Nuremberg trials

Acha ujinga wewe
 
Reading this with great awe and wonder....
 
USSR na baadaye Russia ina historia ndefu ya mauaji ya kimbari kwa maana halisi ya mauaji ya kimbari mfano ni mauaji ya Stalin ya njaa ya kutengeneza ya Holodomor ya Ukraine. US kupiga nyuklia Hiroshima na Nagasaki wakati wa vita sio mauaji ya kimbari, labda tunaweza kuita ni uhalifu wa kivita.
Jielimishe zaidi kuhusu genocide.

Allies hawakafikishwa kwenye mahakama za Nuremberg kwa sababu ile ilikuwa mahakama maalum kwa ajili ya Wanazi kwa makosa dhidi ya ubinadamu waliyofanya kabla na wakati wa vita, kumbukua Wayahudi walianza kuuwa na Hitler hata kabla ya vita kuanza.

Pia fahamu mahakama ya Nuremberg huundwa kwa sababu inaonekana jeshi na mahakama za nchi husika haziwezi kuwawajibisha raia na wanajeshi wake waliohusika na uhalifu wa vita au genocide. Ilitegemewa majeshi ya Allies yalikuwa na uwezo wa kuwawajibisha wanajeshi wake waliohusika na uhalifu wa kivita.
 
Japan wahalifu wakivita waliundiwa Tokyo trials.Wakina Hideki Tojo walihukumiwa hapo.Siyo kila mhalifu wa NAZI alipewa justice kama ilivyokusudiwa ,,wale wanasayansi wabobezi walichukuliwa na kufutiwa mashtaka na ndiyo msingi wa tekinolojia ya ya Urusi na USA.
 
Bali...
Maarufu ni Werner von Braun aliyewezesha Marekani kutua mwezini.
 

Sasa wewe kwa akili yako unaamini kulikuwa na mauaji ya kimbari dhidi ya Mayahudi au ni propaganda tu? Hivi kwa population ya Mayahudi kipindi hicho wangeuawa milioni tano kungekuwa na Myahudi aliyesalia duniani hivi sasa? Kama kuna ukweli mbona hakuna tume yoyote huru iliyoundwa kuchunguza jinai hiyo na kila anayetaka kuchunguza au kuzungumza kinyume anawekewa vikwazo? Kuna Gypsies na Roma pia waliuawa kwa maelfu wakati wa WW2 mbona wao hakuna anayewazungumzia zaidi ya Mayahudi? Sipingi kuwa Mayahudi waliuawa kwenye WW2 lakini si kwa kiwango kinachosemwa ni propaganda tu hizo ili kulinda maslahi ya Mayahudi.
Pili, nikukumbushe tu kuwa Nuremberg trials hazikuwa tu kwa mauaji ya kimbari bali mashtaka mengine kama crimes against peace, crimes against humanity and war crimes yalisikilizwa ambapo pia Allies committed such atrocities. Mahakama ya Nuremberg ilikuwa ni victors justice against the vanquished.
 
Fahamu mahakama ya Nuremberg huundwa kwa sababu inaonekana jeshi na mahakama za nchi husika hazina uwezo wa kutosha na wa kuaminika kisheria kuwawajibisha raia na wanajeshi wake waliohusika na uhalifu wa vita au genocide .
Ilitegemewa majeshi ya Allies yalikuwa na uwezo wa kuwawajibisha wanajeshi wake waliohusika na uhalifu wa kivita.
 
Israel nao wakaja na kikosi chao wenyewe avengers wakawa wanaenda nchi moja baada ya ingine na kuwaua mmoja moja na Kuna mmoja walimteka Heichman walimteka toka amerika ya kusini na kumpeleka Israel na kumnyonga baada ya kumfungulia kesi mahakamani
 
Nitajie hata kesi moja wanajeshi wa ushirika (allies) walishtakiwa kwa uhalifu wa kivita walioufanya. Kumbuka pande zote mbili Allies na Axis of Power walifanya ukatili mkubwa na uhalifu lakini walioshughulikiwa ni wa upande mmoja tu. Pia, kule Japan Gen. Douglas MacArthur aliwakingia kifua wahalifu wa kivita wa Japan akiwemo Mfalme Hirohito, familia ya kifalme na baadhi ya watu wazito ambao aliona kama wangeshughuliwa Marekani ingeshindwa kutawala Japan kwa amani (occupation). Matokeo yake lawama zote akashushiwa Gen. Hideki Tojo. Soma kazi za revisionist historians kama David Irving ndiyo utapata facts badala ya kutegemea sources from the victors alone.
 
Ukianzisha vita na ukashindwa lazima ulipe gharama.Adolf Hitler kosa lake ni kianzisha vita na kukiuka sheria za kimataifa.Stalin na Mao waliua watu wengi lakini wao hawakuanzisha vita.
 
Mfalme Hirohito aliachiwa kwakuwa alikubali kujisalimisha baada ya madhila ya Hiroshima na Nagasaki lakini pia yeye alishaachia madaraka ya kiutendaji kwa mawaziri wakuu wakina Tojo.Majeshi ya washirika hayakuwa majeshi ya wavamizi wavamizi ni Axis powers.Allied powers waliingia vitani baada ya aggression ya Axis powers.Kibaya zaidi ni kushindwa vita kwa kuwa the winner takes everything.
 
Hata Italy ya Mussolini ilikuwa na Mfalme Victor Emmanuel ila alikuwa ceremonial tu.Emperor Showa aka Hirohito hakuwa na madraka ya utendaji.Hirohito aliaga kwa amani kabisa 1989.
 
Na wale wana ufalme wengine waliohusika na mauaji makubwa kule China na wenyewe unasemaje?
 
Hata Italy ya Mussolini ilikuwa na Mfalme Victor Emmanuel ila alikuwa ceremonial tu.Emperor Showa aka Hirohito hakuwa na madraka ya utendaji.Hirohito aliaga kwa amani kabisa 1989.
Lakini kumbuka huyo Mfalme alimfukuza kazi Mussolini kama angekuwa hana mamlaka aliwezaje kumfukuza kazi?
 
Lakini kumbuka huyo Mfalme alimfukuza kazi Mussolini kama angekuwa hana mamlaka aliwezaje kumfukuza kazi?
1943,Italy ilikuwa imeshindwa karibu kila pahala na ulishatokea mgawanyiko kwa raia na jeshi.Walitokea waasi dhidi ya Mussolini,pale ndo mfalme constitutional akamfukuza kazi Mussolini lakini mwamba aliendelea kupambana hadi akauwawa.Mfalme kikatiba alikuwa mkuu wa nchi kama ilivyo Uingereza ila hakuwa mkuu wa serikali.Baada ya kuona Kuna haja ya kusign ceasefire akaamua amuondoe Kwanza IL duce Mussolini.Hiyo ni baada ya Baraza kuu la chama cha kifascist kupiga kura ya kumkataa
 
Hata Italy ya Mussolini ilikuwa na Mfalme Victor Emmanuel ila alikuwa ceremonial tu.Emperor Showa aka Hirohito hakuwa na madraka ya utendaji.Hirohito aliaga kwa amani kabisa 1989.
Heads of state anayeruhusu nchi kuingia kwenye mikataba ya kujihami (Military Alliances), atakuwaje hahusiki na vita. Mfalme Hirohito alihusika sana na vita na yeye mwenyewe alikiri hivyo kwasababy ndiye aliruhusu Japan ijiunge na Wanazi.

Aliachwa bila kuwajibishwa kwasababu za kimkakati. Hata babu yake Shinzo Abe aliyekuwa waziri mkuu wa Japan, alishitakiwa na mahakama ya Tokyo kama class A Criminal, lakini baadae akatolewa na kuwa Wazir Mkuu. Jina lake ni Nobusuke Kishi hebu mtafute....

Kuna kitu hakipo sawa hapa kuhusu Hirohito. Siku zote katika jinai sheria inatoa kitu kinaitwa Command Responsibility ambapo mtu wa juu anawajibishwa kwa makosa ya watu walio chini yake, hata kama hakuwepo eneo la tukio. Sasa utasemaje hawajibiki ????

Lakini zaidi, chini ya katiba ya Japan (The Meiji Constitution), mfalme wa Japan ndiye alikuwa mtawala mkuu wa nchi (Supreme Ruler) ambapo jeshi na sera ya mambo ya nje vilikuwa chini yake. Hata Waziri Mkuu alikuwa chini yake.....
 
Kwa nini wayahudi walikuwa wana uwawa?

Haiwezekani waiwawe tu bila sababu za msingi?

Kosa lao lilikuwa ni lipi?

Kwa nini mpaka sasa wayahudi hawapendwi huko mashariki ya kati na sehemu zingine duniani? Tatizo lao ni nini?
Shida ilianza walipomuacha Solemba Farao kule Egypt. Sababu walipendelewa kujua elimu fulani adimu, waliishi kama ni watu special. Wanafanya kazi sana. Wabunifu sana. Wanafuata culture na dini yao sana. Sisi watu wa mataifa hatupendi hizi akili nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…