada ya yule jamaa kukaa pale,yani harufu fulan ikatanda bajaji nzima kama kuna mbwa kafia mule,yani unaziba pua hamna tofauti na usipoziba mpaka machozi yanatiririka.

Nkaanza kujiuliza nini hiki? Au jamaa ametoka kutahiriwa nini? Lakini mbona kama jamaa ni mtu mzima 40+? Kwanini kavaa msuli unatema hivi?

Nikataka kushuka ila yule jamaa wa bajaji akawasha akimbize bajaji, sasa sijui alifanya vile kuniwahi kabla sjashuka au alifanya vile ili tuwahi kufika mwenge kabla hatujafia mle, maana aliondoka chap sana bajaji ikiwa na watu wawili 2.

nkataka kumwambia asimame fasta nshuke, ila nkahisi utakuwa kama unyanyapaaji kwa binadamu mwenzangu nkaamua nivumilie kibingwa.

Aisee kumbe nmetomber moto, leo ni siku ya pili bado naisikia ile harufu,nikilala nahisi mashuka yangu yametapaka hiyo harufu hata nguo mpya natoa kwenye begi nikiivaa nahisi ina ile harufu.

Nimefua nguo zote na kufanya usafi kwangu lakini bado naisikia.

Sasa swali kwenu waungwana,hii harufu ipo kichwani mwangu tu, is it just in my head au jamaa ameniroga baada ya kuona pale nlitaka kushuka?
Huyo alikuwa mchawi na yawezekana amekufanyia uchawi wa nuksi ukataliwe na kuchukiwa na watu.

Fanya maombi kama unajua kuomba kwa Mungu Aliye Hai au mtafute mtumishi wa kweli wa Mungu akuombee avunje uchawi huo kwa Jina la Yesu.
 
Daah sipat picha muonekan wako mleta uz ukoj¿
maan unav andika mtu mwenye busara zake hawez kukuelewa kabisa.
Kama mwenye busara haelewi lakini asiye na busara anaelewa…Je ni nani kati ya hao atakuwa na busara?
 
Kuna mavitu yanaitwa Donda ndugu hayo madonda hayaponagi na yanatema harufu inakarahisha sana halafu inakua kama ina gundi yani ukikaa nae karibu harufu inakunasa
 
Nadhani harufu ilikuwa ni kali sana kiasi kwamba imekukaa kichwani. Hii hali inaweza kukukuta hata kwenye vyakula pia. Unakula chakula aidha kimepikwa vibaya kikakuchefua siku ukikiona unapata kinyaa unatamani kutapika.

Namna ya kurekebisha inabidi ule chakula kizuri ambacho hakina dosari ili kuondoa ile dhana ya chakula kuwa kibaya kwako.
 
harufu umeshaipata bado kuvaa msuli tu hapo
 
Back
Top Bottom